MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Asikudanganye Mtu popote pale ulipo kuwa kauli za Watu waliokufa namaanisha Marehemu wakizisema huwa hazitimii. Ni kwamba huwa hawatanii kabisa na wayasemayo hutokea na hutimia.
Mwaka jana nilihudhuria Msiba Mmoja ambapo kumbe Marehemu wakati anakata Roho alisema akifa azikwe Dar es Salaam na Ndugu wakampuuza wakamsafirisha wanafika tu Segera wakapata Ajali na wale wale waliolazimisha asafirishwe Wakafa na Msafara ukageuka na kuja Kuzikwa Dar kama ambavyo Marehemu aliagiza.
Mwaka huu Mwezi February kuna Marehemu alisema akifa tu asizikwe Dar es Salaam na akazikwe Kijiini Kwao na Ndugu walipolazimisha Kumzikia Dar es Salaam kwa Kigezo cha Kuokoa Gharama Jeneza lake liligoma Kubebeka ila baada ya muda tu Ndugu walipokubaliana asafirishwe kama alivyoagiza Jeneza lilikuwa jepesi mno Kubebeka na akasafirishwa Kijiini Kwake kwa Maziko.
Leo hii kwa wale Wakazi wa Chang'ombe Temeke nadhani Ajali mbaya iliyotokea Mataa na kusababisha Vifo na Majeruhi mmeisikia.
Ni kwamba Marehemu ambaye ndiyo alikuwa anasafirishwa kwenda Kuzikwa kabla ya kufa kwa Hasira alisema kuna Watu Wawili katika Familia yake akifa hataki waende Kumzika kwani wakati anaumwa na Kalazwa Hospitali walishindwa kwenda Kumuona huku uwezo huo wakiwa nao isipokuwa Dharau na Kupuuza kuliwatawala.
Na katika Ajali hi ya leo ambayo ilikuwa na Msafara wa Gari kadhaa Gari ambayo imegongwa na Kuharibika vibaya ni ya Watu wale wale Walengwa Wawili ambapo wote Wamefariki huku Mmoja Viganja vyake vikikatika.
Hivyo basi baada ya Msiba huu kutokea Msafara wa kumsafirisha Marehemu umeendelea na wale Watu aliowakataa wasimzike nao Wamefariki hivyo Maiti zao zipo Mochwari kwa sasa ukisubiri Msafara ulio Safarini ukirejea ndiyo waanze Kuhangaika nao na Wawazike.
Hata hivyo kuna Mbinu moja nilipewa na Wabobezi wa Kusafirisha Maiti / Marehemu wenye Masharti magumu hasa ya Kusafirishwa kuwa mkianza tu Safari tafuta Jiwe Kubwa / Jiwe Dogo liweke juu ya Jeneza na Marehemu / Mwili hautowasumbueni hadi mnafika. Bado sijaiamini ila kama hapa JamiiForums kuna wenye kuijua zaidi watufafanulie tafadhali.
Jamani tujitahidi mno na sana Kuziheshimu Kauli za mwisho mwisho za Marehemu kwani nimeamini kuwa kwa 85% huwa zinatimia japo kwa 15% zinaweza zisitimie vile vile kama ilivyo kwa Chanjo ya UVIKO-19 ambapo kwa 15% inaweza isikusaidie na ikakuathiri ila kwa 85% huwa inasaidia Kukukinga.
Mwaka jana nilihudhuria Msiba Mmoja ambapo kumbe Marehemu wakati anakata Roho alisema akifa azikwe Dar es Salaam na Ndugu wakampuuza wakamsafirisha wanafika tu Segera wakapata Ajali na wale wale waliolazimisha asafirishwe Wakafa na Msafara ukageuka na kuja Kuzikwa Dar kama ambavyo Marehemu aliagiza.
Mwaka huu Mwezi February kuna Marehemu alisema akifa tu asizikwe Dar es Salaam na akazikwe Kijiini Kwao na Ndugu walipolazimisha Kumzikia Dar es Salaam kwa Kigezo cha Kuokoa Gharama Jeneza lake liligoma Kubebeka ila baada ya muda tu Ndugu walipokubaliana asafirishwe kama alivyoagiza Jeneza lilikuwa jepesi mno Kubebeka na akasafirishwa Kijiini Kwake kwa Maziko.
Leo hii kwa wale Wakazi wa Chang'ombe Temeke nadhani Ajali mbaya iliyotokea Mataa na kusababisha Vifo na Majeruhi mmeisikia.
Ni kwamba Marehemu ambaye ndiyo alikuwa anasafirishwa kwenda Kuzikwa kabla ya kufa kwa Hasira alisema kuna Watu Wawili katika Familia yake akifa hataki waende Kumzika kwani wakati anaumwa na Kalazwa Hospitali walishindwa kwenda Kumuona huku uwezo huo wakiwa nao isipokuwa Dharau na Kupuuza kuliwatawala.
Na katika Ajali hi ya leo ambayo ilikuwa na Msafara wa Gari kadhaa Gari ambayo imegongwa na Kuharibika vibaya ni ya Watu wale wale Walengwa Wawili ambapo wote Wamefariki huku Mmoja Viganja vyake vikikatika.
Hivyo basi baada ya Msiba huu kutokea Msafara wa kumsafirisha Marehemu umeendelea na wale Watu aliowakataa wasimzike nao Wamefariki hivyo Maiti zao zipo Mochwari kwa sasa ukisubiri Msafara ulio Safarini ukirejea ndiyo waanze Kuhangaika nao na Wawazike.
Hata hivyo kuna Mbinu moja nilipewa na Wabobezi wa Kusafirisha Maiti / Marehemu wenye Masharti magumu hasa ya Kusafirishwa kuwa mkianza tu Safari tafuta Jiwe Kubwa / Jiwe Dogo liweke juu ya Jeneza na Marehemu / Mwili hautowasumbueni hadi mnafika. Bado sijaiamini ila kama hapa JamiiForums kuna wenye kuijua zaidi watufafanulie tafadhali.
Jamani tujitahidi mno na sana Kuziheshimu Kauli za mwisho mwisho za Marehemu kwani nimeamini kuwa kwa 85% huwa zinatimia japo kwa 15% zinaweza zisitimie vile vile kama ilivyo kwa Chanjo ya UVIKO-19 ambapo kwa 15% inaweza isikusaidie na ikakuathiri ila kwa 85% huwa inasaidia Kukukinga.