Allency
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 13,466
- 12,916
Habari wakuu.
Moja kwa moja kwenye mada, Jumapili iliyopita ya tarehe 05/06/2022 mida kama ya saa 1 usiku kuelekea saa mbili nikiwa natoka Dar kwenda Morogoro ndani ya bus mali ya kampuni ya Frester nikaamua kushukia Chalinze na kusahau begi langu lenye computer na vitu vingine. Nikatafuta usafiri mwingine kwenda Moro ili kufatilia begi langu lakini mpaka nafika Moro nikakuta bus limefika muda mrefu sana na abiria wote wameshashuka na bus limepaki kimya kabisa.
Ikabidi niende ofisini kuulizia maana ilikiwa usiku tayari mida kama ya saa saba. Ofisini sikukuta mtu zaidi ya abiria waliolala wakisubiri kusafiri kesho yake. Narudi nyuma kidogo, ni kuwa baada ya kujua nimesahau begi nilipiga zile namba za simu za kwenye tiketi kama nne ndipo nilipompata muhusika kwani wengi walisema wameshaacha kazi kampuni ile.
Muhusika alipokuja mida kama ya saa kumi tukaenda kwenye bus na kukuta dereva kalala kwenye bus na akajibu kupitia dirishani kuwa hajaona hilo begi. Nikapata wazo la kwenda Polis, nikaja na Polis wa kike na dereva akafungua mlango tukaingia ndani kukagua, kweli hakukuwa na begi ila mkoba tu wa kike uliosahaulika pamoja na demu wa dereva kumbe walilala humo.
Hisia zangu zinaniambia kuwa dereva, demu wake na kondakta ndiyo wamechukua mbegi langu. Naombeni msaada wa kipi cha kufanya kupata begi langu kwani ni muhimu sana na niko tayari kwa njia yoyote ile na kulipa gharama.
Ikumbukwe pia kuwa mzigo wa ndani ni dhamana yako/yangu.
Moja kwa moja kwenye mada, Jumapili iliyopita ya tarehe 05/06/2022 mida kama ya saa 1 usiku kuelekea saa mbili nikiwa natoka Dar kwenda Morogoro ndani ya bus mali ya kampuni ya Frester nikaamua kushukia Chalinze na kusahau begi langu lenye computer na vitu vingine. Nikatafuta usafiri mwingine kwenda Moro ili kufatilia begi langu lakini mpaka nafika Moro nikakuta bus limefika muda mrefu sana na abiria wote wameshashuka na bus limepaki kimya kabisa.
Ikabidi niende ofisini kuulizia maana ilikiwa usiku tayari mida kama ya saa saba. Ofisini sikukuta mtu zaidi ya abiria waliolala wakisubiri kusafiri kesho yake. Narudi nyuma kidogo, ni kuwa baada ya kujua nimesahau begi nilipiga zile namba za simu za kwenye tiketi kama nne ndipo nilipompata muhusika kwani wengi walisema wameshaacha kazi kampuni ile.
Muhusika alipokuja mida kama ya saa kumi tukaenda kwenye bus na kukuta dereva kalala kwenye bus na akajibu kupitia dirishani kuwa hajaona hilo begi. Nikapata wazo la kwenda Polis, nikaja na Polis wa kike na dereva akafungua mlango tukaingia ndani kukagua, kweli hakukuwa na begi ila mkoba tu wa kike uliosahaulika pamoja na demu wa dereva kumbe walilala humo.
Hisia zangu zinaniambia kuwa dereva, demu wake na kondakta ndiyo wamechukua mbegi langu. Naombeni msaada wa kipi cha kufanya kupata begi langu kwani ni muhimu sana na niko tayari kwa njia yoyote ile na kulipa gharama.
Ikumbukwe pia kuwa mzigo wa ndani ni dhamana yako/yangu.