Nimehitimisha kwamba watu wasioamini uchawi upo hayajawakuta, na yakiwakuta huteseka bila kupona mpaka kifo

mkuu Hazard CFC ni ngumu kukuelewesha ukanielewa bt nakushauri jenga urafiki na watu wa afya kisha katika maongezi uwe unawaulize juu ya haya mambo, pia kitu kingine kama uliwahi shuhudia hata mazingaombwe wakati upo shule basi itatosha kujua kua uchawi upo.
Mazingaombwe zile ni acting tu mkuu..hata mimi najua some tricks zakubadili mchanga uwe pipi
 
Unaruhusa kuwaza kwa uhuru, lakini huwezi kupinga nguvu za giza kwa akili yako peke yake. Mambo mengi ya Kimungu na nguvu za giza mara nyingi sana hupingana ama huenda kinyume na logic ya kawaida ya mwanadamu, ndiyo maana wengine wanakataa havipo vitu hivyo. You cannot logically reason about the reality of the existence of God and the devil. Huwa zinakinzana na logic ya mwanadamu, kwa sababu ya ufinyu wa mawazo yetu. Imagine hata kwenye "electromagnetic spectrum," range ya miali tunayoweza kubaini kwa macho yetu tu ni ndogo sana -- visible light, basi. Sasa hatujui ni vitu vingi kiasi gani tusivyoweza kujua, na viko countless.

Kwahiyo chochote amacho hakina logical explanation au hatujui ni uchawi? Kwanini kisibaki kutojulikana mbaka hapo kitapojulikana badala ya kukimbilia ni uchawi au Mungu.
 
nimekwambia naamini mungu yupo,,,ila shetani jini sijui uchawi hivyo vyote siamini hata dhambi siamini kama kuna dhambi
Sidhani kama huamini kama Shetani ama dhambi havipo. Nadhani ukweli sahihi hapo ni kwamba hujui maana ya dhambi au Shetani. Kwa description ya kitu fulani kinaendana na uhalisia uliopo, kudai tena eti hakipo ni kuukana tu ukweli. The existence of the devil and sin is as real as our own presence, you can only deny it fruitlessly.
 
Mungu alietumba sisi binadamu naamin yupo,,ila izi mambo za uchawi mashetan majini malaika siamin kama vipo
Itabidi labda tuanzie hapo. Unamwamini Mungu kuwa nini nani!? (In short, huwezi kuamini kwamba Mungu yupo halafu ukashindwa kuamini kwamba Shetani yupo na kwamba wachawi wapo, unless hujui maana ya Mungu).
 
Kwahiyo chochote amacho hakina logical explanation au hatujui ni uchawi? Kwanini kisibaki kutojulikana mbaka hapo kitapojulikana badala ya kukimbilia ni uchawi au Mungu.
Umeninukuu vibaya. Nimesema generally uchawi ni counterintuitive, supernatural, beyond reasonable explanation. Ambacho sijasema ni kwamba kitu chochote ambacho ni counterintuitive, supernatural, beyond reasonable explanation ni uchawi. Kama utanielewa vizuri, uchawi ni subset ya "counterintuition, supernatural power, etc."
 
Huyo daktari ni wakumfukuza kazi kabisaa...

Dawa uliotumia haihusiani kabisa na uchawi ni dawa za kawaida kabisa za mitishamba zilizotumika na mababu zetu.

Mke wangu nae alipitiliza siku za kujifungua tukaenda hospital sikutaka maneno mengi nikaacha uchawi wa kizungu ufanye kazi,akala kisu chap mtoto katoka salama kabisa na mama yake akawa vizuri kabisa,ila ninge zubaa pale ningeanza kuletewa ngonjera za kua kafungwa na mambo mengine kibao ya kipuuzi
Kuna watu matapeli wanaowadanga wagonjwa kwamba kuna nguvu za kishirikina nyuma ya matatizo yao, lakini hiyo haiondoi ukweli huu tunaojaribu kuuzingumzia, ya uwepo wa uchawi.
 
Niroge au tafuta mchawi aniroge acha ngonjera.
Mimi sikuombei urogwe wala siwezi kukufanyia majaribio. Inaonekana wazi kuwa hujui maana ya uchawi ama umejitoa ufahamu makusudi. Kwa sababu hata ungerogwa, huwezi hatimaye kuappriciate (kutambua) kwamba umerogwa. You are playing on fruitless logic ambayo kimsingi haina msaada wowote. But, luckily, kuna countless, real stories juu ya uchawi ambazo almost kila mtu ameshuhudia. So, siyo kitu kigumu kiasi hicho kuthibitisha. Tatizo tu labda liwe binafsi kukiri uhalisia wake. But kitu kama uchawi wala haihitaji kumlazimisha mtu aamini uwepo wake kwa sababu ni dhahiri shayiri.
 
Mungu alietumba sisi binadamu naamin yupo,,ila izi mambo za uchawi mashetan majini malaika siamin kama vipo
Mungu aliyewaumba nyie "binadamu" vitabu vilivyomuelezea vinakubali uchawi upo.

Sasa unamkubali huyo Mungu halafu unavikataa vitabu vinavyomuelezea uwepo wake?
 
Unajuaje huu ni uchawi na hiki ni kitu ambacho sijakijua tu?

Mababu zetu walioishi miaka 140 iliyopita wangeoneshwa TV na internet leo, wangesema uchawi.

Lakini si uchawi, ni sayansi tu ambayo hawakupata kuijua.

Unahakikishaje hicho unachosema ni uchawi si kitu tofauti tu ambacho hukijui?
Kwanza kabisa hujui uchawi mkuu hata maana yake, hujui hata kitu unachotaka kukibisha, uchawi una lengo la kumweka mtu matatizoni ama kuweweseka,

Hio TV mtu unacheki mechi ya mpira unaoata burudani inakuaje uchawi sasa??

Muwage mnafanya hata karusechi ka maana ya neno,
 
Hapa jamii forums watu wakiwa nyuma ya keyboard wanakua na misimamo ya kushangaza sana,unaweza hisii wote wako ulaya huko kwa jinsi wanavyo dharau na kubisha kwamba uchawi hakuna. Uchawi upo sana hapa Africa na majority ya watu wana practice kwa mdgumuni mbali Mbali.

Wengine wanaenda kwa wataalam wa asili kupata kinga za biashara zao ,afya na familia,wengine wanaenda kuroga kwa sababu ya mapenzi aidha wake au kuolewa,kulipiza kisasa nk. Haya mambo yamenikuta kama mhanga wa hii kitu usiombe,sikia tu kwa mwingine.
 
Kwanza kabisa hujui uchawi mkuu hata maana yake, hujui hata kitu unachotaka kukibisha, uchawi una lengo la kumweka mtu matatizoni ama kuweweseka,

Hio TV mtu unacheki mechi ya mpira unaoata burudani inakuaje uchawi sasa??

Muwage mnafanya hata karusechi ka maana ya neno,
Uchawi ni nini? Unaweza kuu define uchawi ni nini?

Ukisema "uchawi una lengo la kumuweka mtu matatizoni" bado huja define uchawi, kwa sababu hata uongo unaweza kuwa na lengo la kumuweka mtu matatizoni, hata kumpiga mtu risasi kunaweza kuwa na lengo la kumuweka mtu matatizoni.

Unaweza kuthibitisha hicho unachofikiri ni uchawi ni uchawi kweli na si kitu kingine ambacho hukijui tu?
 
Kwanza kabisa hujui uchawi mkuu hata maana yake, hujui hata kitu unachotaka kukibisha, uchawi una lengo la kumweka mtu matatizoni ama kuweweseka,

Hio TV mtu unacheki mechi ya mpira unaoata burudani inakuaje uchawi sasa??

Muwage mnafanya hata karusechi ka maana ya neno,
Good point. Watu wanadhani uchawi ni kaujuzi tu ka namna yake ambako mtu anaweza kujifunza kama anavyofanya mcheza-mpira. Wanasahau kwamba uchawi ni ibada ya mashetani. Nguvu za giza giza zinatoka kwa Iblisi baada ya mtu kumwamini na kumpatia utashi wake.
 
Uchawi ungekuwepo:-

Wakoloni wasingewanyanyasa Babu zetu kiasi kile mpaka wanaume wanne wakiwa nusu uchi wanambeba mwanaume mmoja wa kizungu juu kuanzia Kigoma mpaka Kilimanjaro

Wasingechapwa mijeledi kiasi kile na waarabu

Wanaume wa kinijeria wasingechukuliwa watumwa na kupelekwa America kutumikishwa wazee wao waangalie tu

Timu za Simba na Yanga zingekuwa club bingwa za dunia

Wachezaji wa kibongo wangechezea Barca, Real Madrid, Liverpool etc

Mwisho kabisa hao wachawi wenyewe wangekuwa ni matajiri wakubwa mno sio wa kuomba kuletewa Kuku mweusi
Kama huamini nenda youtube kasachi matukio ya kichawi kwenye michezo hasa mpira wa miguu.
 
Mimi nimeshaomba sana wachawi waniroge ila wanaishia kubwabwaja tu.

Hata hapa nimeshawaambia wachawi waniroge. Kama wanataka kucha au sehemu ya nywele zangu au kipande cha nguo waje kuchukua

Huwa wanaishia kutishia tu.
Hawapo huku mkuu, nenda vilingeni kwao uje tuletee ushuhuda
 
Hapa jamii forums watu wakiwa nyuma ya keyboard wanakua na misimamo ya kushangaza sana,unaweza hisii wote wako ulaya huko kwa jinsi wanavyo dharau na kubisha kwamba uchawi hakuna. Uchawi upo sana hapa Africa na majority ya watu wana practice kwa mdgumuni mbali Mbali.

Wengine wanaenda kwa wataalam wa asili kupata kinga za biashara zao ,afya na familia,wengine wanaenda kuroga kwa sababu ya mapenzi aidha wake au kuolewa,kulipiza kisasa nk. Haya mambo yamenikuta kama mhanga wa hii kitu usiombe,sikia tu kwa mwingine.
Absolutely. Watu wamejizoeza kwenye uganga, uchawi na ushirikina kiasi kwamba imekuwa sehemu ya maisha; watu hawawezi kutambua tena kama ndio uchawi wenyewe. Halafu uchawi uko kila mahali, siyo kwa Waafrika peke yao. Kila jamii ya watu wanapojitenga na Mungu, by default, wanakuwa wamejiweka chini ya utawala wa giza wa mashetani.
 
Uchawi ni nini? Unaweza kuu define uchawi ni nini?

Ukisema "uchawi una lengo la kumuweka mtu matatizoni" bado huja define uchawi, kwa sababu hata uongo unaweza kuwa na lengo la kumuweka mtu matatizoni, hata kumpiga mtu risasi kunaweza kuwa na lengo la kumuweka mtu matatizoni.

Unaweza kuthibitisha hicho unachofikiri ni uchawi ni uchawi kweli na si kitu kingine ambacho hukijui tu?
Keyword katika kudifaini uchawi ni "supernatural influence." Hii ni nguvu ambayo kimsingi haiwezekaniki na wala haielezeki kwa namna yoyote ya fikra za kawaida kibinadamu. It is simply beyond reason.
 
Absolutely. Watu wamejizoeza kwenye uganga, uchawi na ushirikina kiasi kwamba imekuwa sehemu ya maisha; watu hawawezi kutambua tena kama ndio uchawi wenyewe. Halafu uchawi uko kila mahali, siyo kwa Waafrika peke yao. Kila jamii ya watu wanapojitenga na Mungu, by default, wanakuwa wamejiweka chini ya utawala wa giza wa mashetani.
Kuna sister alienda chimbo anataka kuolewa na yule Mzee akamfanyia kazi Kisha akamwambia mwanaume wa 3 kukutongoza ukirudi town lazima akuoe kwa harusi ndani ya siku 90 zijazo. Wiki mbili zilizopita tumekula wali ndani ya time frame ile ile ya mtaalam.
 
Kuna mtu keshawai nisingizia Uchawi... Wewe Dada Rachel ..Mimi hayo mambo Wala siyajui maskini... Sijui nilikufanyaje Hadi ukaniita Mchawi... Nimemuachia Muumba wa mbingu na ardhi... Anitetee
 
Back
Top Bottom