Nimeitwa kwenye interview canada ila sina nauli.

Nyamuleha jr

Senior Member
Feb 20, 2013
185
65
Miezi miwili iliyopita niliaply kazi katika kiwanda kimoja cha usindikaji wa samaki wameniita kwenye interview tarehe 22january ila tatizo sasa sina nauli nimemwambia mzee auzee hata vishamba vyake na nyumba amekataa daa nishaurini nifanyaje nakama mnavyo jua bongo maisha magumu
 
Miezi miwili iliyopita niliaply kazi katika kiwanda kimoja cha usindikaji wa samaki wameniita kwenye interview tarehe 22january ila tatizo sasa sina nauli nimemwambia mzee auzee hata vishamba vyake na nyumba amekataa daa nishaurini nifanyaje nakama mnavyo jua bongo maisha magumu

Waombe wakufanyie interview kwa njia ya simu,,, We unataka uuze shamba hafu ukienda ukakosa wadogo zako watakula nini?
 
Pole mwanangu kweli taiti bongo cha kufanya kaongee na hata na mapadri wa kanisa watakusaidia uclale mwanangu humiza kichwa
 
jaribu kuwasiliana nao mapema sana kuwaomba wakufanyie intvw kwenye simu tu uongee nao maana hapo hakuna jinsi...usiuze shamba ndg yangu, je ukakosa na kazi yenyewe itakuwaje?
 
hongera.
nauli huna, hio visa utapata kweli?
Nijuavyo ili kupata visa lazima uonyeshe ka balance flani ka kuridhisha kwenye akaunti yako.
 
Why uliomba kazi huko wakati nauli huna?

inaitwa ku testi zali mkuu! sasa zali lime tick jamaa hana option b,c wala d.
Lakini nampa hongera kwa kujaribu! Hatuwezi jua anaweza pata hio nauli na ikawa bahati yake!
 
Hakuna interview siku hizi ya kusafiri hasa hasa nchi za nje, interview zote tunafanyia palepale ulipo either kwa simu au computer, ukionekana unafaa ndio unapewa letter of offer na unaanza taratibu za visa au work permit. wewe unatudanganya au la umeitwa na matapeli
 
hata kama si utapeli hiyo kazi hailipi, usiende hata kama ni kweli, hela ipo huku huku Afilika!
 
angalia mkuu kuwa makini na watu kama hao wengine ni matapeli tu ukifika kazi hakuna bali wanakulazimisha uwe shoga kwenye macasino, imesha watokea baadhi ya watu so fanya uchunguzi kwanza!
 
Mimi kuna emails kila kukicha wananitumia kuna nafasi za kazi,marriot hotel,canada..na bla bla kibao..huu ni mwaka wa tatu sasa still wananitumia tu hizo employment opportunities.....hao si kitu zaidi ya matapeli...anagali sana kaka...usije ukaenda kufanywa mtumwa na wakati kipindi cha utumwa kimeshapita.
 
Miezi miwili iliyopita niliaply kazi katika kiwanda kimoja cha usindikaji wa samaki wameniita kwenye interview tarehe 22january ila tatizo sasa sina nauli nimemwambia mzee auzee hata vishamba vyake na nyumba amekataa daa nishaurini nifanyaje nakama mnavyo jua bongo maisha magumu

Ndugu yangu huwezi ukapata mtu wa kukupa hela ndefu hivyo, kwani haina uhakika kama utafanikiwa kupata kazi au utaweza kuirudisha hiyo hela. Wewe omba interview ya kwenye simu au video conference. Vipo vituo vingi tu Dar km pale IFM kuna kituo cha video conference.
 
Miezi miwili iliyopita niliaply kazi katika kiwanda kimoja cha usindikaji wa samaki wameniita kwenye interview tarehe 22january ila tatizo sasa sina nauli nimemwambia mzee auzee hata vishamba vyake na nyumba amekataa daa nishaurini nifanyaje nakama mnavyo jua bongo maisha magumu

Kwanza huna nidhamu, mashamba ya baba yako unayaita Vishamba kweli? Kuwa na adabu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom