Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Tulianza awamu ya tano tukapiga makofi wapinzani walipofilisiwa na kufunguliwa kesi tukiamini tunakijenga chama. Tulipomalizana nao tuliamia kwa wana CCM nakuwachapa kuanzia kwenye fikra Hadi kwenye akaunti zao. Leo Wana CCM wote waliokuwa na nguvu ya kiuchumi wamefilisika, au wamekufa kwa presha na baadhi wamepoteza madaraka.
Kwanini yamewapata hayo? Ni kwa sababu waliamua kuishi maisha ya Mwenye nchi badala ya kuishi maisha yao. Wapo watu kwa uzembe kabisa bila kujali elimu zao waliumizwa kisa tu wanamwelekeo na mawazo tofauti. Lakini pia wapo watu walitumia nguvu za kibinadamu na dola kutesa wengine wakiamini zamu yao itadumu Sana. Pole kwao maana Mungu alipangalo si la wanadamu.
Tukamaliza harakati za awamu ya tano, walioamini wapo salama wakageuziwa kibao nakuondolewa kwenye nafasi zao Kisha kukalishwa kimya. Kwa frastration wakanzisha Hadi madarasa ya uongozi na wengine kujifanya wataalamu wa afya kupinga chanjo ya COvID19 lakini leo wote wamenyamazishwa na wanatakiw kuongea lugha moja na waliyedhani Hana nguvu.
Lakini ni Jambo kubwa kwamba unapopanga kuwanyoosha na Mungu naye anapanga ratiba yake, unapotumika kuwanyoosha na Mungu naye anapanga ratiba yake. Akina Rwegamalila waliishi utumwani kwa uvumilivu wakiaminishwa kwamba hakuna namna wanaweza kurudi uraiani lakini Leo wale wote waliokuwa wanawakandamiza awapo kwenye nafasi zao na wengine hata Duniani awapo.
Wapo watu wachache Sana nimeona wanashangilia maamuzi ya kesi ya Mbowe, lakini madhara ya maamuzi haya Ni makubwa Sana kwa wanyonge wa nchi hii. Ninaposema wanyonge simaanishi kwamba watu wasio na fedha Bali namaanisha wale wote ambao maamuzi haya yanawaruhusu kuteswa na dola na bila kuhojiwa. Mfano mkubwa ni utata wa kifo Cha dreva wa kampuni ya Dangote ambapo maelezo ya Polisi yaliyotolewa kila mtu ameyatilia mashaka lakini kile walichotamka Polisi ndicho kinachoishi.
Siyo hayo, tumeshuhudia machinga wakijaribu kufanya fujo karikoo lakini uongozi wao leo wamejitokeza na kusema wale siyo machinga bali Ni wahuni na imepita hivyo. Usidhani Kiongozi wa machinga anappsema Yale aliyoyasema hajui ukweli wake Bali ndivyo amabvyo tunaishi. Kwamba Mwenye kusema hiki ni sawa na si sawa ni serikali.
Niseme wazi kwamba tunaposhangilia maamuzi ya Jaji ambayo hayana hata kifungu Cha sheria kinachoonyesha msingi wa maamuzi yake Basi tutambue kwamba hii siyo huku ya Mbowe. Ni hukumu yakuigwa na mahakama zetu nyingi nchini. Tukumbuke ipo siku Kama ilivyozoeleka kwa miaka mitano viongozi na watu wenye ushawishi ndani ya CCM ambao Sasa hivi wanaona dola na mahakama Wana ndoa nzuri ndoa hiyo itawaathiri wao na famililia zao.
Nimalizie, Makonda aliteuliwa na JK kabla yakuteuliwa kuwa RC na JPM. Lakini ni Makonda huyo huyo wakati anataka kuonyesha ana nguvu alisau mambo yote Jk na familia yake waliyomfanyia na kumtangaza Riz one kwenye skendo za madawa ya kulevya bila hata kutoa ushahidi wowote. Lakini pia wazee wa CCM wasiwe wepesi wa kusahau namna ambavyo wao na familia zao walinyanyasika, mateso waliyopata hayakuzongatia tuhuma zilizothibitika Bali yalijikita kukomoa.
Maamuzi ya Jaji Siyani ambayo yanafuatia uendeshaji wa kesi huku muda wa Azana kesi ikiwa inasimamishwa kumheshimu Mungu itufumbue macho kwamba hawa watu tunaowashangilia ndio hao hao wanaotafuta kututawala wanapokuwa mafichoni au sirini. Tufurahie maana tunamwona Mbowe akiwa anapita mateso lakini naamini vijana waliopo naye kwenye kesi wana wazazi kama ambavyo qatoa maamuzi Wana wazazi.
Tukumbuke Kama baba Riz alivyoumia mwanaye kutajwa kwenye madawa ndivyo wazazi, mke na watoto wa watuhumiwa wanavyoumia wanapogundua muda wakusubiri vijana wao wawahudumie watu wachache ambao Sasa hivi usiku huu wapo wanastarehe na familia zao, wanaitwa Dad na Mom, wanaulizia mshahara utatoka lini wameamua bila sababu yoyote kuakikisha kwamba vijana wale wanateseka na may be wanakufa ili wao malengo yao yatimie.
Mungu aishiye anaweza akanyamaza kwa machozi ya familia hizi kwa muda ila atonyamaza milele. Tunaposherekea ushindi uluotolewa na Jaji leo Ni vyema pia tukaandaa nafsi zetu kupokea maamuzi ya mwenyenzi Mungu dhidi ya watuhumiwa na waliosababisha wapate mateso wanayopitia Sasa.
Niwatakie sherehe njea, bia ziendelee kuwa tamu kwenu lakini pia muda wa majonzi utakapowadia tuwe tayari kuupokea. Hongera wote tunaofurahia ushindi mkuu.
Kwanini yamewapata hayo? Ni kwa sababu waliamua kuishi maisha ya Mwenye nchi badala ya kuishi maisha yao. Wapo watu kwa uzembe kabisa bila kujali elimu zao waliumizwa kisa tu wanamwelekeo na mawazo tofauti. Lakini pia wapo watu walitumia nguvu za kibinadamu na dola kutesa wengine wakiamini zamu yao itadumu Sana. Pole kwao maana Mungu alipangalo si la wanadamu.
Tukamaliza harakati za awamu ya tano, walioamini wapo salama wakageuziwa kibao nakuondolewa kwenye nafasi zao Kisha kukalishwa kimya. Kwa frastration wakanzisha Hadi madarasa ya uongozi na wengine kujifanya wataalamu wa afya kupinga chanjo ya COvID19 lakini leo wote wamenyamazishwa na wanatakiw kuongea lugha moja na waliyedhani Hana nguvu.
Lakini ni Jambo kubwa kwamba unapopanga kuwanyoosha na Mungu naye anapanga ratiba yake, unapotumika kuwanyoosha na Mungu naye anapanga ratiba yake. Akina Rwegamalila waliishi utumwani kwa uvumilivu wakiaminishwa kwamba hakuna namna wanaweza kurudi uraiani lakini Leo wale wote waliokuwa wanawakandamiza awapo kwenye nafasi zao na wengine hata Duniani awapo.
Wapo watu wachache Sana nimeona wanashangilia maamuzi ya kesi ya Mbowe, lakini madhara ya maamuzi haya Ni makubwa Sana kwa wanyonge wa nchi hii. Ninaposema wanyonge simaanishi kwamba watu wasio na fedha Bali namaanisha wale wote ambao maamuzi haya yanawaruhusu kuteswa na dola na bila kuhojiwa. Mfano mkubwa ni utata wa kifo Cha dreva wa kampuni ya Dangote ambapo maelezo ya Polisi yaliyotolewa kila mtu ameyatilia mashaka lakini kile walichotamka Polisi ndicho kinachoishi.
Siyo hayo, tumeshuhudia machinga wakijaribu kufanya fujo karikoo lakini uongozi wao leo wamejitokeza na kusema wale siyo machinga bali Ni wahuni na imepita hivyo. Usidhani Kiongozi wa machinga anappsema Yale aliyoyasema hajui ukweli wake Bali ndivyo amabvyo tunaishi. Kwamba Mwenye kusema hiki ni sawa na si sawa ni serikali.
Niseme wazi kwamba tunaposhangilia maamuzi ya Jaji ambayo hayana hata kifungu Cha sheria kinachoonyesha msingi wa maamuzi yake Basi tutambue kwamba hii siyo huku ya Mbowe. Ni hukumu yakuigwa na mahakama zetu nyingi nchini. Tukumbuke ipo siku Kama ilivyozoeleka kwa miaka mitano viongozi na watu wenye ushawishi ndani ya CCM ambao Sasa hivi wanaona dola na mahakama Wana ndoa nzuri ndoa hiyo itawaathiri wao na famililia zao.
Nimalizie, Makonda aliteuliwa na JK kabla yakuteuliwa kuwa RC na JPM. Lakini ni Makonda huyo huyo wakati anataka kuonyesha ana nguvu alisau mambo yote Jk na familia yake waliyomfanyia na kumtangaza Riz one kwenye skendo za madawa ya kulevya bila hata kutoa ushahidi wowote. Lakini pia wazee wa CCM wasiwe wepesi wa kusahau namna ambavyo wao na familia zao walinyanyasika, mateso waliyopata hayakuzongatia tuhuma zilizothibitika Bali yalijikita kukomoa.
Maamuzi ya Jaji Siyani ambayo yanafuatia uendeshaji wa kesi huku muda wa Azana kesi ikiwa inasimamishwa kumheshimu Mungu itufumbue macho kwamba hawa watu tunaowashangilia ndio hao hao wanaotafuta kututawala wanapokuwa mafichoni au sirini. Tufurahie maana tunamwona Mbowe akiwa anapita mateso lakini naamini vijana waliopo naye kwenye kesi wana wazazi kama ambavyo qatoa maamuzi Wana wazazi.
Tukumbuke Kama baba Riz alivyoumia mwanaye kutajwa kwenye madawa ndivyo wazazi, mke na watoto wa watuhumiwa wanavyoumia wanapogundua muda wakusubiri vijana wao wawahudumie watu wachache ambao Sasa hivi usiku huu wapo wanastarehe na familia zao, wanaitwa Dad na Mom, wanaulizia mshahara utatoka lini wameamua bila sababu yoyote kuakikisha kwamba vijana wale wanateseka na may be wanakufa ili wao malengo yao yatimie.
Mungu aishiye anaweza akanyamaza kwa machozi ya familia hizi kwa muda ila atonyamaza milele. Tunaposherekea ushindi uluotolewa na Jaji leo Ni vyema pia tukaandaa nafsi zetu kupokea maamuzi ya mwenyenzi Mungu dhidi ya watuhumiwa na waliosababisha wapate mateso wanayopitia Sasa.
Niwatakie sherehe njea, bia ziendelee kuwa tamu kwenu lakini pia muda wa majonzi utakapowadia tuwe tayari kuupokea. Hongera wote tunaofurahia ushindi mkuu.