Nimechoshwa na kuombwa pesa kila siku na vijana

Nilitaka nigonge like 1000 ila haiwezekani,hili tatizo si kwa vijana tu hata watu wazima nao wamo,yaani mpaka inafikia hatua mtu unakuwa namba ya watu wako wa karibu tu,ambao una uhakika hawawezi kukupiga mizinga.
Na ukishampa mmoja kosa la jinai ,wanaanza kuambiana fulani hana noma ongea naye atakupa tu,mwisho wa siku unajikuta unatoa misaada zaidi kwa watu wa nje kuliko hata wazazi wako au hata nduguzo wa kuzaliwa,halafu siku ukiyumba haohao wanakuwa wa kwanza kukupaka ,chondechonde jamani Kila mtu apambane na maisha yake tuache hii tabia ya ukupe.
 
Kamundu,

Acha kutukana watu mkuu. Kisa wewe umezaliwa 1984 ndio unajiona mjanja na kutukana watu.

Kuna self made millionaires kibao unatutukana.
 
Drat, Kwa kuwa umeongelea kundi na ukaweka miaka ya 1985 - 2000, basi na mimi nitaanzia hapo kwenye waliotangulia wametufikisha hapa, nakuunga mkono.
 
kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe, na mbuzi atakula kima cha urefu wa kamba yake.

kadili tunavyosonga mbele fursa zinazidi kubana kwa sababu mzunguko wa pesa umezorota.

kinachoendelea ni kubanwa zaidi wale ambao wapo kwenye mifumo rasmi, tukiamini wana unafuu lakini hawana unafuu nao wamepigika sana kwa marejesho ya mikopo na nk.

ni vizuri ukamueleza mtu kwa nini nashindwa kukusaidia, sio unajikamua kusaidia hadi mwenyewe unapauka.

Hasara Umfika Mwenye Mabezo
 
Kwanza naomba niseme uzi umenihuzunisha sana kwasababu mimi ni mmoja wa vijana katika umri huo...
Lakini ngoja nikuvunjie hapa ukweli wa hali halisi....

Kizazi chetu kimeathiriwa na vitu vifuatavyo:-
MFUMO WA ELIMU umetufanya tuwe tegemezi wa ajira sana kuliko ubunifu binafsi na ujasiriamali yaani nakumbuka hata tukiwa shule kiutaniutani mwalimu anakwambia EGM maana yake ni Expected General Manager tena wanakupa story za makampuni makubwa so unasoma ukiwa na fikra fulani tegemezi kwa ajira......

UKOSEFU WA AJIRA: baada ya mfumo wa elimu kukuandaa kutegemea ajira sasa unamaliza shule unakuja mtaani unakutana na kisanga kingine kabisaaa cha ukosefu wa hizo ajira na ubaya zaidi watanzania wengi hatuna transparency so kuambiana ukweli ni shida.. Utaanza kudanganywa na ndugu, marafiki na wengi watakwambia lete cheti huku! Lete CV huku! na ww unakaa kusubiri tu muda unazidi kwenda.. Bila ya kuwa na plan B ndio unaishia kupiga vizinga na kushinda mitandaoni hopelessly....

UGUMU WA MAISHA KATIKA AWAMU YA TANO YA UONGOZI:- hapa naomba tuwe wawazi jamani awamu hii ya uongozi imeleta changamoto sana ya maisha kuliko iliyopita ndio maana hata issue ya upungufu wa ajira haikusikika sana awamu iliyopita kutokana na unafuu wa maisha... Mfano sasa hivi unaona watanzania hawazungumzii tena siasa au kushiriki uchaguzi kwa wingi tofauti na awamu iliyopita kwasababu ni ngumu kuongea ukiwa na njaa tumboni yaani hii stlye ya kubana maisha ili watu wawe busy na vitu vingine imefanikiwa... Jamani familia nyingi zina maisha magumu sana kwa sasa na hii ni hatari sana kwa nchi na uongozi mzima inaweza ibua matatizo mbeleni huko.... (Mtoa uzi naamini awamu iliyopita hukuwahi pata vizinga sana)

UTANDAWAZI:- hapa naomba nicheze na social networks.. Kutokana na ugumu wa maisha na ukosefu wa ajira vijana wengi wakakimbilia kwenye mitandao ili kupunguza makali na kupoteza muda kidogo.... Wasichokijua mitandao ina addiction kama dawa za kulevya yaani ukisha ingia inakuchanganya akili haswaa (wahanga wananielewa, yaani ukiingia mtandaoni unajikuta unapoteza muda mrefu bila kutegemea hii ni kwa sababu ubongo unapigwa na butwaa kwa kukuta taarifa nyingi kuliko uwezo wa ku process) na wakuu wa dunia wanaitumia kufanya Mass control kwa kupenyeza ajenda za kipuuzi ambazo vijana tunazikuta na kuzibeba bila kujua purpose yake... (JAPO MITANDAO INA POSITIVE SIDE YAKE)

Natamani kuendelea lakini let me jump to solutions:-
AJIRA:- Kuna trick mimi huwa napenda kuwaelekeza watu "Katika mazingira magumu ya ajira kama una degree bhasi tafuta kazi za form6 au diploma au form4 kwanza then piga show hapo huku unaangalia channels zingine maana ni rahisi sana kupata kazi ukiwa kwenye kazi kuliko ukiwa nje ya kazi maana inaweza tokea ukapandishwa cheo hapo ulipo au kutokana na utendaji wako wa kazi ukapata shavu sehemu nyingine" TATIZO vijana hatupendi kujishusha.
UJASIRIAMALI:- Hapa unatakiwa kuwa mbunifu sana, tumia mitandao ya kijamii, usiwe muoga wala aibu kwenye kutafuta pesa.
Ikiwezekana hama mtaa au mji kabisa tafuta sehemu ambayo utakuwa comfortable kufanya mambo yako..
Ahsanteni..
VIJANA TUACHE UVIVU NA UJINGA NDIO CHANZO CHA VIZINGA.
 
Ukiona mtu anakusumbua sanaa mara mizinga mara kelele za hapa na pale Mkopeshe afu usimudai hatakusumbua kabisa na namba yako atafuta
 
Nilikua nahesabu watu walinipiga mizinga nilivoenda mtembelea mama week mwanzoni, wamefikia 14....dah raia hawa
 
Kwanza naomba niseme uzi umenihuzunisha sana kwasababu mimi ni mmoja wa vijana katika umri huo...
Lakini ngoja nikuvunjie hapa ukweli wa hali halisi....

Kizazi chetu kimeathiriwa na vitu vifuatavyo:-
MFUMO WA ELIMU umetufanya tuwe tegemezi wa ajira sana kuliko ubunifu binafsi na ujasiriamali yaani nakumbuka hata tukiwa shule kiutaniutani mwalimu anakwambia EGM maana yake ni Expected General Manager tena wanakupa story za makampuni makubwa so unasoma ukiwa na fikra fulani tegemezi kwa ajira......

UKOSEFU WA AJIRA: baada ya mfumo wa elimu kukuandaa kutegemea ajira sasa unamaliza shule unakuja mtaani unakutana na kisanga kingine kabisaaa cha ukosefu wa hizo ajira na ubaya zaidi watanzania wengi hatuna transparency so kuambiana ukweli ni shida.. Utaanza kudanganywa na ndugu, marafiki na wengi watakwambia lete cheti huku! Lete CV huku! na ww unakaa kusubiri tu muda unazidi kwenda.. Bila ya kuwa na plan B ndio unaishia kupiga vizinga na kushinda mitandaoni hopelessly....

UGUMU WA MAISHA KATIKA AWAMU YA TANO YA UONGOZI:- hapa naomba tuwe wawazi jamani awamu hii ya uongozi imeleta changamoto sana ya maisha kuliko iliyopita ndio maana hata issue ya upungufu wa ajira haikusikika sana awamu iliyopita kutokana na unafuu wa maisha... Mfano sasa hivi unaona watanzania hawazungumzii tena siasa au kushiriki uchaguzi kwa wingi tofauti na awamu iliyopita kwasababu ni ngumu kuongea ukiwa na njaa tumboni yaani hii stlye ya kubana maisha ili watu wawe busy na vitu vingine imefanikiwa... Jamani familia nyingi zina maisha magumu sana kwa sasa na hii ni hatari sana kwa nchi na uongozi mzima inaweza ibua matatizo mbeleni huko.... (Mtoa uzi naamini awamu iliyopita hukuwahi pata vizinga sana)

UTANDAWAZI:- hapa naomba nicheze na social networks.. Kutokana na ugumu wa maisha na ukosefu wa ajira vijana wengi wakakimbilia kwenye mitandao ili kupunguza makali na kupoteza muda kidogo.... Wasichokijua mitandao ina addiction kama dawa za kulevya yaani ukisha ingia inakuchanganya akili haswaa (wahanga wananielewa, yaani ukiingia mtandaoni unajikuta unapoteza muda mrefu bila kutegemea hii ni kwa sababu ubongo unapigwa na butwaa kwa kukuta taarifa nyingi kuliko uwezo wa ku process) na wakuu wa dunia wanaitumia kufanya Mass control kwa kupenyeza ajenda za kipuuzi ambazo vijana tunazikuta na kuzibeba bila kujua purpose yake... (JAPO MITANDAO INA POSITIVE SIDE YAKE)

Natamani kuendelea lakini let me jump to solutions:-
AJIRA:- Kuna trick mimi huwa napenda kuwaelekeza watu "Katika mazingira magumu ya ajira kama una degree bhasi tafuta kazi za form6 au diploma au form4 kwanza then piga show hapo huku unaangalia channels zingine maana ni rahisi sana kupata kazi ukiwa kwenye kazi kuliko ukiwa nje ya kazi maana inaweza tokea ukapandishwa cheo hapo ulipo au kutokana na utendaji wako wa kazi ukapata shavu sehemu nyingine" TATIZO vijana hatupendi kujishusha.
UJASIRIAMALI:- Hapa unatakiwa kuwa mbunifu sana, tumia mitandao ya kijamii, usiwe muoga wala aibu kwenye kutafuta pesa.
Ikiwezekana hama mtaa au mji kabisa tafuta sehemu ambayo utakuwa comfortable kufanya mambo yako..
Ahsanteni..
VIJANA TUACHE UVIVU NA UJINGA NDIO CHANZO CHA VIZINGA.

Umejitahidi sana kueleza vizuri poleni. Kitu kimoja kina nishangaza kwenye kizazi chenu ni kwamba hamtafuti michongo mfano kuna wakubwa wengi sana sana wapo tayari kuwapa njia lakini kibaya madogo badala ya kuomba mipango wanaomba pesa. Mfano miaka michache kama 5 niliwapa wapa vijana njia ya kupata ajira wakiwa sehemu yeyote Duniani kwa wana vyuo kusoma sofware fulani hivi nikawaambia kuna watu wanafanya kazi za US na Canada hasa wahindi basi badala ya kusikiliza maelezo na mbinu wakaanza kunijadili mimi na kutafuta visingizio. Mjue tu kwamba maisha sio magumu kuliko zamani maisha ni marahisi kuliko zamani ni kwamba hamfikirii “ out of the box” tofauti. Wakati sisi tunakuja nje kwanza kulikuwa hakuna watu wa kuuliza, pili kulikuwa hakuna mitandao ya kufanya application za vyuo, tatu kila kitu mnatuma kwa DHL bila msaada wa wazazi, nne yulifanya mitihani ya english ya kimataifa, tano kulikuwa hakuna hata nafasi za vyuo bongo ukipata 3 unapelekwa ualimu, kulikuwa hakuna simu za mikonon. Pamoja na yote hayo tulipenya sasa sijui ni kudekezwa au bongo flava na hii mitandao ndiyo imedumaza vijana. Mimi mara ya mwisho kupewa pesa nilikuwa na miaka 21 na ni pesa ya ticket na muhula mmoja wa shule sijawahi kuomba pesa tena kwa miaka 20 sasa na nilikuwa sijui mtu. Na sio mimi tu kizazi chetu wengi walikuwa wana uchungu zaidi. Kila siku unatakiwa kuwa mwanafunzi mpaka leo watu tunajifunza
 
Mkuu kweli vijana wanaomba na wewe kweli una pesa, kuomba sana ni kosa inaonekana na inaonekana umewasaidia financially mpaka umechoka, na naamini kuna walokuomba ambao ni watu wa karibu yako na ukawasaidia pia. Je ni wangapi umewasaidia labda kujikwamua kiuchumi nao wawe kama wewe, kwa kuwapa mitaji, mawazo na usimamizi ( ambalo ndio swala gumu katika kudevelop kwene biashara) , kama hili hujafanya usilalamike mkuu sio kila mtu ana mentality ya kuhustle, sisi tumejifunza kuhustle tukiwa wadogo sana, rai yangu ni kwamba ni bora uwaonyeshe njia ya kupita kuliko kuwapa hizo elfu kumi zako haziwez kuwasaidia... Usiwape elfu kumi alafu ukaja huku kuwasema hiyo sio poa...OVA

NB: wazee punguzeni kuomba mnapigwa majungu na watoa misaada, sio kila anaekupa msaada ana nia njema ya kukusaidia wengine watakupa msaada ili wakikaa vijiwen wanakuwa na vivid example ya kujustify kile wanachokisema na wewe ndio unakuwa mfano mkuu..TUPIGE KAZI 🤣🤣🤣


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
sio ajabu unajaribu kuwakwepa hao madogo sababu waswahili usema
"watu wakipata ujitenga"

nipo bize, nimebenwa sana, lengo kuepuka karaha za kuombwa ombwa pesa. tunaomba tu bila sababu etii?

Hasara Umfika Mwenye Mabezo
 
Hii ndiyo misingi mnayowajengea ninyi wazee wa miaka ya 1960.
Mnapolalamika mkiwa hai mtambue ipo siku watawakabeni na kuwatoa roho zenu ili waishi.
Hii ndiyo Tanzania mnayojinasibu kuijenga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom