nimeachwa njia panda..........

matumbo

JF-Expert Member
Jul 9, 2011
7,225
3,944
Leo nimeenda kumtembelea rafiki yangu mchana huu nyumbani kwao,tumepiga stori sana.basi chakula cha mchana kilipotengwa mezani ghafla akaniomba nimsindikize dukani nami nikamkubalia,ila tumefika dukani ananiambia nimsubiri amesahau pesa nyumbani...sasa ni mda kidogo tangu aniache hapa..naomba msaada ndugu zangu hii inamaanisha nini?
 
ha ha ha...pole lakini siku hizi chakula kwa budget sa we umeenda bila taarifa ameshindwa kukwambia kwa mdomo so ametumia vitendo.
 
Ameangalia mdomo wako akajua utamaliza chakula fasta.
Pole sana.
OTIS.
 
ha ha ha...pole lakini siku hizi chakula kwa budget sa we umeenda bila taarifa ameshindwa kukwambia kwa mdomo so ametumia vitendo.


lakini utamaduni wetu si kushirikiana ata kwenye chakula jaman
 
Leo nimeenda kumtembelea rafiki yangu mchana huu nyumbani kwao,tumepiga stori sana.basi chakula cha mchana kilipotengwa mezani ghafla akaniomba nimsindikize dukani nami nikamkubalia,ila tumefika dukani ananiambia nimsubiri amesahau pesa nyumbani...sasa ni mda kidogo tangu aniache hapa..naomba msaada ndugu zangu hii inamaanisha nini?
Mfumuko wa bei ndugu yangu, hata hivyo amekuheshimu sana, angeweza kukupa live
 
Leo nimeenda kumtembelea rafiki yangu mchana huu nyumbani kwao,tumepiga stori sana.basi chakula cha mchana kilipotengwa mezani ghafla akaniomba nimsindikize dukani nami nikamkubalia,ila tumefika dukani ananiambia nimsubiri amesahau pesa nyumbani...sasa ni mda kidogo tangu aniache hapa..naomba msaada ndugu zangu hii inamaanisha nini?

Ukome kutembelea watu bila taarifa,tena ingekua mimi ndio huyo rafiki ningekuchana live..
 
Tatizo kwa muonekano wa nje unaonekana wapakia sana.
Housing imekuponza.
OTIS.


usiogope ukubwa wa samaki uliza bei..housing isiwatishe waungwana tuwe tunakalibisha ata siku moja moja kwenye minuso
 
kakuacha njia panda?pole kwa kudoea msosi...ulizia watu njia ya kwenda kwenu teh teh teh..people dont like spongers now adays
 


Ukome kutembelea watu bila taarifa,tena ingekua mimi ndio huyo rafiki ningekuchana live..


sasa bora ningepewa live nijue moja,ila hii ya kutelekezwa dukan na swaiba imenistua kidogo..
 
Tatizo lako huwa unakaba mpaka mwisho, unatakiwa unakula tonge mbili kisha unasema ilikuwa suna tu. Tumbo lako kubwa kumbe unategemea kula kwa jirani!
 
Wakati nilipoanza maisha nilikuwa nakaa kwenye chumba kimoja na nilikuwa na jirani yangu ambaye kila anaposikia jiko langu la stove linazima yeye aliingia chumbani kwangu na kuketi mezani na kula nami. Nilishindwa kumvumilia na nikaamua nitumie njia nyingine. Siku moja baada ya kumaliza kupika, sikuzima jiko bali nilikula mpaka nikamaliza chakula. Baada ya hapo nikazima jiko na yeye akaingia akakuta mimi naosha vyombo. Sasa hiyo huenda ina maanisha kwa upande mwingine kuwa wewe si mstaarabu unatabia za kama yule aliyekuwa akisubiri jiko kuzimwa. Badilisha mwenendo wako kama uko hivyo otherwise jamaa anatabia ya uchoyo.
 
Wakati nilipoanza maisha nilikuwa nakaa kwenye chumba kimoja na nilikuwa na jirani yangu ambaye kila anaposikia jiko langu la stove linazima yeye aliingia chumbani kwangu na kuketi mezani na kula nami. Nilishindwa kumvumilia na nikaamua nitumie njia nyingine. Siku moja baada ya kumaliza kupika, sikuzima jiko bali nilikula mpaka nikamaliza chakula. Baada ya hapo nikazima jiko na yeye akaingia akakuta mimi naosha vyombo. Sasa hiyo huenda ina maanisha kwa upande mwingine kuwa wewe si mstaarabu unatabia za kama yule aliyekuwa akisubiri jiko kuzimwa. Badilisha mwenendo wako kama uko hivyo otherwise jamaa anatabia ya uchoyo.


kumbe tupo wengi tuliokumbwa na hii dhahama
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom