Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Huo ndo ukweli ndugu yangu. Ukizunguka zunguka duniani utaona jinsi wanaija na wakenya wanatupiga magepu yaani kuna watoto wazazi wao walifanya shughuli za ajabu ajabu wanesomea mambelez huko saiv wana kazi za heshima balaa. Na huwez amin kiakili za darasani tumewaacha mbali sana ngozi nyeupe. Sie tunadumaa kutokana na malezi

Ila mwanao akikulia mbelez wanakujaga kuwa moto sana biashara kubwa au makazi makubwa udaktari mainjinia IT specialists ila watoto wa vibaka wa zamani. Saivi wanarudisha investment nyumbani

Sasa huku wewe unazaliwa masikini unalaani hadi kizazi chako wazaliwe vile vile km ww kwa uoga wa kujilipua

Ndo nimetoa mfano mdogo huo wale wapelelezi waliokuja mwanzoni kabla ya ukoloni unadhani walikua hawaogopi?? Wamekuja sehemu ni misitu tu na stori kuwa watu wanakula nyama za watu hata nguo hatuvai ila wakaja wakatuua wakatukata mikono mpk tukatia akili na wakatutawala kwa manufaa ya nchi zao. Leo hawaonekani kama wahalifu Bali mashujaa
Thanks Mkuu.... This Year..... Lazima nivuke Boda Kadhaa
 
Wakuu eeh mnawafahamu wasomali...
Umoja wao mnaufahamu?
Umeshawahi onalife lao?
Wanaishi mtaa mmoja..
Wanachukuana kwao kila siku...
Tatizo wanalibeba wote...
Pia nao kwa kujilipua so haba ..border hapa karibu kila siku wanavushwa kwenda Sa ...Baada ya muda wanarudi walionyookewa na maisha wanakuja kuchukua wenzao.. l
Kama wasomali wa hapa border dah Mshikamano wao nimeipenda.

Wabongo tuache ungese
 
Hii Kitaalamu tunaitaje mkuu?
900099.jpg
 
@Noelia unajua huwa tunakosea sana sisi wabongo...

Passport ni hati au kibali cha kusafiria na tena kukutambulisha wewe kwa taifa jingine kama ni Mtanzania...

Sasa tujiulize wote tu, kama hauna mpango wa kwenda nchi nyingine, kwa nini uhitaji passport?

Halafu pia restrictions zinakuwa nyingi sababu kuna watu wanatumia passport kufanikisha shughuli zao za kiharamia kama kupitisha madawa ya kulevya n.k, sasa kama taifa huwezi tu kuwa unatoa passport ili kufanikisha mauharamia...

Mfano kipindi tulipokuwa na passport ya zamani (ile ya gamba la kijani), passport ya bongo ilikuwa shamba la bibi, watu wa mataifa mengine waliitumia sana kufanya mambo yao especially kwa zile nchi ambazo mbongo anaingia kwa kupata entry visa airport...
Sasa pamoja na kubana kote huko "kwa RAIA wote wanaostahili" bado wakapewa "Wasiokua RAIA" unadhani ni approach sahihi???

Kwani wanaouaza madawa ya kule vya hapa hapa Tanzania wana passport?? Yaan passport haishusiani na madawa ya kulevya kwanini waihusishe??? Hapo ndo kuna tatizo ni mawazo ya kizamani sana

Okay kama Passport ni document mpaka uwe na safari Ingekua inadumu kwa hiyo safari moja uliyoombea tu halafu inaexpaya. Mtu aliyesafir mara moja tu kihalali anakua nayo kwa miaka 10 kwanini kila mtu anayehitaji asiwe nayo standby?? Mtu akishaomba manaake ana mpango wa safari na ni haki yake apewe. Makosa yatakayofanyika akiwa na hiyo passport atahukumiwa kwa aliyotenda kwann umnyime kwa kudhania "eti" atafanyia uhalifu

Muhalifu ni muhalifu tu akiamua hata asipokua nayo atasafiri tu......
 
Ila tuache Utani JF Ni Raha Sana Yaani Mpaka unakuwa Addicted kabisa Bila Kuingia JF unaona siku haijaenda Kabisa
Mimi (Keagan Paul) nikiwa na akili zangu timamu, naapa kwamba nitasimulia kila kitu kama nilivyoahidi kwa mujibu wa sheria iliyowekwa.

Na kwamba nitasimulia mwanzo hadi mwisho bila kuingiwa na tamaa za kuhamia telegram.

Ee mnyaazi Mungu nisaidie.
 
SEHEMU YA KUMI NA NNE

Basi nikaanza maisha yangu mapya ndani ya south pale Kalfonteen. Ratiba ya kwenda Kanisani ilikuwa ni karibia kila siku. Uzuri wao muda wa kwenda Kanisani ni Jioni kuanzia saa kumi na mbili na kutoka saa nne usiku. Mpaka Jumapili muda ni huo huo. Gari ilikuwa inatufata mpaka getini, tunaingia hao kanisani. Kwenye gari mnakuwa wengi. Nilikuwa nikifika Kanisani najichanganya sana na Vijana wenzangu, wazee, watoto mpaka Mchungaji nilianza kumzoea. Kwenye maisha ukiamua kujilipua, jilipue mazima, usijilipue nusu nusu, lazima uwe na uwezo mkubwa wa kujitoa ufahamu. Mimi sikuwa mwoga kama Wabongo wengi. Hata hapa Bongo nilikuwa sio mtu wa kwenda sana Kanisani, lakini kule ilikuwa kila siku nipo. Tena vile usafiri wa kwenda na kurudi bure, nyumba Bure, Basi kila siku nilihudhuria Ibada.

Kiongozi wetu kwenye upande wa Camera alikuwa anaitwa Max. Nilimfanya Max kuwa rafiki. Ndani ya muda mfupi nilihakikisha watu wengi wananizoea. Kanisa lilikuwa na siku za Michezo, ilikuwa ikifika siku hiyo naingia uwanjani kucheza mpira wa miguu. Nilikuwa najitahidi kucheza kweli kweli. Uwanja mzima nakimbiakimbia tu. Macho yangu yote yalikuwa kwa washua. Nikaanza kujipendekeza kwa watoto wao. Kupitia Kanya niliwazoea watu wengi pale Kanisani mpaka watu wakaanza kuhisi na date na Kanya hata kabla sijaanza hizo harakati.

Kanya alikuwa anapenda sana kupiga story na mimi. Ukweli hapa ndo kidogo nilianza kuinjoi maisha ya South Africa. Nilikuwa nakaa na watu ambao hata nikitembea nao barabarani nina amani.

Nilichokuwa nafanya muda wa mchana ambao nakuwa free, Kwa kutumia ile Akiba yangu nilikuwa natoka mwenyewe nakwenda mpaka Johanesburg kutembea tembea, Nilikuwa nashuka pale MTN Taxi Rank huyo naingia Mitaani. Nilikuwa nasambaza Barua zangu za Maombi ya Kazi. Niliomba kila aina ya Kazi ilmradi tu iwe ya halali. Nakumbuka niliendaga mpaka sehemu inaitwa Auckland Park, Sehemu ambayo kuna Media mbalimbali kubwa kama SABC, BBC na Media 24. Kwa kuwa nilikuwa najua kidogo mambo ya Camera, kote huko niliacha Barua zangu. Pale BBC nilikutana na Jamaa wa BBC Swahili, Nilikutana na Mzee Anaitwa Omary Muktadha. Hapa nitarudi kufafanua zaidi huko mbele. Kwa hiyo nikawa nafanya hivyo kila nikiwa free nakwenda maeneo mbalimbali, nilikuwa siogopi, nakwenda kwenye maviwanda huko.

Nirudi kwa Thomas, Thomas alikuwa ni mpiga Kinanda pale Kanisani, alikuwa hajui kama Kanya aliniambia kila kitu kuhusu Chumba tulichokuwa tunakaa kama kinalipiwa Kodi na Kanisa. Nashangaa siku moja nimeamka zangu Thomas ananiomba hela ya Kodi. Nikamwambia mbona nimeambiwa hapa Kodi inalipwa na Kanisa, alivyojua najua kila kitu, akaanza kuwa ananuna nuna bila sababu. Hakuna tabu kama kuishi na mtu ambae asubuhi anaamka amenuna bila sababu. Mtapiga story pale atakapojisikia yeye kuongea. Alikuwa Mjinga kweli yule jamaa. Kwa kifupi Thomas alitaka kunipiga hela Kupitia hicho chumba, Chakula tu ndo mtu ulikuwa unajitegemea.

Nilikuwa natumia Akiba yangu nanunua chakula cha kutosha naweka ndani nakuwa najipikia tu. South Africa chakula bei rahisi. Kule gharama kubwa ipo kwenye Kodi za Nyumba na Nauli kwenye vyombo vya Usafiri. Kule Umbali wa Makumbusho mpaka Posta, Kwa Taxi zao, Kule ukisema Taxi ndio Daladala, unaweza kulipia hata Elfu 2 mpaka 3 za Kitanzania. Hiyo ni nauli ya kwenda tu.

Sasa Thomas alikuwa hanunui chakula. Yeye alikuwa akirudi akikuta chakula anakula tu. Tena wakati mwengine alikuwa anakuja kula na rafiki zake. Wakiwa na hela hao walikuwa wanaenda kula KFC, Hakikosa hela anarudi kula nyumbani. Mimi nanunua chakula kwa bajeti zangu. Nilikuwa navumilia ivo ivo tu siku ziende nitimize malengo yangu.

Mara nyingi Kanya alikuwa anakuja pale ghetto, ananisaidia kupika, kufua na kufanya mambo mengine. Kanya alikuwa mzuri na halafu alikuwa na Bonge la Tako.Yan bonge la Shape. Ila mimi ni kama vile nilikuwa namkwepa kwepa kwa sababu mle Kanisani kuna demu nilishamuona, huyo demu huwa anakuja na gari yake, halafu anaonekana kama matawi fulani hivi. Nilikuwa namkwepa Kanya ili asije kuniaribia kumpata huyo mtoto, Kanya alikuwa anaishi kama mimi tu kwenye nyumba inayolipiwa Kodi na Kanisa. Niliona nikianzisha nae mahusiano atakuwa mzigo kwangu, wakati mimi nilipanga kuwa mzigo kwa mtu mwengine.
Lakini Kanya aliniganda kinyama.

Hata Mimi majina ya kina Thomas nilip wahi kukutana nao ni watu kama huyo jamaa wana tabia za kujisikia na kususa susa
 

Similar Discussions

67 Reactions
Reply
Back
Top Bottom