Nimeguswa na ubunifu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), nawapongeza na kuwataka waongeze ubunifu

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,196
25,515
Jumapili ijayo, klabu za Simba na Yanga zinapambana kwenye mchezo wa fainali wa Kombe la Shirikisho almaarufu kama Azam Conf. Cup. Mchezo huo kabambe ambao unabeba tukio kubwa la kisoka nchini utapigwa kwenye uwanja wa Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma.

Katika kuchagiza na kusherehesha mechi hiyo ya watani wa jadi, Shirika la Reli nchini (TRC) imeandaa safari ya treni kwa ajili ya mashabiki wa Simba na Yanga kuanzia Dar es Salaam hadi Kigoma na kurudi katika hali ya ubunifu. Safari husika itafanyika leo (?) na kurudi ni Jumapili baada ya mechi.

Ndani ya treni husika kutakuwa na michezo ya aina mbalimbali kama drafti huku watanzania wapenda furaha wakijumuika kubadilishana mawazo na 'kusahau' shida zao wakati wa kwenda na kurudi. Kitu pekee kinachppaswa kuzingatiwa safarini ni hatua za tahadhari dhidi ya maambukizi ya UVIKO.

Kwa moyo wangu wa dhati, nawapongeza TRC. Nawaomba na kuwahamasisha kubuni mambo mengine mazuri kwa ajili ya watanzania na maendeleo ya Shirika la Reli kwa ujumla.
 
Jumapili ijayo, klabu za Simba na Yanga zinapambana kwenye mchezo wa fainali wa Kombe la Shirikisho almaarufu kama Azam Conf. Cup. Mchezo huo kabambe ambao unabeba tukio kubwa la kisoka nchini utapigwa kwenye uwanja wa Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma.

Katika kuchagiza na kusherehesha mechi hiyo ya watani wa jadi, Shirika la Reli nchini (TRC) imeandaa safari ya treni kwa ajili ya mashabiki wa Simba na Yanga kuanzia Dar es Salaam hadi Kigoma na kurudi katika hali ya ubunifu. Safari husika itafanyika leo (?) na kurudi ni Jumapili baada ya mechi.

Ndani ya treni husika kutakuwa na michezo ya aina mbalimbali kama drafti huku watanzania wapenda furaha wakijumuika kubadilishana mawazo na 'kusahau' shida zao wakati wa kwenda na kurudi. Kitu pekee kinachppaswa kuzingatiwa safarini ni hatua za tahadhari dhidi ya maambukizi ya UVIKO.

Kwa moyo wangu wa dhati, nawapongeza TRC. Nawaomba na kuwahamasisha kubuni mambo mengine mazuri kwa ajili ya watanzania na maendeleo ya Shirika la Reli kwa ujumla.
Hivi huo si mkusanyiko..!?
 
Huo ubunifu umetoka kwa Joseph Kusaga wa Clouds media
TRC miaka yote hawajui usafi wala fummigation ya mabehewa ila Kusaga anajua kutumia fursa na kampuni yake kuwa sehemu ya mradi huu
 
Huo ubunifu umetoka kwa Joseph Kusaga wa Clouds media
TRC miaka yote hawajui usafi wala fummigation ya mabehewa ila Kusaga anajua kutumia fursa na kampuni yake kuwa sehemu ya mradi huu
Watanzania ni nai alituloga? Hili nalo ndilo linaitwa ubunifu? Kusafirisha washabiki wa mpira kwenda kwenye mechi ndiyo ubunifu? Hakika nchi yangu inaangamia kwa kukosa watu weledi
 
Tatizo Taasisi za Serikali wengi wenye Mitazamo ya Kisasa hawana nafasi za Maamuzi. TTCL kuna vijana wemgi sana wa kisasa lkn hawana nafasinza kufanya maamuzi.
Wanawaona ni threat kwao, badala ya kuwatumia productively wao wana wasuppress
 
Wanashangaza sana hawa watu. Wanapiga marufuku mikusanyiko ya watu ili kupambana na COVID-19 lakini mikusanyiko wanayoitaka wao RUKHSA!!!! Acha COVID-19 iendelee kutambaa nchini kwa uzembe wa Serikali.
Hivi huo si mkusanyiko..!?
 
Back
Top Bottom