Nimefukuzwa kazi kisa nimekula chakula cha boss, inauma sana

TheDreamer Thebeliever

JF-Expert Member
Feb 26, 2018
2,490
3,534
Habari wadau.

Miezi kadhaa iliyopita nilibahatika nilipata kazi katika kampuni moja kubwa ya uzalishaji .

Nilianza kazi vizuri tu, ila siku ya kwanza tu naingia ofisini sekretari wa boss akaonyesha kunichangamkia kama tulishawai kuonana before mpaka nikaogopa, nikajitahidi kumkwepa sana lakini hakuwezekana.

Weekend moja akanipigia simu anakuja ghetto maana hata namba aliniomba nikampa, nikamwambia sipo nyumbani nimetoka kidogo lakini ghafla nikashangaa mlango unagongwa kumbe wakati anapiga simu teyari alishakuwa amefika na sikuwahi kumuelekeza ninapoishi. Kumbe wakati anapiga simu alikuwa anasikilizia nitamjibu vipi iwapo atataka kuja kwangu.

Mungu anisamehe kwa kweli, kama kawaida alipoingia tunduni tu sekretari wa boss na mimi nikaweka nyavuni pasipo kujua kwamba ni chakula ya boss wangu.

Siku moja tu kwa kweli imeharibu ajira yangu yote, kumbe kuna watu walimuona wakati anatoka ghetto wakaenda kumwambia Mr.Boss man kwamba nimekula tunda yake.

Kibaya zaidi boss ana undugu na mwenye kampuni kwa hiyo boss akaongea na Hr mshahara wangu nisiingiziwe, na nifanyiwe figisu mpaka kazi niione chungu.

Huwezi amini miezi yote miwili sikupata mshahara, kila siku mm nina kesi ofisini kwa Hr.

Naombeni ushauri bandugu hii job niipige chini au nifanyeje? Maana wajuba wamenambia yote unayopitia ni sababu umekula chakula ya boss ila mm kiukweli sikujua kama ile manzi sekretari ni kipoozeo ya boss.
 
Habari wadau..!
Miezi kadhaa iliyopita nilibahatika nilipata kazi katika kampuni moja kubwa ya uzalishaji .

Nilianza kazi vizuri tu ,ila siku ya kwanza tu naingia ofisini sekretari wa boss akaonyesha kunichangamkia kama tulishawai kuonana before mpaka nikaogopa ,nikajitahidi kumkwepa sana lakini hakuwezekana.
Kwa kifupi umepoteza ada za wazazi wako na juhudi zako sababu ya njaa na ulafi ni jambo la kusikitisha sana.
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom