Mlabondo
JF-Expert Member
- Oct 13, 2010
- 223
- 129
Kama ni Azam wapigie watakusidia kuna jamaa aliibiwa kingamuzi jamaa aliyauziwa kikaharibika akapeleka azam kutengeneza.siku kimepona azam wanampigia mmiliki akachukue kingamuzi chake hivyo yule jamaa akashindwa kufuata kwasababu majini yake na mmiliki ni tofautiHabari wana jamvi,
Naandika nikiwa na jazba na hawa watu wanaoitwa wezi. Nimepanga geto langu nikajibana nikaeka vitu vyote vya ndani sasa hawa jamaa wamenilia time nimetoka wamenisafisha hadi kijiko ila kwenye vitu walivoiba wamebeba hadi king'amuzi.
Ila kuna mdau aliyeniambia king'amuzi kinatafutika kama ilivyo kwa simu.
Msaada jamani kwa mwenye ujuzi maana nikimpata mwenye king'amuzi ndio nitamtolea uvivu.
Nawasilisha