Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Nimeamini kwamba Nassary alipoeleza kuwa aliwasiliana na Spika kuhusu taarifa zake kuwa nje ya Bunge alikuwa sahihi, nimeamini alipomtaja Mhe.Ndugai kuwa wakati wa harusi yake alisimama Kama baba na hakutegemea kuwa ataweza kutoa maamuzi bila hata kumpa muda wa kujieleza alikuwa sahihi.
Ofisi ya Spika imekuwa Kama ofisi za wakurugenzi ambazo wagombea wakirejesha fomu wanafunga ofisi na kuingia mitini wasipokee fomu zao. Ofisi ya Spika haipo kwa ajili ya kulisaidia Bunge kufanya kazi na wabunge Kama timu Bali ipo kwa ajili ya kutekeleza matakwa ya chama.
Wakati wa Nassary tuliambiwa hakutoa taarifa alipo na hivyo kwa muda aliokuwa amekaa nje ya Bunge alifukuzwa, hawakuangalia mke wa Nassary kuwa alipita matatizo gani bali aliuangalia ubunge wake kwamba utarudije ccm? Leo Jimbo lipo ccm, Ni kipi kimebadilika huko Arumeru? Miujiza gani imefanyika kwa zaidi ya miezi mitatu ya Mbunge mpya?
Leo hata Lisu ambaye alipigwa risasi akitoka bungeni na kila mtu anajua spika anasema Hana taarifa alipo, je mtu Kama Huyu ndo tulimtegemea apokee barua ya Nassary?
Lakini tujiulize, hivi kuwa na wabunge wa ccm kila Kona ndo nchi inaendelea? Wingi wao bungeni umeisaidiaje nchi?
Naamini Nassary alichoeleza ni kile tu alichotendewa tukakiona adharani lakini upo uwezekano alifanyiwa mengine ambayo wenye uchu wa madaraka na ubunge walitamani aondoke Duniani awaache wawe wabunge. Na watu hao hao yawezekana wanatamani na mrithi wa Nassary aondoke aje mwingine kwa sababu madaraka ya ila siku zote umweka matatizoni mtawala.
Nimpongeze kijana Nassary, kazi yake inajulikana nje na ndani ya bunge...ni mpe pole lisu nikimtaka atambue kwamba anayopitia yanapangwa na wale wanaoamini wao tu ndio wanafaa kuiongoza nchi na wengine. wanaamini kuua ili waongoze lakini nao watauwawa na wanaopenda waongoze.
Ofisi ya Spika imekuwa Kama ofisi za wakurugenzi ambazo wagombea wakirejesha fomu wanafunga ofisi na kuingia mitini wasipokee fomu zao. Ofisi ya Spika haipo kwa ajili ya kulisaidia Bunge kufanya kazi na wabunge Kama timu Bali ipo kwa ajili ya kutekeleza matakwa ya chama.
Wakati wa Nassary tuliambiwa hakutoa taarifa alipo na hivyo kwa muda aliokuwa amekaa nje ya Bunge alifukuzwa, hawakuangalia mke wa Nassary kuwa alipita matatizo gani bali aliuangalia ubunge wake kwamba utarudije ccm? Leo Jimbo lipo ccm, Ni kipi kimebadilika huko Arumeru? Miujiza gani imefanyika kwa zaidi ya miezi mitatu ya Mbunge mpya?
Leo hata Lisu ambaye alipigwa risasi akitoka bungeni na kila mtu anajua spika anasema Hana taarifa alipo, je mtu Kama Huyu ndo tulimtegemea apokee barua ya Nassary?
Lakini tujiulize, hivi kuwa na wabunge wa ccm kila Kona ndo nchi inaendelea? Wingi wao bungeni umeisaidiaje nchi?
Naamini Nassary alichoeleza ni kile tu alichotendewa tukakiona adharani lakini upo uwezekano alifanyiwa mengine ambayo wenye uchu wa madaraka na ubunge walitamani aondoke Duniani awaache wawe wabunge. Na watu hao hao yawezekana wanatamani na mrithi wa Nassary aondoke aje mwingine kwa sababu madaraka ya ila siku zote umweka matatizoni mtawala.
Nimpongeze kijana Nassary, kazi yake inajulikana nje na ndani ya bunge...ni mpe pole lisu nikimtaka atambue kwamba anayopitia yanapangwa na wale wanaoamini wao tu ndio wanafaa kuiongoza nchi na wengine. wanaamini kuua ili waongoze lakini nao watauwawa na wanaopenda waongoze.