n
I love it.Same to me...Kuna jumamosi(haikuwa mwisho wa mwezi) na Kuna ripoti nilikuwa sijatuma. Ile nataka kwenda ofisini kwa miguu kwa kuwa sikuwa na nauli (Mimi ni mwanaume was mikoani) mwanangu akagoma katakata nisimuache....nikipiga hatua ishirini namsikia huko akilia roho inauma narudi....boss naye anapiga simu balaa...nikitaka kuondoka mtoto analia..mwanagu alikuwa na kilo 16 nikaamua kumbeba kwenda naye kazini, umbali ni km 10 hivi. Kufika kazini yule mlinzi tu akampenda akasema mtoto mzuri, shika hii (akatoa buku mbili) nikapita floor ya chini, dada wa mapokezi akasema duh ndio una mtoto mzuri hivi(akampa buku mbili)..zote hizo nazidaka...tukaingia kwenye lift watu wakampenda pia...maza mmoja akampa buku ya pipi. Kufika ofisini Sasa nikamuwekea kiti, nikawa naandaa ripoti boss yupo pembeni...nikitaka peni namwambia C.... naomba hiyo peni, analeta...boss akitaka kuweka itv namwambia C.... mpe babu rimoti ile pale anampa boss basi ripoti nikaimaliza, ile namtumia boss tu, akampa Kwanza dogo 20 halaf akaniambia nipite kwa muhasibu....kwa mara ya kwanza (ndani ya miaka mitatu) boss alitoa nauli ya weekend.....I love my daughter