Nimependa Rais wa wanyonge anapochukua maamuzi magumu ili kuwavusha wanyonge!

Ni sawa....lakini!

Ukiangalia kwa undani na objectively, unaona kuna unafiki unafanyika au ni siasa za kilaghai tu. Nitafafanua.

Kodi inatozwa kwa kufauata sheria za kodi. Baada ya mwanzo Rais kutoa maelekezo, waziri alipeleka mapendekezo ya kubadilisha sheria za kodi. Kabla ya mapendekezo (mswada) ya kupelekwa bungeni, yanapita kwanza kwenye baraza la mawaziri (BLM) ambalo mwenyekiti wake sote tunamjua. Baada ya BLM mswada wa sheria unapelekwa bungeni. Baada ya mswada kupitishwa na bunge hauwezi kuwa sheria mpaka Rais akubali (accent). Kwa hivyo inashangaza sana (kama sio dharau kwa wananchi) mtu ambaye amehusika moja kwa moja na uwepo wa sheria hiyo (mbovu??) akiwa wa mwanzo kuilalamikia. Hakujua alichosaini? Ni wazi alijua kila kitu.

Tunaweza kuwalaumu TRA katika hili lakini kwa hakika anayepaswa kubeba hilo zigo la sheria mbovu ni waziri wa fedha, Bunge letu na zaidi Rais (kama kweli tunataka kuwa fair na objective). Maana kama Rais aliletewa sheria ambayo inaenda tofauti na maelekezo yake alikuwa na uwezo wa kuizuia ndani ya BLM kabla hata muswada haujaenda bungeni. Au la kapitiwa katika stage hivyo, angeweza kukataa kusaini. Mind you imeshapita karibia miezi 18 sasa tangia mabadiliko yafanyike.

Najua uchaguzi wa serikali za mitaa unakaribia kwa hivyo, kwa sisi wengine wenye makengeza sio vigumu sana kuona sababu ya hizi sarakasi zinazoendelea. Wengine mnayo haki ya kuoiga makofi na vigeregere.
Mkuu jambo la heri halina msimu wa uchaguzi!
 
tumepata chanzo kingine cha kodi.
670,000×20,000.
Ni pesa nzuri tu.
yaani hautumii nguvu MZIGO HUU HAPA.
 
Mwanzoni aliagiza kodi ya majengo iwe 10,000 lakini TRA kwa ujuaji wakaweka wathamini ambao wakifika kwako wanakadiria kila banda 10,000 na unaweza kujikuta unalipa hadi 40,000 kwa plot moja. Leo mkuu wa nchi amedisitiza tena ni 10,000 kwa plot bila kujali mabanda yaliyomo.
Na hii ya wajasiriamali ndio mkombozi, pale Tegeta Nyuki sokoni wale wa wanaouza vitu vidogo vidogo wanatozwa ushuru wa sh 1300 kwa siku sawa na sh 39000 kwa mwezi au 468,000 kwa mwaka. Na hii fedha sidhani kama inafika kwa mkurugenzi wa manispaa ya kinondoni nadhani inaishia kwa wale matumbo tumbo watatu wanaotoza ushuru. Lakini leo ukombozi umewafikia wajasiriamali hawa ambao wengi ni wachagga na sasa watalipa sh 20,000 tu kwa mwaka mzima.

Maendeleo hayana vyama....... CCM hoyeee!
Tofautisha kodi inayokusanywa na TRA (kozi) na Ushuru unaokusanywa na Halmashauri (Tozo). Hiyo 20,000 ni kodi ya faida unayopata kwa kufanya biashara na 1,300 ni tozo ya kutumia eneo la Halmashauri kufanyia biashara
 
Tofautisha kodi inayokusanywa na TRA (kozi) na Ushuru unaokusanywa na Halmashauri (Tozo). Hiyo 20,000 ni kodi ya faida unayopata kwa kufanya biashara na 1,300 ni tozo ya kutumia eneo la Halmashauri kufanyia biashara
Mbwiga umeambiwa ukishavaa kitambulisho chako usisumbuliwe na " yeyote" uwe unaelewa!
 
Ni mawazo yangu ila nimeshuhudia kwa macho na masikio.Baada ya kodi za majengo kuhamia TRA manispaa nyingi zimechukia na haziwapi TRA ushirikiano ukizingatia watumishi wa TRA ni wachache.hilo kichele hajaliona au ameogopa kulisema.
 
TRA mkajitathmini. Bado tunahitaji kudhibiti hiyo kidi ikashalipwa isiiishie kwa wajanja.
 
Magu yupo vizuri katengeneza income kiaina hapo amefikilia mbali sana
Kawanyanganya manispaaa kipato tena na watu hawajaona kuwa manispaa kodi walikuwa wanapata kwa machinga yeye kachukua kirahisi
 
Nchi ya ajabu Sana kodi ya Magari ni kubwa kuliko nchi zisizo na bandari sijui kwanini? Unanunua gari milioni kumi ushuru milioni kumi na mbili, TRA jipange umpya jamani.
 
Sisi wachagga wa soko la nyuki tegeta twasema yatosha Chadema bye bye sasa ni ccm mbele kwa mbele!

Hao wachaga wana mafanikio toka enzi za Nyerere, hawajawahi kuhitaji msaada wa rais aliye madarakani au aliyestaafu ili kufanikiwa. Na hawahitaji hisani yoyote ya ccm ili kufikia maanikio. Na hata Magu akitoka akaja rais yoyote na chama chochote hao wachaga wataendelea kuwa na mafanikio kwani mafanikio yao ni ya kigenetic zaidi.
 
Mwanzoni aliagiza kodi ya majengo iwe 10,000 lakini TRA kwa ujuaji wakaweka wathamini ambao wakifika kwako wanakadiria kila banda 10,000 na unaweza kujikuta unalipa hadi 40,000 kwa plot moja.

Leo mkuu wa nchi amedisitiza tena ni 10,000 kwa plot bila kujali mabanda yaliyomo.

Na hii ya wajasiriamali ndio mkombozi, pale Tegeta Nyuki sokoni wale wa wanaouza vitu vidogo vidogo wanatozwa ushuru wa sh 1300 kwa siku sawa na sh 39000 kwa mwezi au 468,000 kwa mwaka.

Na hii fedha sidhani kama inafika kwa mkurugenzi wa manispaa ya kinondoni nadhani inaishia kwa wale matumbo tumbo watatu wanaotoza ushuru.

Lakini leo ukombozi umewafikia wajasiriamali hawa ambao wengi ni wachagga na sasa watalipa sh 20,000 tu kwa mwaka mzima.

Maendeleo hayana vyama....... CCM hoyeee!

Unashabikia ujinga usiojua madhara yake..!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom