Nilizaa nae mtoto tukaachana, kaolewa kakosa mtoto, eti nimsaidie apate mtoto

Massa

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
647
794
Habari za jioni wapendwa,

Kuna inshu inanitatiza kuhusu mzazi mwenzangu.

Ni kwamba nilizaa nae mtoto miaka 13 iliyopita alafu tukaachana baada ya yeye na familia yake kudai hawezi kuwa na mimi maana kwetu na mimi mwenyewe masikini choka mbaya. Na kweli tulikua choka mbaya baada ya mzee kutumbuliwa enzi za Nyerere.

Sasa tatizo lake ni kwamba kizazi kwake kimekataa kabisa yaani tokea alipo achana na mimi baada ya miaka mitano akaolewa mpaka leo hajapata mimba.

Anasema wameenda hospitali na wote wako poa yeye na mmewe. Sasa amekuja kwangu nipo na mke wangu na watoto wawili + mwanae na mwingine yupo njiani ananiambia nimsahidie ili apate mtoto nae labda kuna kitu nilifanya na anasema labda kutokana na tulivyoachana kwa masimango labda nilifanya chochote kibaya.

Ingawa ukweli sikufanya lolote baya kwake na wala sina hata wazo hilo.

Ndugu zangu naomba ushauri hivi sasa yupo kwangu siku ya tatu leo yeye na mme wake ingawa mme yuko kwa ndugu yake sio mbali na kwangu.

Yaani mke analala kwetu mme analala kwa ndugu zake
 
Daaaah kweli wakati wa shida hata utu wako una utupa.kweli mume nae kamruhusu kabsa?
Na mkeo anasemaje?
Mungu akupe hekima ndugu. Binafsi nakushauri uzungumze na mkeo kwanza, akiridhia mpe mtoto aende nae akawape faraja.
Mungu awape amani hao watu mwee huruma
 
Daaaah kweli wakati wa shida hata utu wako una utupa.kweli mume nae kamruhusu kabsa?
Na mkeo anasemaje?
Mungu akupe hekima ndugu. Binafsi nakushauri uzungumze na mkeo kwanza, akiridhia mpe mtoto aende nae akawape faraja.
Mungu awape amani hao watu mwee huruma

Duuhh suala la kumpa mtoto tuliyezaa wote haiwezekani kwanza mke wangu hatokubali niliangaika sana na huyu Binti yangu walinisusia akiwa na miezi 11 nimelea hadi alipofikia kwa msahada wa mke wangu mpenzi. Leo hii siwezi kabisa kumwachia. Na kuhusu mke wangu naona wanaelewana vizuri tu kaja na gear ya kumtembelea mtoto hivyo mke wangu anatimiza wajibu kwa mgeni tu
 
Aisee walimwengu wanavituko wamekuja kwako kukuomba uzae na mkewe....we zaidi ya dume la mbegu

Blaki Womani mimi sio dume la mbegu nazani labda alitaka kujua tu labda nilimwendea kwa mshana Jr baada ya kuachana. Nazani anaogopa kuzaa na mimi maana Binti yake ni copy yangu kweli kweli hivyo itakua aibu kwa kweli akisema azae na mimi tena ingawa mimi mwenyewe siwezi kukubali kwa kweli
 
Usiombe kitu km hiki kikutokee. Niliwahi pia kuchumbia mahali afu yule dem akanitosa kwa sababu enzi hizo yeye pamoja na wazazi wake waliona mi sina hela wala lile. Nilikubaliana na maoni yao ingawa niliumia sana moyoni, coz nilimpenda sana. Yule dada akaolewa na jamaa mwingine sasa kila akishika mimba inatoka. Mpaka ikafika mimba 6, zote chini, wakahisi mi nimemfanyia yule dada uchawi ili asizae, hilo nalo likaniumiza tena. Wao wakapata wazo la kumwona dr wa kinamama, wakashauriwa mimba itakaposhika warudi Hosp ili wapate tiba ya tatizo hilo. Iliposhika wakarudi wakatibiwa tatizo likaisha. Akajifungua vizuri. Baada miaka 2 akanasa mimba tena akajifungua vizuri... Mtoto alipokua siku moja huyo dada akanitafuta akaniomba msamaha, tuliposameheana km vile anatania akaniomba ili yaishe kabisa naomba tuzae na wewe. Nilimkatalia kiaina nilipoona anakazia zaidi ikabidi nimkubalie nikazaa nae mtoto wa kike akaniambia "sasa nimefuta laana yako kwangu". Tukakubaliana tuvunje uhusiano kwa amani.
 
Duuhh suala la kumpa mtoto tuliyezaa wote haiwezekani kwanza mke wangu hatokubali niliangaika sana na huyu Binti yangu walinisusia akiwa na miezi 11 nimelea hadi alipofikia kwa msahada wa mke wangu mpenzi. Leo hii siwezi kabisa kumwachia. Na kuhusu mke wangu naona wanaelewana vizuri tu kaja na gear ya kumtembelea mtoto hivyo mke wangu anatimiza wajibu kwa mgeni tu
Mkeo ana moyo mzuri sana, Mungu ambariki..daaah ndo maana nimesema Mungu akupe hekima jinsi ya kumsaidia mzazi mwenzio.
 
Usiombe kitu km hiki kikutokee. Niliwahi pia kuchumbia mahali afu yule dem akanitosa kwa sababu enzi hizo yeye pamoja na wazazi wake waliona mi sina hela wala lile. Nilikubaliana na maoni yao ingawa niliumia sana moyoni, coz nilimpenda sana. Yule dada akaolewa na jamaa mwingine sasa kila akishika mimba inatoka. Mpaka ikafika mimba 6, zote chini, wakahisi mi nimemfanyia yule dada uchawi ili asizae, hilo nalo likaniumiza tena. Wao wakapata wazo la kumwona dr wa kinamama, wakashauriwa mimba itakaposhika warudi Hosp ili wapate tiba ya tatizo hilo. Iliposhika wakarudi wakatibiwa tatizo likaisha. Akajifungua vizuri. Baada miaka 2 akanasa mimba tena akajifungua vizuri... Mtoto alipokua siku moja huyo dada akanitafuta akaniomba msamaha, tuliposameheana km vile anatania akaniomba ili yaishe kabisa naomba tuzae na wewe. Nilimkatalia kiaina nilipoona anakazia zaidi ikabidi nimkubalie nikazaa nae mtoto wa kike akaniambia "sasa nimefuta laana yako kwangu". Tukakubaliana tuvunje uhusiano kwa amani.
Haya mambo ya uzazi yanafanya uwe na imani ambazo nahisi hadi shetani hua anakataa kwa Mungu kua yy hapo hausiki
 
Mkeo yupo vizuri sana mpaka kumruhusu kukaa nanyi Leo siku ya Tatu.. Waambie wakasali sana na kuwa na subira Muda ukifika watapata wa kutosha.
 
Achana nae mzushi huyo! kama alimtelekeza mtoto wa miezi 11 ni kama muuaji! mwambie atembee mbele.
 
Waambie muongozane kwenda kwenye nyumba ya ibada
na mfanyiwe maombi/dua ya pamoja kuondoa chochote kibaya kama kipo..
na uwaambie tu kuwa roho yako nyeupe huna kinyongo...waende

Duuuhh the boss mimi muumini wa RC hayo mambo ya maombi labda tukaungame sasa swali ni dhambi gani ya kuungama ambayo nimefanya??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom