Nimeamini Mwalimu Nyerere alikuwa anaona mbali sana...Tazama hii!

Mkeshaji

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
4,262
1,416
Hii ilikuwa kauli ya Mwalimu Nyerere miaka 58 iliyopita.


nyerere_ardhi.jpg
 

Attachments

  • mwalimu.doc
    73.5 KB · Views: 666
Hii ilikuwa kauli ya Mwalimu Nyerere miaka 58 iliyopita.

Tukumbuke pia kwamba ni Mwalimu huyo huyo aliyenena miaka takribani 20 hivi iliyopita kwamba chama makini cha upinzani kitatokana na CCM no actualy "nyinyiemu" na chama alichokiona kina mwelekeo huo wakati huo alinena ni CHADEMA, now that prophesy has come true for everyone to see. Mwalimu was agreat philosopher and thinker. Kwa kweli kama watawala wetu hawa magamba wangemuenzi na kujifunza na kutenda kama maono yake yalivyokuwa Tanzania ingekuwa inapaa katika kila nyanja ya maisha. Asante Mungu kwa maisha ya Baba wa Taifa. RIP Mwalimu
 
Na lile la kuvunjika muungano na baadae kujikuta kumbe kuna wagogo, wahaya......na wazanzibara na wazanzibari nalo linakuja. Heri yetu watanganyika kama tutabaki wamoja tukikataliwa na wapemba na waunguja.
 
Mwalimu aliacha mashirika ya umma na viwanda zaidi ya 300. hatukua na chuo kikuuu hta kimoja, tukavijenga vingi na kwa taaluma tofauti. akaanzisha vijiji, tukashindwa kuviendeleza. leo tunataka kupeleka huduma mbalimbali vijijini. tutawezaje wakati watu wametapakaa huku na kule. angalia nchi za ulaya kama watu wanaishi hivyo. Hata mkapa alikiri pale mlimani city kwamba hakujenga viwanda wakati wake na tangu aondoke madarakani hilo halijafanyika vile vile. sasa tumlaumu aliyeanzisha msingi wa kujenga nyumba au walioshindwa kuendeleza ujenzi? tujaribu kuwa waungwana; historia itakuja kutusuta kama haijaanza tayari. hata umoja wa taifa na amani vinaanza kuyeyuka. Lakini Mwalimu ametutoka zaidi ya mwongo mmoja sasa lakini tunaelekea kucheza tu nduwala.
 
.
Mkuu Mkeshaji . nimeona niiweke hiyo doc yako hapa Jamvini ili kila mtu aweze kuiona ... maana unajua mpaka mtu aanze ku-download then aisome alafu arudi tena kuchangia .. naona kama inachukua muda mwingi

Anyway hii ndio quote anayoiongelea Mkuu Mkeshaji katika hii thread!


Hii ilikuwa kauli ya Mwalimu Nyerere miaka 58 iliyopita.

nyerere_ardhi.jpg
 
.
Mkuu Mkeshaji . nimeona niiweke hiyo doc yako hapa Jamvini ili kila mtu aweze kuiona ... maana unajua mpaka mtu aanze ku-download then aisome alafu arudi tena kuchangia .. naona kama inachukua muda mwingi

Anyway hii ndio quote anayoiongelea Mkuu Mkeshaji katika hii thread!


Hii ilikuwa kauli ya Mwalimu Nyerere miaka 58 iliyopita.

nyerere_ardhi.jpg
Umefanya jambo la maana sana. Hapa kwangu ilinigomea.
 
Bado tunajadili hili la mwalimu! ila kwa ufupi kikao chetu kimesha kwama kwani mwalimu alikuwa ni wa pekee kabisa katika tasnia ya utawala wa nchi yetu. Na wakati anaondoka madarakani alisema wazi kwamba

"Ni muda mrefu sasa nimekuwa napenda nipumzike kuuongoza nchi yetu ili kuwapisha wa tz wengine wenye uwezo nao wachangie kuleta maendeleo ya nchi yetu. Lakini baadhi yenu mmekuwa mkipinga mimi kung'atuka katika nafasi hii ya uongozi wa nchi kwa sababu zenu mnzozijua ikiwemo maslahi binafsi."

Mzee akang'atuka akaenda zake kijijini kwao butiama kwenda kulima. Akawaachia viwanda (vya nguo, bia, sigara, viatu, korosho, nguo, kuchambua pamba, tumbaku, mkonge, kahawa, chai, almasi n.k), reli na treni zake, ndege za ATC, mashamba ya kahawa, pamba, mkonge, chai, misitu, ardhi, meli, mabenki (Nbc & Crdb, TIB), NHC, PPF, NIC, NSSF, bodi za mazao yote ya biashara, NMC, NDC, STAMICO, Mgodi wa almasi mwadui, madini chini ya ardhi (dhahabu na mengineyo), Makaa ya mawe, TANESCO, gesi chini ya ardhi na mafuta, Vyuo mbalimbali, secondary schools, primary schools, majeshi na vyuo vyake, viwanja vya ndege (Dar na KIA na kila mkoa), Hoteli za kitalii kila mkoa na kwenye hifadhi za taifa, hifadhi za taifa na maeneo yake na mengi mengineyobila kusahau Muungano wa Zbr na Tngk na Kuondoa ukabila.

Leo hii miaka 27 toka ang'atuke tumepata maraisi wa 3 kwa kila mmoja miaka 10. Swali ni je katika machache yaliyotajwa hapo juu ni yapi tumeboresha ama kuyasimamia wenyewe na kuyadumisha yakaendelea kuwepo ama kuwaletea watanzania maendeleo?

Wakati ukiwa unchangia kwa ulinganifu na umakini mchango wako uzingatie na ukumbuke yafuatayo: -

1. Mwalimu alitawala kwa miaka 24 tu. kuanzia 1961 mpaka 1985 ukilinganisha na miaka 27 ya viongozi waliyofuata badaye kwa awamu 3 tofauti.

2. Mwalimu alikuwa akitawala nchi katika mfumo wa kisiasa wa ujamaa na kujitegemea ambapo mifumo yote ya uzalishaji mali ilikuwa chini ya dola.

3. Wakati wa utawala wa mwalimu, nchi ilikumbana na majanga makuu mawili kiuchumi na kijamii yaani vita vya kagera na TZ ( 1978 - 1980) na kuvunjika kwa jumuia ya africa mashariki ambapo mali katika jumuia hiyo zilichangiwa na wanachama wote (TZ, Kny na Ug) na mali hizo 70% yake zikachukuliwa na Kenya mwaka (1977). Hii maana yake ni kuwa, miaka 5 katika utawala wake haikuwa ya kujenga uchumi hata kidogo (yaani toka 1977 hadi 1981).

Nawakilisha kwa kupokea maoni yenu wadau.
 
Sasa kipi cha maana hapo?

Muulize Nyerere, alifanywa nini na Tiny Rowlands wa LONRHO. Kama hujui uliza waliokuwepo siku hizo.
 
Tukumbuke pia kwamba ni Mwalimu huyo huyo aliyenena miaka takribani 20 hivi iliyopita kwamba chama makini cha upinzani kitatokana na CCM no actualy "nyinyiemu" na chama alichokiona kina mwelekeo huo wakati huo alinena ni CHADEMA, now that prophesy has come true for everyone to see. Mwalimu was agreat philosopher and thinker. Kwa kweli kama watawala wetu hawa magamba wangemuenzi na kujifunza na kutenda kama maono yake yalivyokuwa Tanzania ingekuwa inapaa katika kila nyanja ya maisha. Asante Mungu kwa maisha ya Baba wa Taifa. RIP Mwalimu
Hii ni kweli kabisa ndio mañana viongozi wa CCM wanachomwa na hotuba zake nyingi sana hasa alipozungumzia swala la rushwa.
 
Unazungumzia nyerere huyu aliendesha utawala wake kibabe asie penda kukosolewa na kujifanya mungu mtu kama kuna fisadi wa mwanzo tz ni nyerere ndie aliendesha nchi kidikteta hana lolote ni adui namba moja wa uchumi wa tz kimoja tu mungu alimpa alijua kuzungumza na watu ila vitendo ziro
 
Mkuu Jamani mbona si poa hili nalo neno.

Bado tunajadili hili la mwalimu! ila kwa ufupi kikao chetu kimesha kwama kwani mwalimu alikuwa ni wa pekee kabisa katika tasnia ya utawala wa nchi yetu. Na wakati anaondoka madarakani alisema wazi kwamba

"Ni muda mrefu sasa nimekuwa napenda nipumzike kuuongoza nchi yetu ili kuwapisha wa tz wengine wenye uwezo nao wachangie kuleta maendeleo ya nchi yetu. Lakini baadhi yenu mmekuwa mkipinga mimi kung'atuka katika nafasi hii ya uongozi wa nchi kwa sababu zenu mnzozijua ikiwemo maslahi binafsi."

Mzee akang'atuka akaenda zake kijijini kwao butiama kwenda kulima. Akawaachia viwanda (vya nguo, bia, sigara, viatu, korosho, nguo, kuchambua pamba, tumbaku, mkonge, kahawa, chai, almasi n.k), reli na treni zake, ndege za ATC, mashamba ya kahawa, pamba, mkonge, chai, misitu, ardhi, meli, mabenki (Nbc & Crdb, TIB), NHC, PPF, NIC, NSSF, bodi za mazao yote ya biashara, NMC, NDC, STAMICO, Mgodi wa almasi mwadui, madini chini ya ardhi (dhahabu na mengineyo), Makaa ya mawe, TANESCO, gesi chini ya ardhi na mafuta, Vyuo mbalimbali, secondary schools, primary schools, majeshi na vyuo vyake, viwanja vya ndege (Dar na KIA na kila mkoa), Hoteli za kitalii kila mkoa na kwenye hifadhi za taifa, hifadhi za taifa na maeneo yake na mengi mengineyobila kusahau Muungano wa Zbr na Tngk na Kuondoa ukabila.

Leo hii miaka 27 toka ang'atuke tumepata maraisi wa 3 kwa kila mmoja miaka 10. Swali ni je katika machache yaliyotajwa hapo juu ni yapi tumeboresha ama kuyasimamia wenyewe na kuyadumisha yakaendelea kuwepo ama kuwaletea watanzania maendeleo?

Wakati ukiwa unchangia kwa ulinganifu na umakini mchango wako uzingatie na ukumbuke yafuatayo: -

1. Mwalimu alitawala kwa miaka 24 tu. kuanzia 1961 mpaka 1985 ukilinganisha na miaka 27 ya viongozi waliyofuata badaye kwa awamu 3 tofauti.

2. Mwalimu alikuwa akitawala nchi katika mfumo wa kisiasa wa ujamaa na kujitegemea ambapo mifumo yote ya uzalishaji mali ilikuwa chini ya dola.

3. Wakati wa utawala wa mwalimu, nchi ilikumbana na majanga makuu mawili kiuchumi na kijamii yaani vita vya kagera na TZ ( 1978 - 1980) na kuvunjika kwa jumuia ya africa mashariki ambapo mali katika jumuia hiyo zilichangiwa na wanachama wote (TZ, Kny na Ug) na mali hizo 70% yake zikachukuliwa na Kenya mwaka (1977). Hii maana yake ni kuwa, miaka 5 katika utawala wake haikuwa ya kujenga uchumi hata kidogo (yaani toka 1977 hadi 1981).

Nawakilisha kwa kupokea maoni yenu wadau.
 
Last edited by a moderator:
M4C sasa kuibadilisha nchi kwa nguvu ya umma. Yaushirikisha umma wa watanzania katika kujiletea mabadiliko ya mapinduzi ya amani.
 
Back
Top Bottom