mapipando
JF-Expert Member
- Jun 8, 2015
- 2,921
- 3,549
Heshima kwenu wakuu.
Nilianzisha uzi hapa "huu ni mwaka wangu wa mwisho kuajiriwa" na kweli nilipanga kuacha kazi baada ya kuona mshahara hautoshelezi mahitaji yangu na familia kwa ujumla.
Lakini kutokana na baadhi ya michango yenu hasa mlioniambia nisiache kazi bali nitafute namna yeyote niweze kuongeza kipato nimeheshimu ushauri wenu na ninawashukuru sana sana.
Nimegundua kuna biashara nyingi ambazo ukiziangalia kwa kawaida unazidharau lakini ni biashara ambazo sio pasua kichwa na zina faida sana ila sisi tunazichukulia poa ama kama uchafu flani na kujirundika kwenye aina moja za biashara ambazo ziko na ushindani mkubwa sokoni mfano ufugaji na kilimo.
Mfano biashara ya chuma chakavu, hii inalipa sana kwani kilo moja inanunuliwa kwa 500 na kuuzwa 800, na wewe unauza kuanzia tani moja na kuendelea. Ikitokea kwa mwezi umekusanya tani 3 na kuziuza zote maana yake uko na faida ya 900k
Pia biashara ya makopo ya plastiki pia ni nzuri maana nayo haina stress nyingi lakini inalipa. Kilo moja inanunuliwa 150-200 na kuuzwa kwa 500. Kwa maana hiyo hapo kuna faida sawa na mtaji...ukiwa na mzigo laki tano faida laki tano pia.
Nimeulizia mzani wa kupimia chuma nimeambiwa unanzia laki 7 na mzani wa chupa (ile ya kuning'iniza) inaanzia elfu 25.
Wakati huu ambao siwezi kuanzisha biashara ya chuma, nimeona nianze na hii ya chupa. Nitatengeneza mazingira rafiki hapa home kwangu ili niweze kuiendesha hii biashara na hapo baadae nitafute mashine ya kukatakata ili niwe nahifadhi kwenye mifuko.
Kama kuna mwenye uzoefu na hizi biashara karibu kwa mawazo.
Shukrani.
Nilianzisha uzi hapa "huu ni mwaka wangu wa mwisho kuajiriwa" na kweli nilipanga kuacha kazi baada ya kuona mshahara hautoshelezi mahitaji yangu na familia kwa ujumla.
Lakini kutokana na baadhi ya michango yenu hasa mlioniambia nisiache kazi bali nitafute namna yeyote niweze kuongeza kipato nimeheshimu ushauri wenu na ninawashukuru sana sana.
Nimegundua kuna biashara nyingi ambazo ukiziangalia kwa kawaida unazidharau lakini ni biashara ambazo sio pasua kichwa na zina faida sana ila sisi tunazichukulia poa ama kama uchafu flani na kujirundika kwenye aina moja za biashara ambazo ziko na ushindani mkubwa sokoni mfano ufugaji na kilimo.
Mfano biashara ya chuma chakavu, hii inalipa sana kwani kilo moja inanunuliwa kwa 500 na kuuzwa 800, na wewe unauza kuanzia tani moja na kuendelea. Ikitokea kwa mwezi umekusanya tani 3 na kuziuza zote maana yake uko na faida ya 900k
Pia biashara ya makopo ya plastiki pia ni nzuri maana nayo haina stress nyingi lakini inalipa. Kilo moja inanunuliwa 150-200 na kuuzwa kwa 500. Kwa maana hiyo hapo kuna faida sawa na mtaji...ukiwa na mzigo laki tano faida laki tano pia.
Nimeulizia mzani wa kupimia chuma nimeambiwa unanzia laki 7 na mzani wa chupa (ile ya kuning'iniza) inaanzia elfu 25.
Wakati huu ambao siwezi kuanzisha biashara ya chuma, nimeona nianze na hii ya chupa. Nitatengeneza mazingira rafiki hapa home kwangu ili niweze kuiendesha hii biashara na hapo baadae nitafute mashine ya kukatakata ili niwe nahifadhi kwenye mifuko.
Kama kuna mwenye uzoefu na hizi biashara karibu kwa mawazo.
Shukrani.