Niliyoyaona jana kwenye ATM ya NMB Gongolamboto yanatia aibu kwa watumishi

Walimu kwa mfano hua wanapenda sana kupanga foleni. Ni hobby yao hata ukiwawekea options 90 watakusanyana watiane ujinga weee wote watachagua option moja wakajazane ili wapange foleni.
 
Nilikuwa napita jioni kuelekea job. Si mnajua night shift zetu walinzi ndugu zangu. Nilikuwa nimempa lift mdanyakazi mwenzangu tukitokea Chanika.

Sasa nafika NMB Gongolamboto nikiwa barabarani jamaa akaniambia ona ile foleni, nikacheki kushoto nakuta foleni ya haja. Nikakumbuka kuwa ni tarehe ya mshahara. Mimi tayari nishatoa kwa simu, nina karibu mwaka siijui ATM machine.

Kwanini niseme niliyoyaona ni aibu kwa watumishi wa umma?
1. Hivi enzi hizi bado mtu na akili zake timamu anapoteza muda kwenye foleni huku makato ukitoa kupitia internet au sim banking yanalingana. Huu muda unaopotea kuokoa mia 4, buku au mia 5 mtu haoni ni hasara.

2. La pili linalotia aibu ni kwamba watumishi wengi wameambatana na wadeni wao ambao ndio walimiliki ATM card zao mpaka siku ya mshahara.

Jamaa yangu aliniambia wale waliokaa kwenye mawe ni wadau wanaowakopesha watumishi na kumiliki kadi zao na kuwapa siku ya mshahara wanapokutana kwenye ATM.

Nikafanya utafiti kuhusu hilo na kujihakikishia kuwa ni kweli. Aibu hii itaisha lini?

Serikali ipeleke wataalamu wa fedha na uchumi kwenye taasisi zake ili kuwafunda watumishi. Pamoja na maslahi ndogo ila mambo mengine yanatokana na ujinga (kukosa elimu ya kiuchumi na fedha) kwa watumishi.

Mtu anashindwa hata kui sacrifice laki 3 kujitosa kwenye ufugaji wa kuku. Aibu.
Ahueni kwenye maelezo yako umetumia neno watumishi wa umma!

Angekuwa ni mpwayungu village, moja kwa moja angesema hao watu wote aliowakuta kwenye hiyo ATM mashine ya Gongolamboto; ni walimu!
 
Kutoa wa wakala
KIASI GHARAMA
100,000 4,800

Kutoa kwa ATM
100,000 1,200

Kupanga ni kuchagua.
Binafsi sioni mantiki ya hii tabia ya Watanzania walio wengi ya kupenda kufuatilia maisha ya watu, na pia kupenda kuwapangia watu cha kufanya!

Imagine mtu yuko zake barabarani! Lakini anaumizwa kichwa na watu waliopanga foleni, kwa ajili ya kuchukua hela zao kwenye ATM mashine!!
 
Nilikuwa napita jioni kuelekea job. Si mnajua night shift zetu walinzi ndugu zangu. Nilikuwa nimempa lift mdanyakazi mwenzangu tukitokea Chanika.

Sasa nafika NMB Gongolamboto nikiwa barabarani jamaa akaniambia ona ile foleni, nikacheki kushoto nakuta foleni ya haja. Nikakumbuka kuwa ni tarehe ya mshahara. Mimi tayari nishatoa kwa simu, nina karibu mwaka siijui ATM machine.

Kwanini niseme niliyoyaona ni aibu kwa watumishi wa umma?
1. Hivi enzi hizi bado mtu na akili zake timamu anapoteza muda kwenye foleni huku makato ukitoa kupitia internet au sim banking yanalingana. Huu muda unaopotea kuokoa mia 4, buku au mia 5 mtu haoni ni hasara.

2. La pili linalotia aibu ni kwamba watumishi wengi wameambatana na wadeni wao ambao ndio walimiliki ATM card zao mpaka siku ya mshahara.

Jamaa yangu aliniambia wale waliokaa kwenye mawe ni wadau wanaowakopesha watumishi na kumiliki kadi zao na kuwapa siku ya mshahara wanapokutana kwenye ATM.

Nikafanya utafiti kuhusu hilo na kujihakikishia kuwa ni kweli. Aibu hii itaisha lini?

Serikali ipeleke wataalamu wa fedha na uchumi kwenye taasisi zake ili kuwafunda watumishi. Pamoja na maslahi ndogo ila mambo mengine yanatokana na ujinga (kukosa elimu ya kiuchumi na fedha) kwa watumishi.

Mtu anashindwa hata kui sacrifice laki 3 kujitosa kwenye ufugaji wa kuku. Aibu.
Sasa Hilo Jimbo lenu lots ATM zipo nne tu unategemea Nini?
 
Kumbe na wee unawaonea wivu walimu kwani kupiga foleni Ni aibu gani wakati naenda kuchukuwa mpunga wangu alfu siyo kila kitu nikimbilie internet au sim banking sometime hyo simu bank sinasumbua na kupeleka kusubiri sna pesa iingiee

Tuache bhna tukachukue hell zetu na zako za ulizni subiria upewe dirishani kwa muhindi
Ahahahaha.
Kumbe ni walimu wale waliokuja na wadeni wao.
Hongera mwalimu
 
Mishahara yote kupitia NMB ni maamuzi ya ajabu
Hapana.
Mimi 2015 wakati naajiriwa niliambiwa nipeleke account ya NMB, NBC, penki ya posta au crdb.
Ila kipindi kile crdb walikuwa wakilipwa siku moja kabla ya NMB na siku 2 kabla ya NBC na posta. Hivyo hr akanishauri nitumie crdb .
Sema kuna taasisi hawawaambii watumishi wao kuwa wana uhuru wa kuchagua benki ya kupitishia mshahara wao.
Hata mifuko ya hifadhi ya jamii ma hr wengine walikula rushwa na kuwapangia watumishi mfuko mmoja jambo ambalo ni kinyume cha haki za mtumishi.
 
1. Hivi enzi hizi bado mtu na akili zake timamu anapoteza muda kwenye foleni huku makato ukitoa kupitia internet au sim banking yanalingana. Huu muda unaopotea kuokoa mia 4, buku au mia 5 mtu haoni ni hasara.
Kwani umeshaona mtu ana passbook miaka hii? Nadhani ungeanza kwa kuyashambulia mabank kwanini wanainstall ATM machine na kwanini wanatengeneza card, mabank yakiua hiyo teknolojia ya atm basi watu watatumia simu,
 
Back
Top Bottom