Nimechukua mkopo benki, naomba ushauri katika namna niliyopanga kuutumia

Tumia yote 30mil kununua gari SUV mambo ya wese usiwaze gari sasa zinatumua umeme zaidi, isitoshe jioni utakula vichwa za changia mafuta buku 2 kwa kichwa.
Mjengo achana nao, utajiseti huo baadae usiuache ushauri huu wala usiskilize ushauri mwingine, sasa ziba masikio
Ushauri kama huu unapotosha
 
Bwana mdogo,..mil30 ni hela ndoogo sana ukiishika amini nakwambia,na sikushaur ufanyie biashara hyo hela sabab kwa ulivyo ulivyo tuu nmeona hutoweza,tuanzie hapo kwanza,so hako ka 30 kama ulivosema unataka gar na kumalizia nyumba na hela ya bata,..naona umejitoa muhanga,first of all ushafel so ngoja nikushaur kutoka kwenye hyo failure,..

Subir had december kuna yard nying tu hua wana ofa,mfano pale namanga ile yard ya wa pakistan,acha mbwebwe za IST ziko juu sana mpya,na usinunue gar mkonon,utakuja juta,..nenda pale yard tafta ractis or fun cargo or gar yoyote utakayokuta ,hua ofa znafika had 7.5m..kwa sis wateja wa kudum hua tunapigiwa sim kabsa,kuna gar hii na hii zna ofa..usinunue zaid gar zaid ya m9..then hela inayobak malizia tuu nyumba hyo,namaanisha hela yoteee,usiweke hela ya bata sabab bata hyo na wenge la hela,utapata majanga,ajali,kuibiwa,etc utarud nyuma utatumia hela zilizobak kujiuguza,so hela yote malizia ujenz,tenga 15mil,tafta fund ,tumia budget ndogo uwezavyo,..vifaa vyote nenda dukan usitume mtu..mil6 iliyobak weka bank ipige fixed,huku ukitafta kamrad kakukuingiza sh mbil tatu


Nmeshaur kutokana na experience

Sent using Jamii Forums mobile app
nice
 
Ni kweli mkuu.
Utakuta hapo mshahara wake laki 6 take home.
Akikatwa mkopo wa benki ibaki laki 3.5.
Halaf hyo hyo alishe familia na nyingine anunue mafuta ya gari.
Wakati huo hapo gari ni mpya then baada ya mwaka gari ikianza kuchoka ataanza kununua spea.
Hivi ndio umaskini hukaribishwa kwenye familia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaweza usikope na ikawa maskini vilevile acheni mawazo ya kimaskini hayo maisha yenyewe ya hapa hapa duniani na mafupi sana

Eti akubali kupanda daladala abebe chawa na kunguni apeleke nyumbani huku anapigwa na mvua wakati nafasi ya kununua gari ambayo ataitumia kwa kujinafasi na familia yake bila kiambukizana fungus za ngozi kwenye dala dala nafasi anayo

Eti aogope kununua gari eri kisa tu hana biashara hahaaa umasikini huu haki

Gari kwa sasa ni basic need aisee ana ni muhimu kuliko unavyo dhani , nyumba ina nanafasi yake na gari pia ina nafasi yake hakuna kinacho mtegemea mwenzie hapo.

Ushauri nunua gari kwa matumizi ya familia pua malizia kibanda chako , IST ni gari ambayo kwa kipato chako unaweza kuimudu vyema kabisa, achana na hao wenye mawazo ya kimaskini eti huwezi kukopa ukanunua gari ni umasikini tu wa fikra maana usumbufu unao upata ikiwa huna gari na hasa kama unafamilia ni afadhari ukope ununue gari mpange matumizi ya kipato kinacho baki.

Kikubwa nunua gari unayo weza imudu kiuendeshaji kama kipato chako ni cha kati kama IST,corolla spacio,runx&alex, na mengine ya aina yake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom