Nimeibiwa pikipiki usiku Aina ya sanlg ndani nahisi kufa

kesho kutwa

JF-Expert Member
Dec 7, 2016
1,628
1,786
Wakuu Leo Nina mwez na nusu Toka nimehamia mjini hapa biashara yangu bodaboda. Naamka asubui pikipiki sioni..

Mara ya mwisho mtu akiamka sa 9 aliiona pikipiki lakini cha Ajabu mlango umevunjwa pia.
Baada ya uchunguzi mfupi tu ni Kua Mwizi alipanda juu ya ukuta akashukia kwa ndani akaichukua pikipiki na kutoka nae getini.
Nje tumekuta kamba ya mnyororo tulihisi iliyotumika kuiburuza pikipiki.

Lakini pia Kuna mtu ndani usiku alisikia mtu anagonga lakini alihisi ni mtu yupo room kwake.

Kama Kuna mtu huku ndani anajua jinsi ya kuitraki pikipiki au namna ya kuipata aje anisaidie niweze ipata maisha yatakuja magumu sana hapa nilipo panga pamejaa simanzi Sana kwa tukio hiki. Sipigi picha kwa sababu za kiu salama lakini geti
limevunjwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana, upo mkoa gani hapo uripoti tu polisi kama utaratibu tu ila kuipata ni ndoto kwani watauza hata spare parts tu.
Kama unaamini kamati ya ufundi fanya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nilikuwa nasikia tuu mtu anaweza kuibiwa usingizini. ... kweli usingizi n i nusu ya kifo....harafu mbaya zaidi tukio lote ulikuwa unaliona kama ndoto vile....usingeidharau ile ndoto...piki piki yako ungeinusuru.
 
Hupigi picture kwa sababu za kiusalama wakati umeibiwa?weka picha hapa tuone hii inaweza kuwa inside job hao unaokaa nao hapo inawezekana kuna mmoja amekula mingo akakuchomea kwa wana waje kuchukua chombo upate tabu hapa town.

Mtu hawezi kuingilia juu akashuka chini akavunja mlango kwa ndani hizi nyumba za kupanga hawana kawaida ya kuweka vitasa vyenye funguo tatu huweka komeo ili kila mtu awe na uwezo wa kutoka na kuingia muda anaotaka so mazingira kama haya mwizi angefungua tu komeo siyo kuvunja mlango mlango umevunjwa ili kufanya uchunguzi kuwa mgumu.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Hupigi picture kwa sababu za kiusalama wakati umeibiwa?weka picha hapa tuone hii inaweza kuwa inside job hao unaokaa nao hapo inawezekana kuna mmoja amekula mingo akakuchomea kwa wana waje kuchukua chombo upate tabu hapa town.

Mtu hawezi kuingilia juu akashuka chini akavunja mlango kwa ndani hizi nyumba za kupanga hawana kawaida ya kuweka vitasa vyenye funguo tatu huweka komeo ili kila mtu awe na uwezo wa kutoka na kuingia muda anaotaka so mazingira kama haya mwizi angefungua tu komeo siyo kuvunja mlango mlango umevunjwa ili kufanya uchunguzi kuwa mgumu.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
Kweli naungana na wewe picha limechezwa humo humo ndani ya nyumba na wapangaji wenzake. Akipata mpelelezi mzuri mbona inapatikana hiyo. Mie mwenyewe niliposoma hiyo stori nikaona kabisa wapangaji wenzake wamemchorea ramani mwizi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom