Nimefanyiwa vitendo vya uonevu na askari wa osterbay,naomba msaada

Mopalmo

JF-Expert Member
Nov 11, 2010
533
138
Wadau wa jf,nilikamatwa na askari wa kituo cha osterbay nikiwa coco beach jumatatu ya tar 23 nikiwa na mpenzi wangu,wakatupeleka kituo cha oysterbay nakatubambika kesi ya kufanya mapenz ufukweni,kitu ambacho si cha kweli na kutulazimisha tutoe elfu 50,mpenz wangu kwa kuogopa alitoa kiasi hicho ambacho hakikua chake na tukaachiwa,nilifanikiwa kuchukua namba zao na ninataka niwaanike hadharani nitatumia njia gani angalau niweke hadharani ili askari wengine wenye tabia kama hiyo waache na mimi niridhike
 
Ulitakiwa kuwasiliana na mtu wapige picha wakati wanapokea hiyo pesa. Ulichukua namba zipi ? Za kwenye sare au silaha. Hata hivyo, kuchukua namba tu haina maana hao jamaa wanaweza kukana kuwa hawakuchukua huo mlungula. Lakini kama una uhakika kuwa hukuwa na kosa kwa nini ukakubali wapewe hiyo 50,0000/= ?
 
Ulitakiwa kuwasiliana na mtu wapige picha wakati wanapokea hiyo pesa. Ulichukua namba zipi ? Za kwenye sare au silaha. Hata hivyo, kuchukua namba tu haina maana hao jamaa wanaweza kukana kuwa hawakuchukua huo mlungula. Lakini kama una uhakika kuwa hukuwa na kosa kwa nini ukakubali wapewe hiyo 50,0000/= ?

Mpenz wangu alizitoa kwa uoga,si unajua tungewekwa ndani ingekuaje nyumbani kwao kama asingetoa
 
Mkuu, jeshi la plisi ni kijiwe siku hizi.
That is what they do.

pole sana bana, next time hakikisha una-record mazungumzo yenu........hizi simu tunazitumia za nini kama haziwezi kutusaidia??
ukipata hata audio tu inayothibitisha sauti ikidai buku fifty, hiyo ni bingo.
 
elfu hamsini ndogo sana..jamaangu walimtoa 300,000 alikuwa ana**mbania kwenye gari!
NB:hapo kwenye star weka "to"
 
Nyie ni uoga wenu tuu..ungekomaa wawapeleke ndani kisha wangeandika maelezo ya kosa lenu na nyie mgetoa statement yenu ..ijue sheria na haki yako pia....hapo sahivi unakosa la kutoa rushwa na askari ulemnakili namba anakosa la kupokea rushwa..nyote mnatakiwa kufungwa kwa mujibu wa sheria za takukuru
 
Man hukugangamala aisee mie nilikuwa nimepakai gari yangu nakula mihogo niko mie na mpenzi wangu na mshikaji wangu sasa tukawa tumekaa tunapiga story....mara mshikaji akatoka akaenda kuchukua mihogo mingine mie nimebaki front seat na wangu yuko back seat...tumekaa tunakula story gari zilizokuwa pembeni zilikuwa zimeondoka tumebaki sie tuu sasa wakati tunaongea nikashangaa tochi kwenye kioo cha mbele nikamind nikafungua mlango askari akaninyooshea mtutu nikamwambia unataka kuniua au...akamind eti mnafanya nini hapa peke yenu nyie ndio wahalifu, akaniomba kitambulisho nikamwambia na yeye anipe...akawa mkali nikasimama kidete kuwa asinifanye mie mwendawazimu sheria ipi niliyovunja anipe kifungu basi akawa anajifanya subiri subiri...likaja lile cruiser lao na kwa bahati mbaya na mshikaji kafika basi wakawa wanasema wanataka kusachi nikawaambia on their face ili mnibambikee sifungui milango mpaka wanipe kidhibiti cha kunisachi basi wangu akawa anasema niachane nao niwape wanachokitaka nikampotezea huku nikiwa mkalii kwa maafande huwezi amini afande mmoja nikamsikia akisema huyo sio mwaacheni twendeni mbeleeee nikawa nawaangalia wanatakaje mmoja akanifuata akiniambia tusikukute maeneo haya nikamwambia mie Mtanzania kama hapa nilipopaki ni kenya hutanikuta lakini kama ni Tanzania napaki wakaondoka nikapaki nikala nikaridhika ndio nikaondoka....Lingine la muhimu huo mchezo wa askari kuja kwenye baadhi ya magari unafanywa na baadhi ya wale vijana wa pale ukiona kuna kijana anakuwa hana shughuli maalum jua kuwa anacheki kama mmekaa kimtindo halafu anawapigia majamaa,ili waje kuweni makini ila jamani msikubali kunyanyaswa na hawa wapuuuziii hii ni nchi yetuuu komaaa huvunji sheria kukaa na mpenzi wako kwenye gari sehemu ya public....
 
elfu hamsini ndogo sana..jamaangu walimtoa 300,000 alikuwa ana**mbania kwenye gari!
NB:hapo kwenye star weka "to"

Sisi hatukua tunafanya hivyo,ndio maana najiskia vibaya sana kwa uonevu ule,ni kama uporaji wala si rushwa natamani nipate njia ya kuwatangaza kwa wanajamii,namba za kwenye jezi zao ninazo ila picha sina na walikua watatu na sura zao nazikumbuka na kituo ni oysterbay,kama kuna mwandishi aliye tayari kuwaripoti ani pm
 
Nyie ni uoga wenu tuu..ungekomaa wawapeleke ndani kisha wangeandika maelezo ya kosa lenu na nyie mgetoa statement yenu ..ijue sheria na haki yako pia....hapo sahivi unakosa la kutoa rushwa na askari ulemnakili namba anakosa la kupokea rushwa..nyote mnatakiwa kufungwa kwa mujibu wa sheria za takukuru

Mi nimekuomba ushauri ndugu,hayo uliyoongea hayasaidii zaidi zaidi unanilaumu tu,kitu ambacho hakinisaidii
 
Wadau wa jf,nilikamatwa na askari wa kituo cha osterbay nikiwa coco beach jumatatu ya tar 23 nikiwa na mpenzi wangu,wakatupeleka kituo cha oysterbay nakatubambika kesi ya kufanya mapenz ufukweni,kitu ambacho si cha kweli na kutulazimisha tutoe elfu 50,mpenz wangu kwa kuogopa alitoa kiasi hicho ambacho hakikua chake na tukaachiwa,nilifanikiwa kuchukua namba zao na ninataka niwaanike hadharani nitatumia njia gani angalau niweke hadharani ili askari wengine wenye tabia kama hiyo waache na mimi niridhike

nendeni tena mkafanye mapenzi palepale wakukamateni uwaanike vizuri!
 
Back
Top Bottom