Makanyaga
JF-Expert Member
- Sep 28, 2007
- 10,318
- 6,846
Mjadala ulikuwa kati ya Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Meli (TASAC) na Mawakala kutoka sekta binafsi.
Kitu kilichonivutia kwenye mjadala huu ni baada ya mawakala kutoka sekta binafsi kutoa malalamiko yao kuwa TASAC ameamua kuwa wakala lakini akaweka sheria kuwa yeye hatakuwa na LIABILITY kutoka kwa PRINCIPALS wake. Mimi hiki kitu kilinichanganya kidogo kwa sababu kadhaa kama nitakavyoeleza hapa chini,na kabla ya kwenda mbali zaidi, naomba ni-dikilee interest kuwa NIMESOMA LAW OF AGENCY (kikiwemo kipengele cha AGENCY BY NECESSITY), pamoja na SALE OF GOODS CONTRACT. Hizi sheria mbili nimezisoma na ninazielewa kwa kiasi, japo siyo sana.
Ni kwamba AGENT kutokuwa na LIABILITY kwa principal wake, siyo sheria ya Katiba ya JMT, bali ni sheria inayotokana na "The Doctrine of the Law of Agency", na ni sheria ya kimataifa inayofanya kazi duniani kote na si Tanzania tu. Still zipo exceptions ambazo zinaweza zikapelekea wakala akawa liable kwa hatua alizochukua chini ya mkataba, pamoja na kuwa anakuwa amechukua hatua hizo kwa niaba ya Principal. Nimetaja hapo juu kipengele cha "Agency by Necessity" na ningependa kukitolea mfano katika hili.
Kuna wakala aliwahi kuwa liable kwa vitendo vyake na ilibidi amfidie principal. Kesi siikumbuki vizuri ni ya akina nani, lakini nitajaribu kulielezea tukio lenyewe kwa kina, na kabla ya kufanya hivyo, ningependa kutoa ufafanuzi mfupi namna ambavyo "Agency by Necessity" huwa inajitokeza.
Uwakala wa aina hii wa KULAZIMIKA KUWA WAKALA WA PRINCIPAL, wakati katika hali ya kawaida, wewe siyo wakala wake, huwa unasababishwa na mambo matatu makubwa. Wakala anakuwa katika hali ya kumiliki kitu chenye thanmani cha Principal, na katika mazingira ambayo hawezi kuwasiliana naye kabisa, lakini inatokea hali ambayo asipochukua hatua kuhusu kitu hicho (ambacho siyo chake), mwenye nacho atapata hasara, yaani Principal. Kwa hiyo uwakala wa aina hii huwa unatokea pale ambapo:
MOJA: Hakuna uwezekano wa mhusika (wakala) kuwasiliana na mwenye mali (Principal)
PILI: Inakuwa ni muhimu kwa wakala kuchukua hatua juu ya mali aliyonayo mikononi mwake, vinginevyo mwenye mali atapata hasara
TATU:Wakala anachukua hatua juu ya mali aliyonayo kwa nia njema na ya dhati kabisa, na isiyoweza kutiliwa mashaka na mtu mwingine yeyote yule mwenye nia njema.
Sasa tukirudi kwenye mada.Kuna kesi moja iliwahi kujitokeza. Ni kwamba mmiliki wa meli alikuwa anasafirisha ngozi za mteja kutoka Magogoni kwenda Kigamboni. Mwenye meli hakuwa wakala wa mwenye mali, yaani hakuwa wakala wa mmiliki wa ngozi alizokuwa akizisafirisha. Mwenye meli akiwa bado yuko njiani baharini, ikaonekana kuwa kule alikokuwa anazipeleka kuna vita imetokea na inaendelea, na hivyo meli haiwezi tena kwenda huko, na pia hapakuwa na uwezekano wa kuwasiliana na mwenye ngozi hizo.
Sasa katika kujaribu kuhakikikisha kuwa mwenye ngozi hapati hasara, mwenye meli akaamua kuziuza ngozi hizo, na baadaye mawasiliano yalipkuja kupatikana, akamjulisha mwenye mali na kumpatia fedha iliyopatikana kutokana na mauzo ya ngozi hizo. Baada ya hapo mwenye mali akaamua kwenda kumshitaki mahakamani mwenye meli, kuwa hakuridhika na kitendo kilichofanywa na mwenye meli.
Kesi ilipounguruma mahakamani,mahakama ikaona kuwa mwenye meli ana makosa kwa sababu pamoja na kwamba kule alikokuwa anaelekea kulikuwa na vita, na pia kuwa hapakuwa na uwezekano wa kuwasilian na mwenye ngozi, lakini BADO NGOZI HIZO KAMA ANGEZIFIFADHI VYEMA, HAZIKUWA NA UWEZEKANO WA KUOZA, NA HIVYO ALITAKIWA AKAE NAZO KWANZA AKISUBIRIA MAWASILIANO YAPATIKANE ILI AWEZE KUMJULISHA MWENYE NAZO ILI AWEZE KUAMUA NINI CHA KUFANYA.
Kwa hiyo mwenye meli ilibidi alipe DAMAGES kwa mmiliki wa ngozi. Hii kesi sikumbuki ni ya akina nani kwa sababu ni siku nyingi.
HITIMISHO;
Huu mfano hauhusiana sana na swala lililokuwa likijadiliwa kwenye Kipima Joto lakini ninachotaka kuonyesha hapa ni kuwa, Doctrine ya Law of Agency haijasema kuwa WAKALA ATAKUWA HANA KABISA LIABILITY, isipokuwa kuna exceptional cases zinazoweza kunfanya wakala akawa LIABLE KWA PRINCIPAL, na haijalishi ni wakala wa aina gani, maana hata mawakala nao wapo wa aina nyingi, waliosoma LAW OF AGENCY wanawajua.
Kwa hiyo nia yangu hapa ilikuwa ni kuwaondoa wasiwasi mawakala wa sekta binafsi kuwa TASAC kiutendaji anakuwa governed na The doctrine of law of Agency ambayo si sheria ya JMT. Wataalamu wa sheria watanirekebisha katika hili. Lakini still, hata kama kweli hali ingekuwa iko hivyo kwamba TASAC hayuko liable kwa lolote, sasa wakala mwenzako kama anakataa kuwa na liability si ndiyo anakupa nafasi nzuri zaidi wewe kwa sababu PRINCIPALS wata-tend kumuogopa na kumkimbia, watakimbilia kwako? Au nakosea? Tulisoma zamani haya mambo, enzi za ujana wetu!
Kitu kilichonivutia kwenye mjadala huu ni baada ya mawakala kutoka sekta binafsi kutoa malalamiko yao kuwa TASAC ameamua kuwa wakala lakini akaweka sheria kuwa yeye hatakuwa na LIABILITY kutoka kwa PRINCIPALS wake. Mimi hiki kitu kilinichanganya kidogo kwa sababu kadhaa kama nitakavyoeleza hapa chini,na kabla ya kwenda mbali zaidi, naomba ni-dikilee interest kuwa NIMESOMA LAW OF AGENCY (kikiwemo kipengele cha AGENCY BY NECESSITY), pamoja na SALE OF GOODS CONTRACT. Hizi sheria mbili nimezisoma na ninazielewa kwa kiasi, japo siyo sana.
Ni kwamba AGENT kutokuwa na LIABILITY kwa principal wake, siyo sheria ya Katiba ya JMT, bali ni sheria inayotokana na "The Doctrine of the Law of Agency", na ni sheria ya kimataifa inayofanya kazi duniani kote na si Tanzania tu. Still zipo exceptions ambazo zinaweza zikapelekea wakala akawa liable kwa hatua alizochukua chini ya mkataba, pamoja na kuwa anakuwa amechukua hatua hizo kwa niaba ya Principal. Nimetaja hapo juu kipengele cha "Agency by Necessity" na ningependa kukitolea mfano katika hili.
Kuna wakala aliwahi kuwa liable kwa vitendo vyake na ilibidi amfidie principal. Kesi siikumbuki vizuri ni ya akina nani, lakini nitajaribu kulielezea tukio lenyewe kwa kina, na kabla ya kufanya hivyo, ningependa kutoa ufafanuzi mfupi namna ambavyo "Agency by Necessity" huwa inajitokeza.
Uwakala wa aina hii wa KULAZIMIKA KUWA WAKALA WA PRINCIPAL, wakati katika hali ya kawaida, wewe siyo wakala wake, huwa unasababishwa na mambo matatu makubwa. Wakala anakuwa katika hali ya kumiliki kitu chenye thanmani cha Principal, na katika mazingira ambayo hawezi kuwasiliana naye kabisa, lakini inatokea hali ambayo asipochukua hatua kuhusu kitu hicho (ambacho siyo chake), mwenye nacho atapata hasara, yaani Principal. Kwa hiyo uwakala wa aina hii huwa unatokea pale ambapo:
MOJA: Hakuna uwezekano wa mhusika (wakala) kuwasiliana na mwenye mali (Principal)
PILI: Inakuwa ni muhimu kwa wakala kuchukua hatua juu ya mali aliyonayo mikononi mwake, vinginevyo mwenye mali atapata hasara
TATU:Wakala anachukua hatua juu ya mali aliyonayo kwa nia njema na ya dhati kabisa, na isiyoweza kutiliwa mashaka na mtu mwingine yeyote yule mwenye nia njema.
Sasa tukirudi kwenye mada.Kuna kesi moja iliwahi kujitokeza. Ni kwamba mmiliki wa meli alikuwa anasafirisha ngozi za mteja kutoka Magogoni kwenda Kigamboni. Mwenye meli hakuwa wakala wa mwenye mali, yaani hakuwa wakala wa mmiliki wa ngozi alizokuwa akizisafirisha. Mwenye meli akiwa bado yuko njiani baharini, ikaonekana kuwa kule alikokuwa anazipeleka kuna vita imetokea na inaendelea, na hivyo meli haiwezi tena kwenda huko, na pia hapakuwa na uwezekano wa kuwasiliana na mwenye ngozi hizo.
Sasa katika kujaribu kuhakikikisha kuwa mwenye ngozi hapati hasara, mwenye meli akaamua kuziuza ngozi hizo, na baadaye mawasiliano yalipkuja kupatikana, akamjulisha mwenye mali na kumpatia fedha iliyopatikana kutokana na mauzo ya ngozi hizo. Baada ya hapo mwenye mali akaamua kwenda kumshitaki mahakamani mwenye meli, kuwa hakuridhika na kitendo kilichofanywa na mwenye meli.
Kesi ilipounguruma mahakamani,mahakama ikaona kuwa mwenye meli ana makosa kwa sababu pamoja na kwamba kule alikokuwa anaelekea kulikuwa na vita, na pia kuwa hapakuwa na uwezekano wa kuwasilian na mwenye ngozi, lakini BADO NGOZI HIZO KAMA ANGEZIFIFADHI VYEMA, HAZIKUWA NA UWEZEKANO WA KUOZA, NA HIVYO ALITAKIWA AKAE NAZO KWANZA AKISUBIRIA MAWASILIANO YAPATIKANE ILI AWEZE KUMJULISHA MWENYE NAZO ILI AWEZE KUAMUA NINI CHA KUFANYA.
Kwa hiyo mwenye meli ilibidi alipe DAMAGES kwa mmiliki wa ngozi. Hii kesi sikumbuki ni ya akina nani kwa sababu ni siku nyingi.
HITIMISHO;
Huu mfano hauhusiana sana na swala lililokuwa likijadiliwa kwenye Kipima Joto lakini ninachotaka kuonyesha hapa ni kuwa, Doctrine ya Law of Agency haijasema kuwa WAKALA ATAKUWA HANA KABISA LIABILITY, isipokuwa kuna exceptional cases zinazoweza kunfanya wakala akawa LIABLE KWA PRINCIPAL, na haijalishi ni wakala wa aina gani, maana hata mawakala nao wapo wa aina nyingi, waliosoma LAW OF AGENCY wanawajua.
Kwa hiyo nia yangu hapa ilikuwa ni kuwaondoa wasiwasi mawakala wa sekta binafsi kuwa TASAC kiutendaji anakuwa governed na The doctrine of law of Agency ambayo si sheria ya JMT. Wataalamu wa sheria watanirekebisha katika hili. Lakini still, hata kama kweli hali ingekuwa iko hivyo kwamba TASAC hayuko liable kwa lolote, sasa wakala mwenzako kama anakataa kuwa na liability si ndiyo anakupa nafasi nzuri zaidi wewe kwa sababu PRINCIPALS wata-tend kumuogopa na kumkimbia, watakimbilia kwako? Au nakosea? Tulisoma zamani haya mambo, enzi za ujana wetu!