Nimejifunza kutokufata mkumbo wa biashara inayofanywa na mtu

Balo za jeans zimefawanyika kama ifuatavyo
☆ jeans men
Hizi ni kuanzia size 28 kuendelea wanavaa kuanzia wakubwa kuendelea
Namba 1 bei yake ni laki 5
Namba 2 bei yake ni laki 2½
Zinakaaa peace mia za jeans

☆ladies
Hizi ni jeans mchananyiko za kike na kiume mara nyingi ukinunua hii unakutana na modo za vijana kuliko ukinunua jeans men utakutana na ma bwanga ijapokua inategemea mzigo ni kutoka taifa gan ila kwa experience yangu mzigo wa china na Korea hua mzigo mzuri,
Namba 1 ni laki 5
Namba 2 ni laki 2½

☆ alafu kuna boypant
Hii ndo ninayoiuza mimi humu utakutana na jeans kwanzia watoto wa miaka 8 mpka miaka 18 iv
Namba 1 ni lak 5
Namba 2 ni laki 2½
Hizi zinakaa 125
Kama unauzia kijijini nunua namba 2 km unauzia town nunua namba 1

Kwangu mimi hii biashara naona ina faida kama utakua na boypant na ladies, pia kuna jeans kali utakutana nazo ambazo utauza bei zaidi, na hizi bei ni kwa dodoma

Pia kila balo linajina lake ukitaka kununua tafuta duka watakalokupa details za kutosha ujue ni kitu gani unakwendaa kukutana nacsan,
Safi sana
 
Shida sio kuwa na mauzo mengi, swala ni je unapata faida ya shi ngapi?

Maana usije kuta unajipa moyo kumbe mwenzako anapata faida kuliko wewe.
Anaweza kuwa anauza nguo mbili kwa 10K lakini faida alfu mbili kwa nguo zote.

Mwenzake anauza vitu vya alfu 10K alafu faida ni alfu 6.

Biashara inataka mahesabu makali sana.

Biashara inataka usijilinganishe na wengine.

Biashara inataka uige kwa wengine

Ila nampongeza mtoa mada lakini asiache kujifunza
 
Nadeal na Urembo Asikwambie mtu urembo una faida Mara mbili ya mtaji kuna bidhaa moja Nilinunua 3000 nikauza 10,000/= na zilitembea kama njugu mpaka nikatamani kuuza 15000

Nina Wasiwasi rafiki yako alikupa info za uongo
 
Hata katika faida pia me nimemzidi mfano mimi nanunua robota moja laki mbili na nusu linakua na jeans 125 nakua nimeuziwa kila jeans alfu 2000 kawaida nauza jeans alfu 5 faida yangu ni alfu 3 kwa kila jeans wakat yeye alfu 3 ataipata baada ya kumaliza ki pakti cha hereni chenye pair kumi za hereni
Hizo jinsi za laki mbili na nusu unanua wapi
 
Nadeal na Urembo Asikwambie mtu urembo una faida Mara mbili ya mtaji kuna bidhaa moja Nilinunua 3000 nikauza 10,000/= na zilitembea kama njugu mpaka nikatamani kuuza 15000

Nina Wasiwasi rafiki yako alikupa info za uongo
Urembo kama upi mr Liverpool
 
Mimi katika utafutaji wangu nishawahi kufanya biashala ya urembo na ni moja ya biashala ambayo ilikuwa inafaida Sana mfano nilikuwa nanunua pakiti yenye heleni 12 KWA sh 1000 ambazo nikiuza nilikuwa natoa sh 6000 kiujumla nilikuwa napata faida ya kutosha na moja ya biashala ambayo ilinifanya nikafungua duka la vipodozi maeneo ya Moshi bar kipindi hiko ola Mimi nilikuwa natembeza kwenye kapu japo ilikuwa na changamoto zake ila ni biashala ambayo ukitulia unapata faida ya kutosha tu kikubwa uangalie vitu ambavyo wanawake wanapenda
 
Urembo umegusa Maeneo mengi sana Mkuu mfano unanunua saa 3000 unauza 15000/=
Kuna saa Nilinunua 8000 nikaziuza 30,000/pc so Urembo Ni namna utakavyo ingia sokoni jicho lako likaona mahitaji ya soko.
 
Back
Top Bottom