niliwahi kuiambia tume ya mabadiliko ya katiba ya warioba lakini ilinipuuza

Rose Mayemba

JF-Expert Member
May 7, 2012
721
1,017
Siasa za Tanzania zimekaa kisanii sana,kila mtu anayejiona ana uwezo wa kulaghai hujitafutia tiketi ya kuingia Ikulu ama Bungeni.Hakuna sheria yoyote kwa ajili ya hawa watu hasa inapotokea wamekwenda kinyume na matakwa ya waliowachagua.

Nilitoa mapendekezo yangu kwenye tume ya Warioba kwamba katika katiba wanayoiandaa mbali na wananchi kuwa na mamlaka ya kumwondoa pale wanapoona hatendi sawa na walivyomtuma lakini pia iwepo sheria ya kuwaadhibu pale wanapoonekana kutokutekeleza yale waliyoyaahidi wakati wa kuomba kura pindi wamalizapo muda wao wa uongozi.


Baba wa taifa aliwahi kusema" ili Tanzania iwe IMARA ni lazima tuwe na UONGOZI BORA,ARDHI PAMOJA NA SIASA SAFI"

Lakini sasa hatuwezi kuwa na UONGOZI BORA kwani viongozi wengi tulionao tuliwapata kwa siasa CHAFU,zilizojaa UONGO na ukiukwaji ya maadili.

Mimi nitaendelea kusema hatutapata kuendelea TANZANIA hata tukibadilisha vyama kila siku hadi hapo tutakapopunguza hii idadi ya watu wanaokwenda kuneemesha matumbo na familia zao huku wakiancha wananchi wanateseka.Na mbaya zaidi huachwa tu kama wafalme huku wakiwa wamekengeuka maadili ya kitaifa.


THINGS WILL CHANGE BUT WE NEED TO CHANGE OUR SELVES FIRST
 
Mbunge kazi yake kuisimamia govt,govt ndio inatekeleza mipango ya maendeleo
 
Tume haijakupuuza ndio maana kwenye rasimu hii wametoa pendekezo lako la kumwajibisha mbunge pindi anapoenda kinyume na matakwa ya waliomchagua
 
Mh?! Nitarudi baadaye. Ngoja nijipange

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Mbunge kazi yake kuisimamia govt,govt ndio inatekeleza mipango ya maendeleo

Lipo wazi kabisa, Tatizo wengi wanafikiri kazi ya Mbunge ni Kuleta Barabara, Madaraja, zahanati na shule kama vile mbunge anabajeti. Na hili ndilo lilosababisha wabunge wakaomba Mfuko wa bunge eti na wAo ni watekelezaji wa mipango ya sijuhi ni nani huwa anawasimamia.
 
Siasa za Tanzania zimekaa kisanii sana,kila mtu anayejiona ana uwezo wa kulaghai hujitafutia tiketi ya kuingia Ikulu ama Bungeni.Hakuna sheria yoyote kwa ajili ya hawa watu hasa inapotokea wamekwenda kinyume na matakwa ya waliowachagua.

Nilitoa mapendekezo yangu kwenye tume ya Warioba kwamba katika katiba wanayoiandaa mbali na wananchi kuwa na mamlaka ya kumwondoa pale wanapoona hatendi sawa na walivyomtuma lakini pia iwepo sheria ya kuwaadhibu pale wanapoonekana kutokutekeleza yale waliyoyaahidi wakati wa kuomba kura pindi wamalizapo muda wao wa uongozi.


Baba wa taifa aliwahi kusema" ili Tanzania iwe IMARA ni lazima tuwe na UONGOZI BORA,ARDHI PAMOJA NA SIASA SAFI"

Lakini sasa hatuwezi kuwa na UONGOZI BORA kwani viongozi wengi tulionao tuliwapata kwa siasa CHAFU,zilizojaa UONGO na ukiukwaji ya maadili.

Mimi nitaendelea kusema hatutapata kuendelea TANZANIA hata tukibadilisha vyama kila siku hadi hapo tutakapopunguza hii idadi ya watu wanaokwenda kuneemesha matumbo na familia zao huku wakiancha wananchi wanateseka.Na mbaya zaidi huachwa tu kama wafalme huku wakiwa wamekengeuka maadili ya kitaifa.


THINGS WILL CHANGE BUT WE NEED TO CHANGE OUR SELVES FIRST

Kutekeleza ahadi huwa ni Jambo gumu sana kutokana na Wananchi wenyewe kulazimisha kumpa kura Mbunge ambaye anaenda bungeni kupiga meza na kusinzia kisha kupokea posho na kuhamia Dsm jimboni kwenda kwa nadra .aina ya wabunge Hawa ni vigumu sana kutekeleza ahadi kwani hata Mawaziri hutekeleza ahadi kulingana na speed ya ufuatiliaji na hoja za mbunge mwenyewe .umefika wakati wabunge wote wawe wakazi harisi wa jimbo na waishi huko huko jimboni wasihamie Dsm kama ilivyo sasa .
 
Back
Top Bottom