Matanga
JF-Expert Member
- Nov 13, 2019
- 2,281
- 3,973
.
Sahau kuhusu ubao ila naomba ulikumbuke sana jina Meja Abdul Mingange, ufahamu mkubwa wa kiufundi, kumsoma mpinzani kisha anacheza soka la uchumi sana (speed economy)
.
Sahau kila kitu kuhusu ubao ila mtazame sana Deus Kaseke, leo kama in and out winger kama alikuwa chini, ni half winger kama alikuwa kati binafsi ni Man of the match, kete muhimu kwenye ulinzi na kushambulia
.
Sahau kuhusu ubao ila ondoka na jina la beki Paul Maona, mnara wa Baberi pale Ndanda huyu anakaba sana huyu, anachezesha sana huyu na ana footwork ya hatari sana huyu
.
Sahau kuhusu kitambaa cha Juma Abdul, rejea akili yake inawaza nini akiwa kama beki na miguu yake inaona wapi akiwa pembeni, anafit sana kwenye falsafa za Yanga, anautanua sana uwanja
.
Sahau kuhusu udogo wa Abdul Seleman Khamis, sahau kuwa yupo pale kwa mkopo kutokea Simba, ila rejea bao lake mbele ya Shikalo, brilliance mixed with talent, maamuzi ya kiume mbele ya Wanaume
.
Sahau kila kitu kuhusu umri wa Kelvin Yondan, naomba utazame yule Said Makapu anaecheza pembeni yake, shupavu sana yule ni shetani alievaa ngozi ya malaika, Mwanaume haswa pale nyuma, anajua kufanya marking zote tatu
.
Sahau tena kuhusu msimamo wa Ligi, mpe macho yako Vitalis Mayanga, control ipo mguuni, kasi ipo mguuni na nguvu ipo mguuni, bahati mbaya Makasy ana Uhuru mwingi zaidi yake uwanjani, ila ni hatari sana huyu
.
Sahau kuhusu mikono ya Shikalo, ila mkumbuke sana Feisal Salum 'Modric', Kiungo adimu sana hiki kikilindwa vyema na Makame, pass adimu sana, ni mtu pekee hatari kwenye pass pale Golden Square
.
Kumradhi kuna kiungo mmoja wa Ndanda, alizima namba 10 pale, kumradhi tena inakuwaje yupo pale, Azam inahitaji miguu ile, KMC wanahitaji huduma ile na angekuwa Mnigeria basi Simba wangemtaka yule, what a midfield
.
Wananchi sahauni kuhusu ushindi bali kumbukeni "The second winner is the first looser" hii nayo sahauni kama vipi
Sahau kuhusu ubao ila naomba ulikumbuke sana jina Meja Abdul Mingange, ufahamu mkubwa wa kiufundi, kumsoma mpinzani kisha anacheza soka la uchumi sana (speed economy)
.
Sahau kila kitu kuhusu ubao ila mtazame sana Deus Kaseke, leo kama in and out winger kama alikuwa chini, ni half winger kama alikuwa kati binafsi ni Man of the match, kete muhimu kwenye ulinzi na kushambulia
.
Sahau kuhusu ubao ila ondoka na jina la beki Paul Maona, mnara wa Baberi pale Ndanda huyu anakaba sana huyu, anachezesha sana huyu na ana footwork ya hatari sana huyu
.
Sahau kuhusu kitambaa cha Juma Abdul, rejea akili yake inawaza nini akiwa kama beki na miguu yake inaona wapi akiwa pembeni, anafit sana kwenye falsafa za Yanga, anautanua sana uwanja
.
Sahau kuhusu udogo wa Abdul Seleman Khamis, sahau kuwa yupo pale kwa mkopo kutokea Simba, ila rejea bao lake mbele ya Shikalo, brilliance mixed with talent, maamuzi ya kiume mbele ya Wanaume
.
Sahau kila kitu kuhusu umri wa Kelvin Yondan, naomba utazame yule Said Makapu anaecheza pembeni yake, shupavu sana yule ni shetani alievaa ngozi ya malaika, Mwanaume haswa pale nyuma, anajua kufanya marking zote tatu
.
Sahau tena kuhusu msimamo wa Ligi, mpe macho yako Vitalis Mayanga, control ipo mguuni, kasi ipo mguuni na nguvu ipo mguuni, bahati mbaya Makasy ana Uhuru mwingi zaidi yake uwanjani, ila ni hatari sana huyu
.
Sahau kuhusu mikono ya Shikalo, ila mkumbuke sana Feisal Salum 'Modric', Kiungo adimu sana hiki kikilindwa vyema na Makame, pass adimu sana, ni mtu pekee hatari kwenye pass pale Golden Square
.
Kumradhi kuna kiungo mmoja wa Ndanda, alizima namba 10 pale, kumradhi tena inakuwaje yupo pale, Azam inahitaji miguu ile, KMC wanahitaji huduma ile na angekuwa Mnigeria basi Simba wangemtaka yule, what a midfield
.
Wananchi sahauni kuhusu ushindi bali kumbukeni "The second winner is the first looser" hii nayo sahauni kama vipi