Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Alikuwa anajua machejo lakini? 😂😂
Wala sikujali, aliniambia katokea Republic of Ireland wakati huo 2006 nilikuwa nikifikiri ni Nchi za umoja wa Kisoveti kwenye njaa

Baadae ndio kuja kugundua daah!
 
Mzee wa buza endelea basi na story
SEHEMU YA SABA

Tulifika pale CHIRUNDU nikiwa makini sana yasije yale ya Tunduma yakajirudia. Nilikuwa naogopa sana kutumia pesa nyingi kwa sababu nilikua sijui niendapo.

Kuna swali kuna mdau ameniuliza naomba nilitolee ufafanuzi, ameniuliza kama Bongo nilikuwa sina ajira nilipata wapi hiyo pesa Milioni Moja ya kuweka Akiba Banki. Ni hivi hapo Kabla kuna Ofisi nilikuwa nafanyia Kazi, kuna wafanyakazi tulipunguzwa ndipo nikaanza kufatilia mafao yangu pale GEPF. Mafao yangu hayakuwa makubwa sana ndo nilitumia kwenye hii Safari.

Sasa tuendelee, Pale Chirundu nilipanga foleni hadi kwa Afisa Uhamiaji, Swali langu kichwani likiwa moja tu, Je niweke hela kidogo katikati ya Passport kama nilivyofanya Tunduma? Uzuri hapa hapakuwa na Vishoka wengi kama Tunduma. Yule Dada Matilda ambae ni Abiria mwenzangu tulishaanza kuzoeana kidogo, kumbuka yeye alikuwa ni mzoefu wa hii njia, alinifuata akaniambia mdogo angu sio kila sehemu unakimbilia kuweka hela, soma kwanza upepo. Ukiwa na mazoea ya kuweka hela kila boda utaishiwa utafika South bila hela. Nikamwambia basi Dada tangulia, Mimi nitapanga foleni nyuma yako. Akasema sawa.

Tulifanikiwa kugongewa Mihuri bila kutoa pesa Ila kwa tabu sana maana maswali yalikuwa mengi, Mara kuna karatasi walinipa nijaze, niandike taarifa zangu, Kama Passport Namba, Mahali ninapokwenda, Namba za Bus nililopanda na maelezo mengine. Utaratibu huu wa kupewa karatasi tulipewa wengi. Lakini mwisho wa siku tulikomaa hatukutoa hela.

Tulifanikiwa kuingia nchi ya Zimbabwe mpaka Harare.Tulifika Harare kwenye kama saa kumi na moja jioni. Pale Harare ilikuwa ni stand ndogo, sio kubwa kama Ubungo lakini ilikuwa na Mabus mazuri sana. Tulikuta kuna wapiga debe kibao wa Mabus hayo ambao ni Wabongo, kwa hiyo tulivyoshuka tu kwenye Bus walitukimbilia na kutupa Msaada wa kupata Bus la South.

Pale tulitawanyika kwenye mabasi mbalimbali, kwenye bus nililopanda Mimi tulikuwa wabongo 4 tu, Nilikuwa Mimi , Ahamad, Matlida na Jamaa mwengine. Ndani ya Bus wengi walikuwa ni abiria wa pale Zimbabwe na Zambia. Ndani ya Bus Kiswahili ndo kilipotea kabisa. Hata Matangazo ya ndani ya Bus yalitolewa kwa lugha zao za pale Zimbabwe.

Nakumbuka tukiwa tumeanza safari, tunatoka pale Stand, niliwaona wale madogo wakiingia mtaani utafikiri ni wenyeji vile. Ukweli nilijifunza kitu kutoka kwa wale madogo, walikuwa majasiri mno.

Hatimae usiku wa saa Tisa, tulifika Boda ya Mwisho ya BeitBridge, Nadhan ndio Boda kubwa ukanda wetu wa chini mwa jangwa la Sahara. Palikuwa busy balaa, watu kibao.

Nilivyoona watu wengi vile, kitu cha kwanza nilichojisemea moyoni ni kwamba "Muda huu Mimi huwa nimelala kumbe kuna sehemu nyengine hapa duniani muda huu watu wapo busy hivi"

Kulikuwa na watu mataifa mbalimbal, Weupe na Weusi. Sasa wabongo tukawa kama ndugu tayari. Ukweli moyoni nilikuwa siwaamini sana hawa jamaa maana nilishawai kusikia South Afrika, Wabongo kwa wabongo ndo hatari kuliko hata wageni. Lakini nikasema No sweti maji nishayavulia nguo. Kama wakitaka kuniibia au kunifanya jambo baya poa tu. Hata Matlida mara nyingi alikuwa ananihimiza dogo usiwaamini sana wabongo watakuliza. Basi muda wote nilikuwa makini.

Tulipanga foleni kwenye Ofisi za Uhamiaji, yule jamaa mwengine alisema tukitaka South Africa tupewe siku nyingi za kuishi humo, hapo ni Lazima katikati ya Passport tuweke hela.

Alisema tusipoweka hela basi tutapewa siku chache sana. Huyo jamaa, Ahamad na Matlida wakawa wanabishana pale, Matlida anasema tusiweke, yule jamaa anasema lazima tuweke la sivyo tutapewa siku chache mno.

Matlida anasema hata tukipewa siku chache sio mbaya maana lengo tufike kwanza, tukishafika hayo mengine tutajua huko ndani namna ya kuongezewa muda.

Mwisho wa mabishano tukakubaliana tuweke pesa, ila kwenye foleni yule jamaa ndo asimame mbele yetu, yaani awe wa kwanza. Mimi nilisimama nyuma yake. Matlida akasimama nyuma yangu, Ahamad akasimama nyuma ya Matlida. Foleni yetu ilivyofika Kaunta. Mara nikashangaa yule Askari wa Uhamiaji wa pale Kaunta anamuita Askari mwenzie aje kumkamata yule jamaa etu kwa kosa la kutoa rushwa. Ukweli nilitetemeka kishenzi, fasta sana nilitoa pesa niliyoiweka katikati ya Passport yangu kisha nikasogea pale Kaunta. Yule Mzungu Mkaburu akawa ananiangalia tu.
 
Msimuliaji usiache kujua kuwa kunawatu wameinywea KAHAWA hii story yako mkuu
 
SEHEMU YA NANE

Ukweli ndugu zangu moja ya kitu nilichojifunza kwenye Safari hii sio kwamba ukifika kila boda basi unakimbilia kutoa pesa. Unatakiwa kusoma kwanza upepo wa Boda husika.

Kwenye hii boda ya BeitBridge tulikosea kwa sababu pale Kaunta kulikuwa na Mkaburu. Wazoefu wanasema ukikuta pale Kaunta amekaa Mkaburu basi usikimbilie kutoa rushwa. Sababu wanasema Mkaburu hapendi sana watu weusi, hivyo ukianza tu kutoa rushwa ndo anapata sababu ya kutokukuruhusu kuingia nchini mwao.

Basi Mimi namshukuru mungu yule Mkaburu akaniangalia kisha akanigongea mhuri. Nakumbuka alinipa Mwezi mmoja tu wa kukaa South Africa. Wenzangu walipewa Wiki mbilimbili. Jamaa zangu waliniambia Mimi nilipewa Mwezi mmoja sababu yule Mkaburu aliona Passport yangu haijawai kugongwa Mhuri wa Africa Kusini. Wao walipewa siku chache kwa sababu Passport zao zishagongwa sana Mihuri ya Afrika Kusini.

Mpaka tunarudi kwenye Bus yule Jamaa etu walikuwa bado wamemshikiria. Tuliondoka tukamuacha pale, tena hata namba za simu tulikuwa bado hatujapeana. Mpaka kunakucha tulikuwa bado tupo njiani.

Ahamad aliniambia kama sina sehemu ya kufikia basi nishuke nae Pretoria. Kwa sababu Bus kabla ya kufika Joberg linafika kwanza Pretoria. Ahamad akasema tushuke wote hapo atanitafutia sehemu ya kukaa kwa jamaa zake ambae ni wabongo. Matlida yeye alikwenda kushukia Mwisho wa Bus kule Power House Karibu na Park Station Joberg.

Mimi na Ahamad tulishuka pale Pretoria kama saa Nane mchana. Ukweli nchi ya wenzetu ni nzuri sana.

Nilikuwa natembea huku najiuliza "Kama hapa pako hivi huko Ulaya na Marekani patakuwa vipi?" Watu wanajua kujenga nchi zao.

Ahamad alikuwa na miaka kama mitano toka atoke South hivyo tulivyoshuka tu tukawa tunapita mitaa Fulani ya washkaji zake anakwenda kuwasalimia. Mimi nipo nyuma yake tu. Nakumbuka tulikwenda mpaka mitaa Fulani kuna Wazanzibar wengi wana maduka. Tukaacha hapo mabegi yetu. Mimi nilikuwa sina imani kuacha hapo Begi langu lakini kwa kuwa ATM Card yangu ilikuwa mfukoni nikasema sio mbaya, kilichokuwa kinanipa wasiwasi peke yake ni vyeti vyangu vyote vilikuwepo ndani ya Begi. Ukishaamua kujilipua inabidi uwe na roho ngumu.

Tulivyofika hapo Pretoria ndo nikajua kuwa kumbe Ahamad alikuwa anaendelea na Safari ya kwenda Capetown. Hapo alikuja kukutana na Dada yake ambae wangekwenda wote Capetown kwa ndege. Huyo Dada yake alikuwa ameolewa huko Capetown na Tajiri mmoja. Maelezo yote hayo alinipa Ahamad mwenyewe.

Tukaenda mahali kukutana na Huyo Dada yake, naye ni Mtanzania. Nakumbuka alikuja na Range Rover mpyaa, tukaingia ndani, kisha Ahamad akanitambulisha kwa Dada yake. Dada yake akasema kwa kuwa wao walikuwa wanawahi kupanda ndege basi Mimi ataniacha kwa rafiki yake.

Hao mpaka kwa huyo rafiki yake, tulivyofika kwa huyo rafiki ake, Dada yake na Ahamad akaniuliza "Unamjua huyu". Mimi nikamjibu hapana simjui. Nikawa namwangalia vizuri yule Mrembo ambae nimepelekwa kwake. Nikajiridhisha kuwa simjui.

Dada yake na Ahamad akasema "Huyu ni Vailet, yule Video Queen kwenye Wimbo wa Matonya, ule wimbo wa Vailet, huyu ndo Vailet mwenyewe"

Duh nikabaki nimeduwaa tu, demu amekuwa mrembo kinoma noma. Kumbe Alishakimbiliaga South Afrika Kitambo sana. Wakuu ukitaka kumkumbuka vizuri huyu demu unaweza kuingia YouTube, Video ya Matonya wimbo wa Vailet, ndo huyo demu mule ndani. Mimi nikaachwa pale. Ahamad na Dada yake hao wakaondoka kuchukua mabegi wakaniletea Begi langu kisha wenyewe wakasepa Capetown.
 
SEHEMU YA NANE

Ukweli ndugu zangu moja ya kitu nilichojifunza kwenye Safari hii sio kwamba ukifika kila boda basi unakimbilia kutoa pesa. Unatakiwa kusoma kwanza upepo wa Boda husika.

Kwenye hii boda ya BeitBridge tulikosea kwa sababu pale Kaunta kulikuwa na Mkaburu. Wazoefu wanasema ukikuta pale Kaunta amekaa Mkaburu basi usikimbilie kutoa rushwa. Sababu wanasema Mkaburu hapendi sana watu weusi, hivyo ukianza tu kutoa rushwa ndo anapata sababu ya kutokukuruhusu kuingia nchini mwao.

Basi Mimi namshukuru mungu yule Mkaburu akaniangalia kisha akanigongea mhuri. Nakumbuka alinipa Mwezi mmoja tu wa kukaa South Africa. Wenzangu walipewa Wiki mbilimbili. Jamaa zangu waliniambia Mimi nilipewa Mwezi mmoja sababu yule Mkaburu aliona Passport yangu haijawai kugongwa Mhuri wa Africa Kusini. Wao walipewa siku chache kwa sababu Passport zao zishagongwa sana Mihuri ya Afrika Kusini.

Mpaka tunarudi kwenye Bus yule Jamaa etu walikuwa bado wamemshikiria. Tuliondoka tukamuacha pale, tena hata namba za simu tulikuwa bado hatujapeana. Mpaka kunakucha tulikuwa bado tupo njiani.

Ahamad aliniambia kama sina sehemu ya kufikia basi nishuke nae Pretoria. Kwa sababu Bus kabla ya kufika Joberg linafika kwanza Pretoria. Ahamad akasema tushuke wote hapo atanitafutia sehemu ya kukaa kwa jamaa zake ambae ni wabongo. Matlida yeye alikwenda kushukia Mwisho wa Bus kule Power House Karibu na Park Station Joberg.

Mimi na Ahamad tulishuka pale Pretoria kama saa Nane mchana. Ukweli nchi ya wenzetu ni nzuri sana.

Nilikuwa natembea huku najiuliza "Kama hapa pako hivi huko Ulaya na Marekani patakuwa vipi?" Watu wanajua kujenga nchi zao.

Ahamad alikuwa na miaka kama mitano toka atoke South hivyo tulivyoshuka tu tukawa tunapita mitaa Fulani ya washkaji zake anakwenda kuwasalimia. Mimi nipo nyuma yake tu. Nakumbuka tulikwenda mpaka mitaa Fulani kuna Wazanzibar wengi wana maduka. Tukaacha hapo mabegi yetu. Mimi nilikuwa sina imani kuacha hapo Begi langu lakini kwa kuwa ATM Card yangu ilikuwa mfukoni nikasema sio mbaya, kilichokuwa kinanipa wasiwasi peke yake ni vyeti vyangu vyote vilikuwepo ndani ya Begi. Ukishaamua kujilipua inabidi uwe na roho ngumu.

Tulivyofika hapo Pretoria ndo nikajua kuwa kumbe Ahamad alikuwa anaendelea na Safari ya kwenda Capetown. Hapo alikuja kukutana na Dada yake ambae wangekwenda wote Capetown kwa ndege. Huyo Dada yake alikuwa ameolewa huko Capetown na Tajiri mmoja. Maelezo yote hayo alinipa Ahamad mwenyewe.

Tukaenda mahali kukutana na Huyo Dada yake, naye ni Mtanzania. Nakumbuka alikuja na Range Rover mpyaa, tukaingia ndani, kisha Ahamad akanitambulisha kwa Dada yake. Dada yake akasema kwa kuwa wao walikuwa wanawahi kupanda ndege basi Mimi ataniacha kwa rafiki yake.

Hao mpaka kwa huyo rafiki yake, tulivyofika kwa huyo rafiki ake, Dada yake na Ahamad akaniuliza "Unamjua huyu". Mimi nikamjibu hapana simjui. Nikawa namwangalia vizuri yule Mrembo ambae nimepelekwa kwake. Nikajiridhisha kuwa simjui.

Dada yake na Ahamad akasema "Huyu ni Vailet, yule Video Queen kwenye Wimbo wa Matonya, ule wimbo wa Vailet, huyu ndo Vailet mwenyewe"

Duh nikabaki nimeduwaa tu, demu amekuwa mrembo kinoma noma. Kumbe Alishakimbiliaga South Afrika Kitambo sana. Wakuu ukitaka kumkumbuka vizuri huyu demu unaweza kupitia Video ya Matonya wimbo wa Vailet, ndo huyo demu mule ndani. Mimi nikaachwa pale. Ahamad na Dada yake hao wakaondoka kuchukua mabegi wakaniletea Begi langu kisha wenyewe wakasepa Capetown.
Hio picha ya vailet wa Matonya ipo wapi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom