Kenya 2022 Nimejifunza mambo matano kwenye Uchaguzi Mkuu wa Kenya

Kenya 2022 General Election

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,365
8,098
Uchaguzi Mkuu wa Kenya umefanya nijue umuhimu wa utawala wa sheria na Katiba hasa kwenye masuala muhimu ya kusimamia haki za msingi za wananchi.

1. Hakuna Kupita bila Kupingwa
Kenya imeonesha kuwa wananchi ndio waamuzi wa mwisho wa nani wanataka awe kiongozi wao na si vinginevyo

2. Mtandao Haukuzimwa (No VPN Needed)
Licha ya msuguano mkali wa wagombea pia kutofautiana kwa Naibu Rais Ruto na Rais Kenyatta hakujafanya serikali ya nchi kuzima mitandao, kila traarifa zinapatikana bila matumizi ya VPN.

3. Majukumu ya Vyombo vya Dola (Kulinda usalama wa Wapiga Kura na zoezi hilo)
Tumeshuhudia kwenye baadhi ya nchi majeshi yakitumika kuingilia mchakato wa Chaguzi ikiwa ni pamoja na kukamata wapiga kura wa vyama vya upinzani, lakini kwa Kenya hali imekua tofauti, Wakenya wanapiga kura kwa uhuru na kulindwa katika kutimiza haki yao ya kikatiba.

4. Wagombe Binafsi Kushiriki Uchaguzi
Hili ni kati ya mambo ya kipekee kabisa kwa nchi za Afrika Mashariki ambapo wagombea binafsi wasio na vyama vya siasa wameshiriki uchaguzi na kupigiwa kura bila shida yoyote.

5. Umuhimu wa Tume Huru ya Uchaguzi
Moja ya masuala muhimu kwenye demokrasia ni pamoja na kuwa na chombo kinachoamua na kuendesha michakato ya uchaguzi. Kenya ni kati ya nchi chache za Afrika zilizofanikiwa kuacha suala la uchaguzi liendeshwe na Tume Huru ya Uchaguzi ambayo haiingiliwi na mamlaka yoyote kwasababu viongozi na wafanyazi wake hawawajibiki kwa mamlaka nyingine isipokua Tume ya Uchaguzi.

Uwepo wa Tume Huru unaondoa mambo mengi kutokea ikiwemo wizi wa kura au upendeleo kwa wagombea wa upande wowote.
 
Natamani kuhamia Kenya aisee...daaa jamaa wako mbali sana.Hadi Raha the way wanafanya mambo Yao huchoki kufatilia. Hongera sana kenya
 
Uchaguzi Mkuu wa Kenya umefanya nijue umuhimu wa utawala wa sheria na Katiba hasa kwenye masuala muhimu ya kusimamia haki za msingi za wananchi.

1. Hakuna Kupita bila Kupingwa


2. Mtandao Haukuzimwa (No VPN Needed)


3. Majukumu ya Vyombo vya Dola (Kulinda usalama wa Wapiga Kura na zoezi hilo)


4. Wagombe Binafsi Kushiriki Uchaguzi


5. Umuhimu wa Tume Huru ya Uchaguzi


Uwepo wa Tume Huru unaondoa mambo mengi kutokea ikiwemo wizi wa kura au upendeleo kwa wagombea wa upande wowote.
Hongera sana
 
Uchaguzi Mkuu wa Kenya umefanya nijue umuhimu wa utawala wa sheria na Katiba hasa kwenye masuala muhimu ya kusimamia haki za msingi za wananchi.

1. Hakuna Kupita bila Kupingwa


2. Mtandao Haukuzimwa (No VPN Needed)


3. Majukumu ya Vyombo vya Dola (Kulinda usalama wa Wapiga Kura na zoezi hilo)


4. Wagombe Binafsi Kushiriki Uchaguzi


5. Umuhimu wa Tume Huru ya Uchaguzi



Uwepo wa Tume Huru unaondoa mambo mengi kutokea ikiwemo wizi wa kura au upendeleo kwa wagombea wa upande wowote.
Kimsingi uchaguzi umekuwa rahisi kuusimamia kwa kuwa watu wengi hawakujitokeza kupiga kura. waliopiga kura ni kama 44% na ndio wanafuatilia; inamaanisha raisi wa mwaka huu anaweza kuchaguliwa na kama 18-22% ya wapiga kura. Ukumbuke kwenye hiyo 44% kuna millions ya kura zimeharibika. Sinahakika kama TUME imefanya kazi yake vizuri au wananchi wamejikatia tamaa
 
Ccm Hapa Wanapita Wakisonya Na Kutema Mate Pembeni Kabisa
Hawana Wanachijifunza Zaidi Mipango Ya Hovyo, Fitna, Chuki, Ghiriba, Umimi. Yaani Wanataka Wao Tu Wafanye Watakavyo
 
Hayo mambo 5 yanawezekana kwenye mataifa yenye watu wastaarabu na wenye akili, siyo vinchi vilivyojaa wanafiki, wasiojielewa na wajinga
 
Uchaguzi Mkuu wa Kenya umefanya nijue umuhimu wa utawala wa sheria na Katiba hasa kwenye masuala muhimu ya kusimamia haki za msingi za wananchi.

1. Hakuna Kupita bila Kupingwa


2. Mtandao Haukuzimwa (No VPN Needed)


3. Majukumu ya Vyombo vya Dola (Kulinda usalama wa Wapiga Kura na zoezi hilo)


4. Wagombe Binafsi Kushiriki Uchaguzi


5. Umuhimu wa Tume Huru ya Uchaguzi



Uwepo wa Tume Huru unaondoa mambo mengi kutokea ikiwemo wizi wa kura au upendeleo kwa wagombea wa upande wowote.
Supreme court ya Kenya iliweka mazingira mazuri kwa uchaguzi wa kenya. Tume huru ya uchaguzi ilielekezwa kuwa uchaguzi lazima uzingatie vigezo vifuatavyo:
1. Free and fair election
2. Every vote must be verifiable.
3. All stages of election from voting, counting of votes, verifying of votes and announcement of results must be extremely transparent!

Lakini pia hofu ya mahakama ya THE HAGUE imesaidia sana wagombea kujilinda na uanzishaji wa vurugu!
 
Back
Top Bottom