Mphamvu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 10,702
- 3,285
za jioni bhandugu? ni muda mrefu nimekuwa mteja wa huu mtandao wa tiGO, tangu enzi zile ukiwa unaitwa Mobitel na namba zao za 0811****** na tukijaza vocha kwa kutumia kadi poa zenye rangi ya njano tena kwa dola, ambayo ilikuja kubadilishwa na kuwa Buzz na kufuatiwa na namba yenye mwanzo 0741****** hata majuzi, 2005 nadhani ilipokuwa hili jina ambalo limepewa maana mpya ya tundu la kinyesi na namba zetu kubadilika na kuwa 0713******. sasa kwa vile mtandao si kabila hata lisibadilishike, mwenzenu nimechoka na maudhi, uongo na wizi wa hili kampuni, nimehama, nimehamia Airtel. wote mnaonitafuta nimewatumia namba zangu mpya kwenye simu zenu za rununu. ahsanteni.