Hata kulala naye kitanda kimoja tu, achilia mbali mambo ya kuchakatana, najisikia kama niko gerezani. Inanibidi nipige ulabu ili nimudu kulala hapo kitandani.
Appetite ya kuwa naye imekata kabisaaa. Nikimcheki alivyopauka, midevu imechachamaa utadhani yule mchezaji wa Simba ambaye huwa akifunga goli anaweka mpira kwenye nyeti zake.
Maneno yake hayana tena mvuto kwangu.
Amefulia kiuchumi. Na nafsi yangu imefulia kwake.
Nifanyeje?
ONYO: Usije na swaga eti ooh hukumpenda ulipenda fedha zake. Kwa taarifa yako wooote wanaolewa kwa kuangalia potential ya mtu kimaisha hasa hasa pesa.
Ndiyo maana unapowaeleza wazazi/ ndugu/jamaa/marafiki kuwa umepata mchumba, swali lao la kwanza huwa ni "anafanya kazi gani? Ama anajishughulisha na nini? Why this question?