Star Park hiki kiwanja ni noma sanaaaaa... Juzi nilikuwa pale aisee hilo nyomi si la kawaida, kaunta karibia 4 lakini bado zinazidiwa, jamaa ametega vizuri sana...Mtaa unahitaji ubishi sana, kama unayo spirit ya ubishi kukubali kuchekwa na kuanza 1 huku ukitoa mawazo ya uyatima unatusua ....Elimu uliyo nayo tayar ni advantage achana na vyeti kwanza...
Tafuta club/casino au manager sehem yyt ya starehe kubwa omba nafasi pale kaunta kama mhudumu wa pale pale cheza na kuhudumia huku ukiweka uaminifu wako,kuna hela sana na sehem zile watu wa hesabu wanatakiwa sana maana kuna wakati watu wanajaa wanahitaji huduma ya chap chap...
Nenda morogoro ulizia star park ni wapi, ukifika pale mtafute manager mwambie nimeelekezwa na MD Mbabe au Mbishi.,atanipigia simu nitakusaidia....hata sisi tumekuwa kiyatima ila tukaweka mapambano mbele bila kuangalia watu.
Ulipoona elimu Ni ghali ukajaribu ujinga.Habari wanajamvi,
Natanguliza samahani kwa kuwapotezea muda ila nimeandika huu uzi kwa lengo la kuomba ushauri mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu ndio nilikua namaliza ila nimeshindwa baada ya kufukuzwa chuo na sababu ni kumfanyia mwanafunzi mwenzangu mtihani wa sapp huyu rafiki yangu
Nimejuana nae toka mwaka wa kwanza na changamoto yake toka mwaka ule wa kwanza alikamatwa MATHEMATICS sasa yeye katoka HGL na hakua na msingi wa hesabu aliibebea toka mwaka huo sasa mwaka huu akaona lazima agraduate na njia pekee ni kumuomba mtu amfanyie
Tulienda Kariakoo kuchongesha ID ikafika siku ya mtihani akanipa niliingia kufanya nikamuonyesha examination invigirator ID akaingalia akaniruhusu nifanye kibaya baada ya kumaliza msimamizi akapata hofu akasema nimpe ID tena aiangalie ndipo nilipokamatwa na kupelekwa admission nilipigwa na walinzi mpaka nikamtaja mwenzangu
Sasa hukumu leo imetoka nimefutwa chuo na mimi ni yatima sina wazazi yaani nimesomeshwa na serikali nilipata boom %100 na o-level ni taasisi za dini ndio zilinipa msaada wa kunilipia elfu ishirini ya ada na vifaa vya shule hapa
Nimechanganyikiwa sina hata cha kufanya nahisi dunia imenielemea naombeni ushauri wenu tafadhali
Umeamua kugeuka mshumaa ,kumulikia wenzako.Ni kweli kaka ninachoumia sina baba sina mama na nilikua na pass mark nzuri na dunia inaamini katika certificate sina cha kuipa dunia nashindwa nianzie wapi kutoka sasa