Nimeachwa na mpenzi wangu, nifanye nini niimudu hali hii?

Mshikaji ngoja nikuambie, wengi wetu tunapita njia hiyo hiyo na kwakweli inauma sana, wewe weka ujasiri wa kuacha kumtafuta jiwekee time frame ya siku 90, ni tabia ya mapenzi huwa yako moto sana ndani ya siku hizo kwa wapenzi wapya, usimtafute ingawa utakuwa na emotions nyingi sana jikaze tuuuu. Ikipita hizo siku na ukaweza kuwa kimya utakuja niambia kama hili unalolipitia wewe halitakuwa upande wake!!!!!! we vumilia otherwise kama hatokutafuta then just forget and proceed!!!!
 
Habari wana JF

Hapa nimebakia njia panda muda huu leo baada ya kumpigia mpenzi wangu simu! Ambaye tulipendana saaana, siku za nyuma hapo tulikosana lakini tukapatana tena maisha yakasonga leo hii nimempigia simu ananijibu majibu ya mkato sana. Nikituma sms anajibu kwa mikato nikimuulza shida nini? Anasema hakuna mpaka nilipo mbona saaana akatamuka tu neno moja " naomba uniache " Nikamuulza kivipi anasema tuu nimuache hanipendi.

Tena nashindwa kumwelewa shida nini! Hapa nilipo na hasira natamani hata nikamuue lakini siwezi! Na kumuacha nashindwaaa kabisa naombeni ushauri nifanyeje katika hili?
we jamaa umenichekesha sanaunatamani ukamuue.ila unampenda
 
ulivyoandika tu nataka nikamuue nimejua na wewe mana ndo maneno yako.we kaka mbinafsi sana nilivyojitoa kwako kwa moyo wote unajua ulichofanya.lazima uwe na hasira sababu we ndo mnufaika wa mahusiano what did i get from you zaidi ya kutufolenisha
 
Da
ulivyoandika tu nataka nikamuue nimejua na wewe mana ndo maneno yako.we kaka mbinafsi sana nilivyojitoa kwako kwa moyo wote unajua ulichofanya.lazima uwe na hasira sababu we ndo mnufaika wa mahusiano what did i get from you zaidi ya kutufolenisha
Da ndo wewe unaeongelewa apo au mimi ndo sielewi???
 
Jishibishe na subra na uamini kuwa ni swala la Muda tu...Yupo Mungu wetu anakuona anakuskia atakupa ataekupenda kwa dhati.
 
Ww ni wakiume au wakike , tafuta ile nyimbo ya marioo bia tamu utanishukuru baadae
 
Ukishindwa kabisa kumsahau nicheck pm mkuu,mwanaume huwezi achwa kirahisi hivyo.
 
Huu ni msimu wa kuachana kwa hiyo kubaliana na hali tu kuwa umeingia msimu mwingine. Kama ilivyo kutoka kifuku kuja masika ....Sasa wewe kubali kuwa tumehama msimu ukitaka kililia msimu ulio pita trust me itakula kwako....

Na kwa Sasa kutakua na nyuzi nyingi tu za kupigwa vhini
 
Huu ni msimu wa kuachana kwa hiyo kubaliana na hali tu kuwa umeingia msimu mwingine. Kama ilivyo kutoka kifuku kuja masika ....Sasa wewe kubali kuwa tumehama msimu ukitaka kililia msimu ulio pita trust me itakula kwako....

Na kwa Sasa kutakua na nyuzi nyingi tu za kupigwa vhini
Hata mimi siku ya nne,nimepgwa chini niliandik uzi wangu wa kuachwa uko
 
Back
Top Bottom