King_Villa
JF-Expert Member
- Feb 6, 2012
- 574
- 378
Wakuu heshima kwenu.
Katika harakati za kimaisha nilipata kaeneo maeneo ya CHANIKA sehemu inaitwa ZINGIZIWA .
Nilipelekwa mara ya kwanza na nikaoneshwa kuwa eeneo liko safi kabisa na ni eneo kubwa linaonesha vyanzo vya maji vipo karibu. Pia linafikika kirahisi na nikaenda kwenye mamlaka ya kiserikari nikaoneshwa Ramani kuwa haliko kwenye mipango ya serikari.
Na mtu aliyenitaftia hapo alinihakikishia hilo ila ilinibidi nichunguze mimi kama mimi.
Baada ya kuona eneo liko safi nikaanza mchakato wa malipo kwa kufuata sheria zote.
Sasa juzi nilipo kwenda kulitembelea nikamwona mtu mwenye asili ya pwani (mzaramo, mmakonde) akinifuata na kuniomba aongee na mimi kidogo. Basi bila hiana nikamruhusu.
Alinipa historia ndefu juu ya hilo eneo nikisema niandike ntawachosha. Ila kwa ufupi tu alisema hilo ni eneo ambalo lina wenyewe ati sio langu pamoja na kwamba nalimiliki watakuja kunitfuta siku moja.
Na alidai kuna watu wanakuja maeneo ya jirani kila mwaka kucheza maeneo hayo.
Na kila mwaka hapo tunaokota maiti moja mwisho wa mwaka huwa haijulikani kwanini inakuwa eneo lile na hata wakiitoa hiyo maiti huwa inarudi hapo mpaka baada ya siku saba inapotea yenyewe .Na aliniambia kuwa kama mi ni mzito basi nikae ama la niondoke tu.
Sasa inaonekana pana nguvu za giza pale mahali
.ipi njia bora ya kuepuka hilo tatizo...?
Nafikiria au yule jamaa ananidanganya ni uoga wake tu mbona kwa pembeni kuna watu wanaishi vizuri tu.?
Kwasababu eneo ni zuri sana hasa kwa watoto wangu miaka ijayo.
Au na mimi niliuze kwa mtu mwingine...
Yani nafikiria mengi hadi nakosa usingizi na pesa nimeshatoa kubwa tu.
Kuna mliokutana na shida hii mlifanyaje?
Katika harakati za kimaisha nilipata kaeneo maeneo ya CHANIKA sehemu inaitwa ZINGIZIWA .
Nilipelekwa mara ya kwanza na nikaoneshwa kuwa eeneo liko safi kabisa na ni eneo kubwa linaonesha vyanzo vya maji vipo karibu. Pia linafikika kirahisi na nikaenda kwenye mamlaka ya kiserikari nikaoneshwa Ramani kuwa haliko kwenye mipango ya serikari.
Na mtu aliyenitaftia hapo alinihakikishia hilo ila ilinibidi nichunguze mimi kama mimi.
Baada ya kuona eneo liko safi nikaanza mchakato wa malipo kwa kufuata sheria zote.
Sasa juzi nilipo kwenda kulitembelea nikamwona mtu mwenye asili ya pwani (mzaramo, mmakonde) akinifuata na kuniomba aongee na mimi kidogo. Basi bila hiana nikamruhusu.
Alinipa historia ndefu juu ya hilo eneo nikisema niandike ntawachosha. Ila kwa ufupi tu alisema hilo ni eneo ambalo lina wenyewe ati sio langu pamoja na kwamba nalimiliki watakuja kunitfuta siku moja.
Na alidai kuna watu wanakuja maeneo ya jirani kila mwaka kucheza maeneo hayo.
Na kila mwaka hapo tunaokota maiti moja mwisho wa mwaka huwa haijulikani kwanini inakuwa eneo lile na hata wakiitoa hiyo maiti huwa inarudi hapo mpaka baada ya siku saba inapotea yenyewe .Na aliniambia kuwa kama mi ni mzito basi nikae ama la niondoke tu.
Sasa inaonekana pana nguvu za giza pale mahali
.ipi njia bora ya kuepuka hilo tatizo...?
Nafikiria au yule jamaa ananidanganya ni uoga wake tu mbona kwa pembeni kuna watu wanaishi vizuri tu.?
Kwasababu eneo ni zuri sana hasa kwa watoto wangu miaka ijayo.
Au na mimi niliuze kwa mtu mwingine...
Yani nafikiria mengi hadi nakosa usingizi na pesa nimeshatoa kubwa tu.
Kuna mliokutana na shida hii mlifanyaje?