Vyanzo vizuri zaidi vya madini ni mifupa na chokaa chokaa. Vyote hivi vinapatikana kwenye maduka ya vyakula vya mifugo. Pia waweza tumia DCP au Premix.

Chanzo kizuri zaidi cha protein ni soya. Ila kumbuka protein yoyote itokanayo na mimea hukosa elementi mbili za Lysine na Methionine. Hivyo utalazimika kutumia premix yenye hivyo viwili ndani yake.

Hakikisha pia chakula chako kinawekwa virutubisho kwa uwiano sahihi. Mfano, protein yapaswa kuwa 16% - 22% ya chakula chote. Angalia kwenye desa la uandaaji chakula cha kuku lifuatalo.
Nimeshindwa kuki-attach. Ingia google download kitabu cha UTENGENEZAJI CHAKULA CHA KUKU cha LRDC
 
Safi sana, mimi nimeanza kufuga kuku 6, jogoo mmoja mitetea 5, sasa hivi wote wanataga nnatarajia mda siyo mrefu nitakuwa na vifaranga siyo chini ya 60, ambao nitawachukua kutoka kwa mama yao, baada ya hapo kazi yangu itakuwa kula mayai na nyama wakipungua nazalisha wengine, sifanyi kwa ajili ya biashara, ila nimegundua kufuga wanyama/ndege inakufanya uwe active sana, furaha na stress vyote vyako, kuna kuku mmoja namkubali sana sana sijui kama nitakuja kumla kwa kweli, actually hawa kuku wote nilioanza nao sitawala

Kweli kiongozi kufuga ni raha na sometimes karaha ..Mi nina kuku wangu mmoja namkubali sana mwenyewe namuitaga straika huyu akiniona ananikimbilia na kisha anaruka ruka kama vile anataka kupiga story na mimi.. dah huyu siwezi kumchinja.. kuna mwingine bwege kweli akiniona ananidonoa bila sababu na kukimbia halafu hatagi sana hata akitaga anataga viyai vidogoo huyu hana siku nyingi za kuishi .. ila kiujumla na enjoy sana kufuga hasa ktk zama hizi ambazo binadamu ni wanafiki na wambea ni bora kutumia muda wako kucheza na kuku tu
 
Kuna binadamu hawana huruma kabisaa mwaka 2017 mwisho december nilinunua kuku kutoka mbeya jumla majike na majogoo kama 70 ila mpaka hivi hela hawajaongeza kabisaa zaidi naona wamebakia 30 kila siku mfanyakazi anasema wanaumwa na kufaaaaa
Anawakukula ama anawauza
 
Safi sana, mimi nimeanza kufuga kuku 6, jogoo mmoja mitetea 5, sasa hivi wote wanataga nnatarajia mda siyo mrefu nitakuwa na vifaranga siyo chini ya 60, ambao nitawachukua kutoka kwa mama yao, baada ya hapo kazi yangu itakuwa kula mayai na nyama wakipungua nazalisha wengine, sifanyi kwa ajili ya biashara, ila nimegundua kufuga wanyama/ndege inakufanya uwe active sana, furaha na stress vyote vyako, kuna kuku mmoja namkubali sana sana sijui kama nitakuja kumla kwa kweli, actually hawa kuku wote nilioanza nao sitawala
Utawakula tu nakwambia.
 
Usijali mkuu mafanikio hayakosi changamoto hongera kwa kutokata tamaa
Nashukuru Mungu ufugaji ulienda vizuri ingawa changamoto zilikuwepo kwani kuku walikufa sana mwanzoni ila baadae walikaa vyema, walitaga mzao mmoja baada ya vifaranga kuchangamka niliwauza wale wakubwa sasa nina kizazi kipya ndio naendelea nacho
 
Msaada Wandugu... Kuku wanaokula mayai, dawa Yao NI nini ili waache..??
Kuku Kula Mayai Husababishwa Na Sababu Kuu Nne

1.Upungufu Wa Madini Ya Kalishiamu (Ca).

2.Upungufu Wa Madini Ya Potashiamu (Ka).

3.Kulisha Chakula Kichache (Underfeeding).

4.Tabia Mbaya (Vices)


Tiba:-

1.Kalishiamu.Tumia Chumvi, Dcp,chokaa Au Mifupa Kama Wanakula Mayai Na Kudonoana Manyoya.

2.Potashiamu.Wapatie Majani Yakutosha Pamoja Na Mifupa Kama Wakula Mayai Na Manyoya Yao Kuwa Rafu.

4.Tabia Mbaya.Wakate Midomo Na Kuwapunguza Kwenye Banda Kama Wamebanana Na Wanakula Mayai.

3.Kulisha Chakula Kichache.Ongeza Kipimo Cha Chakula Kama Wanakula Mayai Na Wamepungua Uzito.
 
Nashukuru Mungu ufugaji ulienda vizuri ingawa changamoto zilikuwepo kwani kuku walikufa sana mwanzoni ila baadae walikaa vyema, walitaga mzao mmoja baada ya vifaranga kuchangamka niliwauza wale wakubwa sasa nina kizazi kipya ndio naendelea nacho
Kama hautojali uniambie hapa ama PM idadi ya kuku ulionao hadi sasa...jumla kuu.

Nataka mwezi ujao nianze kufuga kuku wa kienyeji kwa njia huria ama kiholela wanajitafutia msosi
 
umeanda vizuri makara yako ila umeshindwa kuwashawishi watu zaid ya kuwatamanisha <HUU NI MTAZAMO WANGU> ume weka gharama za kununua kuku na ujaeleza chakula na gharama zake
 
Kwa observation ya comments baadhi ya watu mametoa ndio unaona jinsi gani mpaka leo wanakaa na dada zao na shemeji zao chumba kimoja. Mtu anajaribu kufungua milango ya kuiona fursa mtu anataka apewe banda, sijui apewe hao kuku kabisa huu ni uzwa zwa wa hali ya juu na kutoboa ita take muda saaana!.

Hongera sana mtoa Uzi wenye kujielewa wamenufaika kwa elimu hii kubwa.
 
Well, the idea is good but I didn't like the business plan. Your business plan lack some of the very important details when come to cost of production. A serous investor won't invest in such kind of environment.
Now, let's do this... let's calculate the cost of this enterprise all together.
Bei ya kuku 10k
Gharama ya kutengeneza banda kutosha kuku 25? What if watakapoendelea kukua na kuongezeka kua wengi nitahitaji kiasi gani kuongeza banda?
Gharama za chakula zikoje kukudhi kuku 25?
Madawa je,?
Chanjo?
Gharama za mtaalam?
Mpaka baada ya muda gani ntaanza kuuza kuku wangu? Nitauza sh ngap?
Nitamuuzia nani? (soko)
Bei ya kuuzia itanipa faida ya kurudisha gharama na kupanua zaidi biashara yangu?
To name a few, always always an entrepreneur should know how to calculate the cost!
 
Kila mwanadamu huwa ana mawazo tena mazuri sana kichwani kwake au hata kwenye makaratasi ya nini afanye ili awe tajiri na si mtu wa njaa njaaa - sasa challenge huja namna ya kuyahamisha hayo mawazo into reality hapo ndipo kwenye mtego wenyewe....

na ndiyo maana tangu kale kuna watu maskini na matajiri...
 
Mifugo kingine labda lakini kuku ni mtihani
Kuna jamaa aliniuzia dawa na kuku zangu zikawa zinakufa tu kumbe ni dawa fake
Sitaki hata kusikia ufugaji huko nimekoma

Na serikali imetulia tu
 
Fugeni chotara at least ni raisi kufugikaa ..na kutibika but soko lao pia cyo kihvyo lkn nimeona sikuhx tunalishwa sana kuku wa chotara ukizania ni wa kienyeji
 
Kwa uzoefu wangu ukianza na kuku mitetea 20,jogoo wanne maxmam ya jogoo mmoja kwa mitetea mitano,wakatamia wote mayai 12,kila mmoja,ila watapishana kwenye utamiaji,wakatotoa vifaranga 8 kila kimoja,ukawakinga na mwewe ,kunguru,paka na mbwa,mfano wakapona vifaranga vitano kwa kila mtetea mmoja,baada ya miezi 6-8 utakua na kuku 100,hapa kama unawalisha vizuri,au unashamba lenye majani na mbolea.
Kinga ya kienyeji inatosha sana unawatwangia pilipili kwenye maji yao,wanaishi vizuri mnoo
 
Mbona hujaeleza hao kuku watalala wapi,watakula nini nk?!
Huyu anaota ndoto. Kuku hawana banda, chakula cha kuanzia, hawauguwi, wanataga na kutotoa mayai yote, na vifaranga hawafi hata mmoja. Huyu ni mwandishi wa tamthilia na hajawahi kufuga kuku. Atawapoteza wengi.

Kama anataka kusaidia watu awe mkweli. Atoe mchanganuo kuanzia gharama za kibanda. Yeye ameanza na kuku 25, anazungumzia kuongezeka lakini mchanganuo huo haoneshi gharama.
 
acheni kudharau kazi za watu,kilimo,ufugaji ni kazi inahitaji uvumilivu,uzoefu,eleimu na kujitoa kweli kweli kama tu waliosoma na kupata kazi sio rahisi hivyo kama unavyofikiria mtoa mada.hakuna jambo rahisi
 
65 Reactions
Reply
Back
Top Bottom