Nimechoshwa na kuombwa pesa kila siku na vijana

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,600
8,741
Najua nasemea wengi 70% ya Watanzania ni chini ya miaka 25. Mpaka 35 itakuwa karibu 85%. Kumekuwa na utamaduni wa vijana kuombaomba pesa kila siku nimevumilia lakini inabidi niseme ukweli nimechoka.

Yaani tuna wazazi wa miaka 60-80 halafu tunatumia pesa badala ya kusaidia wazazi kila siku vijana wanatafuta mbinu za kutubomu. Wamekuwa wepesi kushinda kwenye mitandao zaidi kujua kila aina ya siasa na wasanii lakini hakuna kazi, kipato wala hata

Kibaya zaidi wengi hawana hata ubunifu wala maamko. Ugumu wa maisha haujaanza leo wakati nikiwa kijana zaidi miaka ya mwisho ya 90’s na 2000’s tulikuja na mwamka wa wakati ule kutafuta shule nyingi kwa shida bila mitandao lakini Watanzania walienda Dunia nzima miaka ile sio kwa kupenda lakini kulikuwa na uhaba wa vyuo.

Hatukuwa ombaomba tulitafuta mbinu. Siku hizi hata na mitandao ukiuliza ni wanavyuo wangapi wametafuta scholarship utapata wachache pamoja na kuwa na simu na kila kitu online. Yaani kwenye maendeleo hata kumsaidia kijana wa siku hizi wewe ndiye umuombe na kumuuliza kuhusu maendeleo yake mwenyewe na wanasiriki hata kukukwepa ukikazania sana kuongea mambo ya maendeleo. Sisi mbona hatukusubiri serikali miaka ile siku hizi ni kusingizia na kushabikia tu lakini hamna utekelezaji.

Vijana wanaoa wakati hawana kazi wala chochote halafu baada ya mwaka ni matatizo tu. Wengine wanasubiri wazee wao wafe ndiye wapate nyumba au hata kupigana kwa vitu vya wazazi. Hii generation ya vijana waliozaliwa kuanzia miaka ya 1985-2000 ni zero na kama wasiikobasilika wanashida maana wanashindana na Dunia nzima siku hizi. Nitaandika zaidi lakini nimeamua kama siku kitu cha kujiendeleza si saidii kijana

Yanni hata diaspora watakuambia ukienda TZ watu wakwanza kukucheka ni hawa vijana kwanini hujajenga, umepoteza muda wakati wenyewe wanakuomba pesa wewe! Nimekuwa frustrated sana na hawa vijana kuomba omba pesa kila siku. Binadamu tunaomba misaada lakini kwa wakati wa shida kama misiba au harusi sio kila wakati.
 
Vyuma aisee.
Si kwa kupenda
Hata ukiwa mbunifu vp vyuma meku
Ila ni kweli aisee usemayo.
Kuna mmoja kaomba kataja mpk mwezi anaotaka nimpe mpunga. nikampa shida zangu nikataja shida zangu zitaendelea mpk kipindi flani miezi kadhaa baada ya ule mwezi anaotaka yeye pesa.
Balaa nakuambia, bado ana ng'ang'ania eti hamna neno usijali hata hiyo miezi ya mbele. Khaaa nkamuambia kimoyo moyo usintanie mm. Shida gani hizo ambazo zinakua "interpolated" aka "previewed"
 
Kazi yao ni kuombaomba na kulialia mitandaoni! Badala ya kutafuta fursa mitandaoni wao wanatafuta umbea
- Hata hapa JF thread wanazo changia ni zile zisizokuwa na tija kwao
- Mfano ni wachche au hakuna kabisa wanao changia mada kwenye thread za member kama GLOBAL CITIZEN ambazo zianwapa kitu cha ziada cha kufanyia kazi na kubadili mtazamo wao: > https://www.jamiiforums.com/search/4551571/
- Ila hao hao vijana wako busy wanatafuta eti_ Connection ya kuona video mpya ya nani sijui. Inasikitisha
 
Kazi yao ni kuombaomba na kulialia mitandaoni! Badala ya kutafuta fursa mitandaoni wao wanatafuta umbea

Umemaliza, nimekuja stajaabishwa sana na wabongo hasa wa JF kuwa ukiona idea fulani imework kwako ni vizuri ukashare na mwenzako. I mean kushare fursa mbali mbali. Lakini kumbe kuna watu wanakuona unaringa, yaani mtu anaamua kukuamsha usingizini unamwambia unaringa? Like serious? Kuna kipindi nilijiuliza sana kwanini matajiri hawashare siri ya utajiri wao? Kumbe jibu nimelipata, akishare mtu ataanza kukukebehi unaringa kumbe wewe unaongea kwa nia nzuri kabisa. Wanajf ni kwikwi. Mimi nimejifunza sana aisee hapa JF kwa njia ngumu sana
 
- Hata hapa JF thread wanazo changia ni zile zisizokuwa na tija kwao
- Mfano ni wachche au hakuna kabisa wanao changia mada kwenye thread za member kama GLOBAL CITIZEN ambazo zianwapa kitu cha ziada cha kufanyia kazi na kubadili mtazamo wao: > https://www.jamiiforums.com/search/4551571/
- Ila hao hao vijana wako busy wanatafuta eti_ Connection ya kuona video mpya ya nani sijui. Inasikitisha
Huyu Global citizen ana madini sana. Huwa nasoma kimyakimya naenda kutafakari
 
Uta-share nini na mtu ambae anaamini huwezi kufanikiwa bila kuiba,kuroga na vitu kama hivyo? Chochote utakachosema utaambiwa kuna mambo nyuma ya pazia unaficha. Dawa ni kunyamaza na kusoma kimya kimya


Nimejifunza somo kubwa sana. Hakuna shid kukaa na jamii isiyoamini katika kujituma kwa nguvu utaona mafanikio!
 
Back
Top Bottom