Nimechoka kunyongwa usiku wa manane, tafadhali msaada wa haraka

Tai jike ni hivi epuka kula chakula cha kushiba sana,jifunze kulala na tumbo siyo na mgongo, chukua kitunguu sahum uweke ndani ya mto na badilisha huo mto unao lalia, na je huko ndani kwako unakaa na nani
 
Mpe yesu maisha yako kwanza uokoke uache dhambi utafte kanisa la kiroho lenye nguvu za Mungu ukae apo ulelewe kiroho ayo mavitu yataisha
 
mpokee Yesu afanyike mwokozi wako hayo majinamizi yatakimbia hayakai kwenye nuru ya utukutufu wa Mungu
 
una paroxysimal noctunal dyspnoea secondary to delusional disorder.. ni PM namba yako kama unatak msaada wangu
 
Mahali nimefika nimekata tamaa kabisa kwa maana sioni nafuu ya tatizo langu. Ninafanya maombi kwa sana kila siku kabla ya kulala lakini cha kushangaza huwa nanyongwa na watu usiku na kulishwa vitu ambavyo sivijui. Sasa naona bora nitumie njia za kienyeji kuliko kuendelea na maombi. Wana bodi ninavyoandika hapa sina raha kabisa katika ujana wangu kutokana na vitu vinavyotokea usiku nikiwa nimelala. Hivyo kama kuna anayejua njia mbadala ya kukabiliana na wachawi pamoja na wanga anipe japo hata namna ya kufanya ili niwe na amani. Nawasilisha»»»»»»»»»»
Inaendelea
Ikiwa kama miezi kadhaa numetulia bila kukabwa. sasa hivi karibuni mwezi wa tisa nimeanza kukabwa tena bila kukoma hata usiku mmoja.
Mchungaji kiongozi Gwajima alikuja arusha ktk viwanja vya relli nilienda pia lakini cha kushangaza nilirudi home hali ikawa ni ile ile.
Ndugu wadau siamini katika giza lakini hali niliyofikia sina budi.
Bado unanyongwa?
 
USHAURI & MTAZAMO:
Imani: hii ina maana ya kwamba huwa hauna imani kwa kile unachoomba, na kukifanya kwa ujumla, imani ndio kila kitu katika uongozi na mfumo wa kiroho.

Kwanza ukiomba omba kwa kumaanisha, sio ili mradi umeomba,
Pili: ukilala kitandani jaribu kula na vitabu vitakatifu vya mungu kitandani hata wanaokuja kukunyonga inakuwa ngumu kama kuna kitabu kitakatifu cha mungu huwa wanaogopa sana.

Mara nyingi kuna vitu ambavyo watu wengi hushindwa kuvielewa na kuamini,
Kumbuka uchawi upo, na dawa ya kukomesha uchawi ni kupotezea,
Mfano: ukilala unahisi kunyongwa we lala kama hamna kitu kinatokea au hata usioneshe hata dalili za kukerwa pindi ubaponyongwa kwa muda mfupi tu, watakuwacha.
Lala na shuka jeusi aina ya kaniki, hii husaidia pale wachawi wanapokuja usiku kuwanga au kukunyonga hushindwa kukuona, wakija wanaona kama hamna mtu kitandani, lakini kumbe umelala usingizi mzuri.

Kidokezo:
Kumbuka imani yako ndio itafanikisha zoezi hili hao waweza ikawa ni majini mara zote na hawa viumbe huwa na nguvu za ajabu sana,
Cha msingi imani yako iwe na nguvu haswa, ni vizuri ulale na kitabu cha dini kama biblia, au Quran itakusaidia kupunguza tatizo ila usiache kuomba,
Na usiende kwa hayo makanisa ya ajabu sijui gwajima, rweakatare, kakobe, mzee wa upako, hawa wenyewe husambaza matatizo kwa waumini na kujifanya kuwaombea.

Zingatia maelezo niliyokupa kwa ufasaha, tatizo likijirudia njoo nijulishe nikupe mbinu nyingine.
 
Kwa kawaida wanga huwa hawakabi kwa mikono ila wanakukalia usoni kwa ushauri wangu wakikukaba kwanza nawa uso maana
 
USHAURI & MTAZAMO:
Imani: hii ina maana ya kwamba huwa hauna imani kwa kile unachoomba, na kukifanya kwa ujumla, imani ndio kila kitu katika uongozi na mfumo wa kiroho.

Kwanza ukiomba omba kwa kumaanisha, sio ili mradi umeomba,
Pili: ukilala kitandani jaribu kula na vitabu vitakatifu vya mungu kitandani hata wanaokuja kukunyonga inakuwa ngumu kama kuna kitabu kitakatifu cha mungu huwa wanaogopa sana.

Mara nyingi kuna vitu ambavyo watu wengi hushindwa kuvielewa na kuamini,
Kumbuka uchawi upo, na dawa ya kukomesha uchawi ni kupotezea,
Mfano: ukilala unahisi kunyongwa we lala kama hamna kitu kinatokea au hata usioneshe hata dalili za kukerwa pindi ubaponyongwa kwa muda mfupi tu, watakuwacha.
Lala na shuka jeusi aina ya kaniki, hii husaidia pale wachawi wanapokuja usiku kuwanga au kukunyonga hushindwa kukuona, wakija wanaona kama hamna mtu kitandani, lakini kumbe umelala usingizi mzuri.

Kidokezo:
Kumbuka imani yako ndio itafanikisha zoezi hili hao waweza ikawa ni majini mara zote na hawa viumbe huwa na nguvu za ajabu sana,
Cha msingi imani yako iwe na nguvu haswa, ni vizuri ulale na kitabu cha dini kama biblia, au Quran itakusaidia kupunguza tatizo ila usiache kuomba,
Na usiende kwa hayo makanisa ya ajabu sijui gwajima, rweakatare, kakobe, mzee wa upako, hawa wenyewe husambaza matatizo kwa waumini na kujifanya kuwaombea.

Zingatia maelezo niliyokupa kwa ufasaha, tatizo likijirudia njoo nijulishe nikupe mbinu nyingine.
Huu ushauri wa kichawi
 
Unalala vibaya hadi njia ya hewa inajikunja hii hali huwatokea wengi na kuamini ni wachawi ila mlalo wako ndio uchawi jaribu kulala vizuri na hakikisha mwili hauchoki sana maana mwili ukichoka sana hufanya ulale bila mpangilio na kujikunjakunja shingo mishipa ya hewa inajikunja na we we kukosa kupumua vizuri kula mapema na Muombe MUNGU YEYE NI MUWEZA WA KILA KITU HAPA DUNIANI
 
Unalala vibaya hadi njia ya hewa inajikunja hii hali huwatokea wengi na kuamini ni wachawi ila mlalo wako ndio uchawi jaribu kulala vizuri na hakikisha mwili hauchoki sana maana mwili ukichoka sana hufanya ulale bila mpangilio na kujikunjakunja shingo mishipa ya hewa inajikunja na we we kukosa kupumua vizuri kula mapema na Muombe MUNGU YEYE NI MUWEZA WA KILA KITU HAPA DUNIANI
Yes, hii husababishwa na tabia ya kulalia tumbo na pili kulalia ubavu wa kushoto na hili la kulalia ubavu wa kushoto huwa linasababisha kubana vena cava (ambayo ipo located left side) na kusababisha damu kuflow kwa kiwango kidogo then suply ya O2 inakuwa ndogo mwilini baadae unapoteza nguvu unadhani UNANYONGWA
 
Gwajima ni miongoni ya wanaokaba usiku hivyo si ajabu wanaokukaba anawajua. Lala na bibilia kwenye kichwa chako na mwambie Mungu atume malaika wailinde nyumba yote na kuwazuia wanaokukaba
 
Nadhani utakuwa shuhuda mzuri kuwa uchawi na ushirikina vipo!! Tafuta wataalamu wa kienyeji, Kuna vitu umetupiwa kwenye nyumba yako vikushughulishe uvuruge pesa urudi nyuma kimaendeleo.Unaweza shangaa na nduguzo wamo kwenye mchezo huo !
 
Back
Top Bottom