Kesi ya Sabaya Inakosekanaje mashahidi? Hapa kichwa kinaniuma kwa kujiuliza. Jinsi huyu dogo alivyokuwa anafanya "unyama" (kwa mujibu wa maelezo ya watu.
Nlitegemea mahakamani pangekuwa panajaa mashahidi wengi mpaka wanarudishwa makwao au kesi ingefanyiwa kwenye uwanja wa mpira. "Huyu dogo kaumiza wengi sana, kawatesa na kuwaua"
Hawa watu hawajitokezi kwenda mahakamani kwa nini? Mbowe naye alitendewa unyama na huyu dogo. Je amesamehe? Aende akafungue kesi asiache tu watu watende makosa akasamehe.
Nikakumbuka MAKONDA NAYE ALISINGIZIWA MENGI SANA. Mbona hakuna aliyeenda mfungulia kesi?alihusishwa na shambulizi la Lissu mbona hajashtakiwa? Aliyoyafanya pale clouds je walikubaliana naye?
Wale waliosingiziwa na kuchafuliwa suala la madawa Wakamshtaki aliyewafanyia hivyo. Kwa nini hawaendi mahakamani ili kukomesha tabia hiyo?
Tunataka Haki itendeke. Wote waliokosea wananchi waadhibiwe. Je yaliyosemwa yalikuwa ni fitna za watu? Why mashahidi wakosekane? Angekosekana mmoja leo wale wengine kadhaa si wangetoa ushahidi?
Topic za kijinga tuna mambo muhimu badala ya kuongelea vijana wajinga jinga