Nime mcheat Mke wangu akagundua naye akalipiza kuwa sasa tupo ngoma draw...tuanze upya

GuDume

JF-Expert Member
Jan 18, 2015
6,652
14,247
Asubuh imeanza kwa ngurumo na mvua za hapa na pale. Hali ya hewa ni ya uvuguvugu anga linaonekana kuwa na mawazo sana.maana halijielew kama liruhusu mvua inyeshe au jua liwake.basi ili mradi ni mkanganyiko kila sehemu.huyu na lake na yule ana lake pia.

Koboko (si jina lake halisi) namfaham kwa muda kidogo nipo naye kazini mwaka wa tatu huu. Week hii nzima amekuwa kama mtu mwenye jambo linalomvurugia utulivu wake awapo ofisini. Mi namfaham kama mmoja ya watu makini linapokuja suala la uchapaji kaz.

Lakini katika week hii nzima inayoelekea ukingoni amekuwa kama kuku anayetaka kutaka.hatulii na wakati mwingine anakuwepo kimwili ila kimawazo mbali sana nasi ofisin. Moja ya shughuli zangu ni kuongea na wafanyakazi mambo yao binafs yanayoathiri utendaj kazi zao.nikamwita ofisini jana tuongee.

Wanaume hufikia kipindi tukafunguka maana kitulacho mara nyingi ni kukumbatia hisia kwa ndani na kuzifungia huko.nazo huwa mara nying haziwez tulia na ndo kisa cha yeye kutokuwa na utulivu.

Kifupi Koboko... Alimgonga demu mmoja huko kitaa. Mkewe akajua hilo pasi na shaka kabisa. Alilishuhudia hilo jambo kwenye 3D halafi HD. So halikuwa na ubishi at all. Basi wakarudi home Koboko anasema hakusema kitu.

Jumamosi iliyopita Koboko alipata ushahidi naye yeye wa picha ambazo mkewe alipigwa na jamaa yake then akamrushia akiwa ametoka kugegeswa wamelala kitandani hoi.na texts nazo zikawa zinajielezea wakisimuliana ilivyokuwa.

Koboko akafura kwa hasira na kutetemeka kana kwamba ameshika umeme grid ya Taifa. Akatoa macho na kumuita mkewe chumbani kumwonesha ushenzi alioufanya.mke akashtuka na baada ya majibizano kadhaa akasema ni kweli alicheat kama ambavyo Koboko naye alovyofanya. Ila sasa waape kuwa wataanza upya kwa kuwa wote ni wakosaji.

Koboko anasema anashindwa aamue nini maana na mkewe ana ushahidi wa jinsi ambavyo ali cheat na dada mmoja migebuka ( mwanamke anayemendea waume za watu) sasa hajielew maana anasema hana hamu tena ya kuwa ana m secrew mkewe na hali hiyo imemuuma sana.

Hii dunia hii "UKISHANGAA YA MUSSA UTAYAONA YA FIRAUNI"
 
Back
Top Bottom