Zero unit
JF-Expert Member
- Aug 9, 2017
- 288
- 220
Hapa jamaa naona alishaanza kutulisha matango poriMkuu mtoto wa mstaafu, Keagan Paul, naomba uniruhusu nicomment kidogo. Kuna vitu kwenye stori yako havipo sawa kidogo, naelewa huenda labda umeamua kuvifanya visiwe sawa kwa maksudi na si kwa bahati mbaya. Kuna sehemu nimekusoma unasema wale jamaa wanaomuuzia "nyaupe" jamaa Y wanafanya kazi kama punda. Hapo mzee umepindisha ukweli, Dizonga hakuna wabongo wanaokula bata kama wauza nyaupe. Kufanya kazi kama punda kwako wewe labda kuna tafsiri gani? Maana hao jamaa kazi yao ni kupokea simu tu na kupeleka mzigo location unapohitajika na akifika pale ni kitendo cha sekunde mbili keshamaliza kazi, haina hata kuhesabu hela, hela itahesabiwa baada ya kuondoka eneo la tukio, na wale wanunuzi ni waamifu sana hawatoi hela pungufu japo hamuhesabiani eneo la tukio. Zaidi ya yote jamaa wana usafiri hawasambazi kwa miguu, hata kama mtu ameanza kuuza leo haiwezi kumchukua zaidi ya mwezi hajapata usafiri, sasa unaposema wanafanya kazi kama punda kidogo kama umepindisha uhalisia. Pia umesema huwa wanaweka hizo kete mdomoni na polisi wakivamia wanazimeza, mzee hii pia sio kaka. huwezi kumeza madawa kizembe hivyo. Donga ndio zinamezwa wakati wa kuzisafirisha intercontinental lakini sio mzigo umeshafika ndani ya nchi bado mtu ameze. Hiyo risk hakuna mtu wa kuitake, kwanza ufungaji wa hizo kete sio imara sana uimeze halafu ubaki salama. Ufungaji wa donga ndio imara unaweza kumeza na ukasurvive lakini sio kete mkuu. Halafu mademu wa Gauteng yaani Joburg na Pretoria wana attitude flani tofauti na uliyoielezea tena kama hapo Midrands ndio kabisa. Nimekaa Randburg kama miaka 6 au 7, 209 Bellairs Drive, Banbury Cross, North Riding. Randburg nadhani kwa Johannesburg ni sehemu wanayokaa matajiri wa South Africa ukitoa Sandton na Fourways. Ninachotaka kusema hapa mademu wa kishua wa Gauteng nazijua attitude zao maana nimeishi nao. Pia umesema permit (viza) yako iliexpire ukiwa bado kwa bwana Y, sasa uliwezaje kutafuta kazi wakati tayari ulikuwa unaishi kinyume cha sheria maana kitu cha kwanza lazima wakuulize ID yako. Mind you Johannesburg na Pretoria ni miji ambayo kama huna permit ni ngumu sana kusurvive. Joburg hata ukiwa unatembea barabarani unaweza kushitukia tu unasimamishwa na police na kuombwa ID tofauti na miji mingine kama Durban, sasa wewe uliwezaje kutafuta kazi wakati hata permit yenyewe huna? sijui kama umenielewa? Na kwa Johannesburg misako ya kutafuta wahamiaji haramu ipo kila uchwao.