Che Kalizozele
JF-Expert Member
- Jul 20, 2008
- 777
- 49
Kuna watu wawili walikuwa wamelala kwenye kitanda cha double deck,nafikiri unakifahamu,ni kile chenye kitanda juu na chini.Katika wawili hao mmoja alikuwa binti aliyekuwa amelala juu na mwingine alikuwa kidume kilichokuwa kimelala chini.Usiku wa manane yule binti akagundua wapo wawili pale juu,si ikabidi apige kelele.Watu wakaja kwa wingi si unajua binti anavyopiga kelele akiingiwa na woga.Kuwasha taa,Hamaad;Si wakakikuta kile kidume kimelala juu wakati kilikuwa kimelala kitanda cha chini.
Si ikabidi aulizwe imekuwaje yuko juu wakati anatakiwa awe amelala kitanda cha chini.
Yule jamaa akajibu,"nimeanguka,si unajua usingizi mzito"
Bwana mmoja akahamaki,"umeanguka au umepanda"
Jamaa akasisitiza,Nimeanguka mkuu,usingizi bwana" huku akishuka eneo lake la awali.
Si ikabidi aulizwe imekuwaje yuko juu wakati anatakiwa awe amelala kitanda cha chini.
Yule jamaa akajibu,"nimeanguka,si unajua usingizi mzito"
Bwana mmoja akahamaki,"umeanguka au umepanda"
Jamaa akasisitiza,Nimeanguka mkuu,usingizi bwana" huku akishuka eneo lake la awali.