Nimebaini mke wangu amezaa nje ya ndoa na amekiri, naombeni ushauri

Naomba niende kwenye mada, mm na mke wangu tulioana mwaka 2015 japo tulianza mahusiano muda mrefu kidogo na mtoto wetu wa kwanza tulimpata mwaka 2013, na wapili mwaka 2018.
Nilihamishwa kikazi kutoka dar kwenda moja wapo ya mikoa ya kanda ya ziwa, hiyo ilikua mwaka 2019 ikabidi wife na watoto wabaki huko mkoa jirani na dasalamu yaliko makazi yetu ya kudumu.
Sababu ya kuibakiza familia huko ni kwamba first born wetu alikua anasoma na ukizingatia huku nilikohamia bado sijajiimarisha vyema.
Nilikua naenda kuwatembelea mara kwa mara na wao pia niliwapa fursa ya kua wanakuja ninakofanyia kazi mara tu shule zilipokua zikifungwa. Nilipanga kuihamisha familia yangu kuja kuishi na mm mara baada ya kukamilisha taratibu za kumhamisha binti yangu kipenzi na pia kumpata mtu sahihi atakaeishi kwenye nyumba yangu.
Mwaka Jana mwanzoni mwa mwezi wa sita mke wangu alinipigia cmu akanieleza kwamba anataka kuhamia huku niliko hivyo nianze taratibu za uhamisho, nami bila kufanya hiana nikaanza hatakati za kupata nafasi ktk shule nzuri za private ktk mkoa huu baada ya shule kufungwa wife na watoto wetu wawili wakatia nanga dogo akaenda akapiga paper akafaulu akapata nafasi hiyo ni mwezi wa saba 2021.
Maisha yakaendelea, mwezi wa nane wife akanambia ana mimba, tukaenda kuhakiki kweli nikadhibitisha ni mjamzito sikutaka kuhangaika na mambo ya mimba ina muda gani
Harakati za CLINIC zikaanza tukaenda tukacheki afya wote tupo sawa japo wife alinihofia Sana kua yawezekana nimeshakanyaga waya
Ilipofika mwezi wa 12 wife akaanza kunambia UNAJUA SIKU HIZI MAMBO YAMEBADILIKA SANA MJAMZITO ANAWEZA KUJIFUNGUA HATA MIEZI TISA HAIJATIMIA, mm nikawanamuuliza hayo mabadiliko yameanzia kwako au ni kwa wajawazito wote na je hiyo ni sayansi ya wapi huku nikimtania kua mbona hiyo mimba yako nikipiga hesabu ulivyofika hapa na jinsi inavyoonekana ni tofauti,(mimba ilionekana kubwa)
Ukweli ni kwamba wife alifika huku ninakoishi mwezi wa saba Kati ya tarehe 15 hadi 23 mwezi wa saba
Kwa haraka haraka kama ni mimba niliipigia hesabu za mwezi wa nane na kama nikujifungua basi itakua mwezi wa nne katikati au mwishoni kabisa
Kilichonishtua ni mke wangu KUJIFUNGUA tarehe za mwisho wa mwezi wa pili huku mimba ikiwa imemchosa Sana ( mtoto wa kiume,ambae Sasa ni mtoto wetu wa 3)
Kilichoanza kunishtua wife anakomalia mtoto apewe jina W na mm nasema kama mm ndie baba wa huyo mtoto basi ataitwa jina Q, tukaendelea kutana Sana na ikumbukwe mm nashinda Sana kazini hivyo hata wakubwa zake wakawa wanamuita jina hilo analolitaka mama yao ikabidi niwapige marufuku kumuita mdogo wao jina hilo na hadi fimbo zilitimika ndio kwa mbaali wakapunguza
Jina hili limeendelea kuitwa na kitajwa na waumini wenzake na wife hata wakija kumtembelea utasikia wanamuita jina hilo mm nakausha naamua kusepa zangu naenda kumwagilia moyo

Ikabidi nikae na wife nimuulize kinagaubaga juu ya kweli wa mimba kujifungua jina pamoja na mtoto kutokuonyesha dalili za kuwafanana wakubwa zake Wala mm Wala yy mwenyewe, wife hakusema kitu japo alionekana kuna jambo anaficha
Niliendelea kumuuliza pasipo kumpiga Wala kuhombana ndipo wife alipoamua kunichana ukweli huku akimsingizia shetani na kunilaumu mm kua nilikua mbali nae akateleza mara moja akafanya ndo ikawaimetokea hivyo, nikatulia sikumshirikisha mtu mwingine hata kidogo maisha yakaendelea lkn moyoni naumia Sana,
Na kadri siku zinavyozidi kwenda nakosa uvumilivu ukizingatia natumia kilevi hua na kua na mawazo mengi Sana nikifikiria kuilea damu isiyokua yangu
Hakika kwa umri wangu huu wa chini ya miaka 35, jamani mm hili jambo limenishinda kabisa naona sitaweza kulibeba

Jana nimemweleza kaka yake mkubwa pamoja na mama yake kua mm uzalendo umenishinda nisijefanya maamuzi mengine yakagharimu pande zote mbili nimeomba mke arudi kwao au aende kwa huyo aliezaa nae mm aniache nilee watoto wangu wawili
Naombeni USHAURI WENU wadu mwenzenu Niko dilemma
NB; matusi nisingependelea kuyaona
Kwasasa hivi, mimi naona umrudishe kwao ili upate muda wa kutafakari ukiwa peke yako. Akili yako itakapotulia na kukubali kuwa kosa alilofanya mke wako ni la kawaida na hivyo huoni shida kuwa naye licha ya mapungufu aliyoonesha hapo unaweza kumrudisha. Kama moyo unagoma kusamehe, ni vema ukawa naye mbali.
Ila kuendelea kuugulia moyoni na wahusika wa maumivu wapo katika mazingira yako ni hatari kwako na familia yako( hivyo ni vema ukawa nao mbali hadi pale maumivu haya ya moyo yatakapopotea) .
 
Kisaikolojia binadamu akikumbana na changamoto, huwa kuna hatua ya kuikataa au kutoikubali, asipokuwa makini inaweza kupelekea maumivu makali yatakayosababisha kujidhuru au kumdhuru aliyemsababishia.

Kwa sasa, wakati unaendelea kutafuta ufumbuzi, nashauri umrudishe mwanamke na mwanae ambaye amekiri sio wako kwao au mpeleke mbali usikoweza kumfikia kwa urahisi. Lengo ni usalama wako, wake na wa mtoto.

Maisha yana matukio ya aina mbili, kwanza ni yale tunayoweza kufanya kitu kuyabadilisha na pili ni yale hakuna kitu tunaweza kufanya kuyabadilisha.

Unachopitia kipo kundi la pili, haya ya kundi hili, hatutakiwi kupoteza muda kutafuta ufumbuzi, kwa sababu hayana. Cha kufanya, ni kuyakubali kwamba yameshatokea, wewe sio wa kwanza na hutakuwa wa mwisho kukutana nayo.

Baada ya kulikubali tatizo, lipe muda, muda ni dawa. Wakati huko karibu na mwanamke wala huyo mtoto, akili itajikusanya na utafanya maamuzi pole pole.

Mwisho kabisa, usisahau kuhesabu ulivyobarikiwa, una watoto wawili unaowapenda na kwa vyovyote maamuzi yako yatawajenga au kuwaharibu, umebahatika kuwa na kazi inayotosha kuwalea, na hata huyo mwanamke usiache kuyakumbuka mazuri yake, ikiwemo kukuamini na kukupa nafasi ya kuwa Baba, na namna alikuwa mwema kwako kabla ya yote haya kutokea.

Asante.
 
upande wa mke ulivyowambia wakakupa majibu yapi?

Sent from my TECNO KD7h using JamiiForums mobile app
Kaka mtu kasema hata yy ni mwanaume hawezi kukubaliana na mke wake kuzaa nje ya ndoa ni bora angefanya mapenzi tu kama kweli alikua amezidiwa ikaisha lkn sio kuzaa nje hiyo ni dharau akanambia nimpeleke kwao

Mama mkwe yy anamtetea mtoto wake ananiuliza wakati anazaa nje wewe ulikua wapi nikakata cmu sikutaka kuendelea kumsikiliza
Tatizo jingine huyu wife analazimisha kua ataondoka ila lazima aondoke na watoto wake wote,
 
Naomba niende kwenye mada, mm na mke wangu tulioana mwaka 2015 japo tulianza mahusiano muda mrefu kidogo na mtoto wetu wa kwanza tulimpata mwaka 2013, na wapili mwaka 2018.

Nilihamishwa kikazi kutoka dar kwenda moja wapo ya mikoa ya kanda ya ziwa, hiyo ilikua mwaka 2019 ikabidi wife na watoto wabaki huko mkoa jirani na dasalamu yaliko makazi yetu ya kudumu.

Sababu ya kuibakiza familia huko ni kwamba first born wetu alikua anasoma na ukizingatia huku nilikohamia bado sijajiimarisha vyema.
Nilikua naenda kuwatembelea mara kwa mara na wao pia niliwapa fursa ya kua wanakuja ninakofanyia kazi mara tu shule zilipokua zikifungwa. Nilipanga kuihamisha familia yangu kuja kuishi na mm mara baada ya kukamilisha taratibu za kumhamisha binti yangu kipenzi na pia kumpata mtu sahihi atakaeishi kwenye nyumba yangu.

Mwaka Jana mwanzoni mwa mwezi wa sita mke wangu alinipigia cmu akanieleza kwamba anataka kuhamia huku niliko hivyo nianze taratibu za uhamisho, nami bila kufanya hiana nikaanza hatakati za kupata nafasi ktk shule nzuri za private ktk mkoa huu baada ya shule kufungwa wife na watoto wetu wawili wakatia nanga dogo akaenda akapiga paper akafaulu akapata nafasi hiyo ni mwezi wa saba 2021.

Maisha yakaendelea, mwezi wa nane wife akanambia ana mimba, tukaenda kuhakiki kweli nikadhibitisha ni mjamzito sikutaka kuhangaika na mambo ya mimba ina muda gani
Harakati za CLINIC zikaanza tukaenda tukacheki afya wote tupo sawa japo wife alinihofia Sana kua yawezekana nimeshakanyaga waya
Ilipofika mwezi wa 12 wife akaanza kunambia UNAJUA SIKU HIZI MAMBO YAMEBADILIKA SANA MJAMZITO ANAWEZA KUJIFUNGUA HATA MIEZI TISA HAIJATIMIA, mm nikawanamuuliza hayo mabadiliko yameanzia kwako au ni kwa wajawazito wote na je hiyo ni sayansi ya wapi huku nikimtania kua mbona hiyo mimba yako nikipiga hesabu ulivyofika hapa na jinsi inavyoonekana ni tofauti, (mimba ilionekana kubwa)

Ukweli ni kwamba wife alifika huku ninakoishi mwezi wa saba Kati ya tarehe 15 hadi 23 mwezi wa saba
Kwa haraka haraka kama ni mimba niliipigia hesabu za mwezi wa nane na kama nikujifungua basi itakua mwezi wa nne katikati au mwishoni kabisa
Kilichonishtua ni mke wangu KUJIFUNGUA tarehe za mwisho wa mwezi wa pili huku mimba ikiwa imemchosa Sana (mtoto wa kiume,ambae Sasa ni mtoto wetu wa 3)

Kilichoanza kunishtua wife anakomalia mtoto apewe jina W na mm nasema kama mm ndie baba wa huyo mtoto basi ataitwa jina Q, tukaendelea kutana Sana na ikumbukwe mm nashinda Sana kazini hivyo hata wakubwa zake wakawa wanamuita jina hilo analolitaka mama yao ikabidi niwapige marufuku kumuita mdogo wao jina hilo na hadi fimbo zilitimika ndio kwa mbaali wakapunguza.

Jina hili limeendelea kuitwa na kitajwa na waumini wenzake na wife hata wakija kumtembelea utasikia wanamuita jina hilo mm nakausha naamua kusepa zangu naenda kumwagilia moyo

Ikabidi nikae na wife nimuulize kinagaubaga juu ya kweli wa mimba kujifungua jina pamoja na mtoto kutokuonyesha dalili za kuwafanana wakubwa zake Wala mm Wala yy mwenyewe, wife hakusema kitu japo alionekana kuna jambo anaficha
Niliendelea kumuuliza pasipo kumpiga Wala kuhombana ndipo wife alipoamua kunichana ukweli huku akimsingizia shetani na kunilaumu mm kua nilikua mbali nae akateleza mara moja akafanya ndo ikawaimetokea hivyo, nikatulia sikumshirikisha mtu mwingine hata kidogo maisha yakaendelea lkn moyoni naumia Sana,
Na kadri siku zinavyozidi kwenda nakosa uvumilivu ukizingatia natumia kilevi hua na kua na mawazo mengi Sana nikifikiria kuilea damu isiyokua yangu.

Hakika kwa umri wangu huu wa chini ya miaka 35, jamani mm hili jambo limenishinda kabisa naona sitaweza kulibeba.

Jana nimemweleza kaka yake mkubwa pamoja na mama yake kua mm uzalendo umenishinda nisijefanya maamuzi mengine yakagharimu pande zote mbili nimeomba mke arudi kwao au aende kwa huyo aliezaa nae mm aniache nilee watoto wangu wawili
Naombeni USHAURI WENU wadu mwenzenu Niko dilemma

NB; matusi nisingependelea kuyaona



Umeamua vizuri. Usikubali kufanya tofauti na hivyo ulivyoamua.
 
Kwasasa hivi, mimi naona umrudishe kwao ili upate muda wa kutafakari ukiwa peke yako. Akili yako itakapotulia na kukubali kuwa kosa alilofanya mke wako ni la kawaida na hivyo huoni shida kuwa naye licha ya mapungufu aliyoonesha hapo unaweza kumrudisha. Kama moyo unagoma kusamehe, ni vema ukawa naye mbali.
Ila kuendelea kuugulia moyoni na wahusika wa maumivu wapo katika mazingira yako ni hatari kwako na familia yako( hivyo ni vema ukawa nao mbali hadi pale maumivu haya ya moyo yatakapopotea) .
Nimepokea USHAURI wako mkuu
 
Wataalamu munisaidie ku attach Uzi wangu usemao "Hakuna ndoa ambayo mume na mke wanaishi sehemu tofauti "
Ndoa yenu ilivunjwa na kazi.
Kila siku nasema usikubali kukaa mbali na mke wako hata kwa miezi 2.
Na wanaume hata wakikaa wiki 2 tu inatosha kusaliti wake zao
Huu ndio ukweli wa mambo.
Mie nasema tugegeduane tuu jameni. Haya mambk ya ndoa kwa hizi lifestyle zetu za mke njombe mume tanga tunadanganyana tuu jameni
 
Ushaur wangu ni bora ufate kka

Mwondoe mkeo mazingira ya krb na wewe kwa sasa
Hii hali ikipita within time utaheal na unaweza samehe au kutosamehe
Ukiendekea kukaa nae karb nakuhakikishia kuna siku atakuudhi au kukujibu vibaya utainganisha na hasira za usaliti utamfanya kitu dunia itakushangaa

Jiepushe na kesi zisizo za lazima mpeleke kwao upumzike miez kadhaa ndo muone solutio

Pls narudia hata kama unamsamehe usikae nae kwa muda huu utaua ndg
 
Kitanda hakizai haramu lea mtoto. Wanakuwaga na vipaji vikubwa baadae.
Ninayo mifano mingi.
Ila kama mkeo bado anakupenda.

Kama mke hakupendi basi achana naye
Sina tatizo na hilo isipokua naweza sema acha nilee nisomeshe na ili ndugu zake wasigundue lazima na yeye aende private school kama wao, kama ulivyosema wanakuaga na vipaji, kesho mke wangu atanigeuka na kumueleza mtoto ukweli kuhusu mimi na kingine kama nilivyosema hapo awali, nina miaka 31 nahitaji kurudi shule kuongeza elimu na mke wangu atatakiwa kurudi kule nyumbani kwetu yaani kwenye makazi yetu ya kudumu akiwa na watoto.

Huoni kwamba ataendelea na mawasiliano na yule mwanaume kama alishindwa kuvumilia miezi miwili ataweza kuvumilia miezi minnee plus na kwa miaka mitatu.

Huoni naweza kuja kujikuta nimeua ndugu yangu
 
Ushaur wangu ni bora ufate kka

Mwondoe mkeo mazingira ya krb na wewe kwa sasa
Hii hali ikipita within time utaheal na unaweza samehe au kutosamehe
Ukiendekea kukaa nae karb nakuhakikishia kuna siku atakuudhi au kukujibu vibaya utainganisha na hasira za usaliti utamfanya kitu dunia itakushangaa

Jiepushe na kesi zisizo za lazima mpeleke kwao upumzike miez kadhaa ndo muone solutio

Pls narudia hata kama unamsamehe usikae nae kwa muda huu utaua ndg
Asante Sana kwa USHAURI mkuu nitazingatia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom