Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
Mkasa : NILIVUNJA NDOA ZANGU 3 KULIPIZA KISASI
Mwandishi: IRENE MBOWE (Irene Mbowe Kungwi Lao)
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
KISA CHA UKWELI ANACHOSIMULIA CHARLOTE, ANASEMA HIVI, MAJIBU YA MAMA WA HAWARA WA MUME WANGU YALIVYOSABABISHA NIKAVUNJA NDOA TATU.
Charlote, mwanamke aliyeishi kwenye ndoa yake kwa miaka 5. lakini baada ya kukutana na changamoto za ndoa ambazo alishindwa kuzivumilia na kujikuta kuwa na kisasi rohoni, Sasa aliamua kulipiza kisasi hicho na kupelekea kuvunja ndoa tatu. Hembu msikilize Charlote anachokisimulia. Hii inaweza kukusaidia sana katika maisha yako kutokuwa na kisasi moyoni.
SEHEMU YA 1: KUPENDWA RAHA
PART 1
Nimelelewa kwenye mazingira ya maisha ya utulivu na amani. Wazazi wangu walipendana na kuheshimiana sana. Na kutufanya sisi watoto wote kuwa na heshima na kupendana . lakini pia kujali jamii iliyotuzunguka na kuishi kwa adabu sana.
Nilipata bahati ya kupata elimu nzuri na ya viwango. Wazazi wetu walitusomesha, tena shule zenye hadhi na gharama kubwa mno.
Nikiwa kidato cha pili , Mtoto wa mzee ambaye ni family friend na sisi aliingia kidato cha tano katika shule niliyosoma. Hivyo kijana huyu Jones tuliheshimiana sana. Alinipenda na nilimpenda wote tulipendana na kuhurumiana na kuheshimiana.
Wengi shuleni walijua sisi ni family friends, na hivyo kila mmoja ni kama alikuwa akimchunga mwenzake. Jones aliogopa kufanya upuuzi akiamini ni lazima ningemsemea nyumbani, lakini na mimi pia niliogopa kufanya upuuzi nikiamini kabisa jones angenisema Nyumbani.
Hivyo Jones na mimi tukajulikana kama wana ndugu haswa haswa, na heshima ikawepo. Sikuwa na utani wala mizaha na watoto wa kiume.. hii ni kwa Vile Jones alikuwa akinifuatilia sana. Lakini na mimi nilimfuatilia sana kuhusu kuwa na mazoea na mabinti na hivyo aliogopa pia nay eye.
Wengi walisema Jones na Charlote ni ndugu. Wengi wa vijana walimtania Jones na kumwambia mwenye dada hakosi shemeji. Na Jones alichukia sana.
Tuliendelea kupendana sana.
Baada ya kumaliza masomo ya Secondary Jones alienda kujiunga na chuo wakati mimi nikiendelea na masomo ya Secondary. Lakini tuliendelea kuwasiliana sana. Na hatukutupana hata kidogo.
Alinipenda na kunikumbuka kila mara.
Nilipomaliza kidato cha sita, yeye tayari alikuwa ameshaanza kazi ya kuajiriwa.
Na sasa nilikuwa najiandaa na mimi kuanza chuo.
Nakumbuka siku moja alinipigia simu na kunitaka tukutane tuzungumze. Wana familia walijua urafiki wangu na Jones. Hakuna aliyekuwa na mashaka juu ya urafiki wetu. Kila mmoja alitupenda na kutufurahia kwa urafiki wetu.
Nilimpa ahadi Jones ya kukutana na mimi. Kwanza nilishangaa sana kwa namna ambavyo alikuwa kabadilika. Alikuwa kanawiri sana, kawa na hali ya utu uzima zaidi na pia alionekana ni kijana ambaye alikuwa na pesa.
Tulikutana na kukaa mahali kwa ajili ya kuzungumza.
Kitu cha kwanza aliniuliza …
Charlote,,, je una rafiki ama mpenzi?
Mwandishi: IRENE MBOWE (Irene Mbowe Kungwi Lao)
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
KISA CHA UKWELI ANACHOSIMULIA CHARLOTE, ANASEMA HIVI, MAJIBU YA MAMA WA HAWARA WA MUME WANGU YALIVYOSABABISHA NIKAVUNJA NDOA TATU.
Charlote, mwanamke aliyeishi kwenye ndoa yake kwa miaka 5. lakini baada ya kukutana na changamoto za ndoa ambazo alishindwa kuzivumilia na kujikuta kuwa na kisasi rohoni, Sasa aliamua kulipiza kisasi hicho na kupelekea kuvunja ndoa tatu. Hembu msikilize Charlote anachokisimulia. Hii inaweza kukusaidia sana katika maisha yako kutokuwa na kisasi moyoni.
SEHEMU YA 1: KUPENDWA RAHA
PART 1
Nimelelewa kwenye mazingira ya maisha ya utulivu na amani. Wazazi wangu walipendana na kuheshimiana sana. Na kutufanya sisi watoto wote kuwa na heshima na kupendana . lakini pia kujali jamii iliyotuzunguka na kuishi kwa adabu sana.
Nilipata bahati ya kupata elimu nzuri na ya viwango. Wazazi wetu walitusomesha, tena shule zenye hadhi na gharama kubwa mno.
Nikiwa kidato cha pili , Mtoto wa mzee ambaye ni family friend na sisi aliingia kidato cha tano katika shule niliyosoma. Hivyo kijana huyu Jones tuliheshimiana sana. Alinipenda na nilimpenda wote tulipendana na kuhurumiana na kuheshimiana.
Wengi shuleni walijua sisi ni family friends, na hivyo kila mmoja ni kama alikuwa akimchunga mwenzake. Jones aliogopa kufanya upuuzi akiamini ni lazima ningemsemea nyumbani, lakini na mimi pia niliogopa kufanya upuuzi nikiamini kabisa jones angenisema Nyumbani.
Hivyo Jones na mimi tukajulikana kama wana ndugu haswa haswa, na heshima ikawepo. Sikuwa na utani wala mizaha na watoto wa kiume.. hii ni kwa Vile Jones alikuwa akinifuatilia sana. Lakini na mimi nilimfuatilia sana kuhusu kuwa na mazoea na mabinti na hivyo aliogopa pia nay eye.
Wengi walisema Jones na Charlote ni ndugu. Wengi wa vijana walimtania Jones na kumwambia mwenye dada hakosi shemeji. Na Jones alichukia sana.
Tuliendelea kupendana sana.
Baada ya kumaliza masomo ya Secondary Jones alienda kujiunga na chuo wakati mimi nikiendelea na masomo ya Secondary. Lakini tuliendelea kuwasiliana sana. Na hatukutupana hata kidogo.
Alinipenda na kunikumbuka kila mara.
Nilipomaliza kidato cha sita, yeye tayari alikuwa ameshaanza kazi ya kuajiriwa.
Na sasa nilikuwa najiandaa na mimi kuanza chuo.
Nakumbuka siku moja alinipigia simu na kunitaka tukutane tuzungumze. Wana familia walijua urafiki wangu na Jones. Hakuna aliyekuwa na mashaka juu ya urafiki wetu. Kila mmoja alitupenda na kutufurahia kwa urafiki wetu.
Nilimpa ahadi Jones ya kukutana na mimi. Kwanza nilishangaa sana kwa namna ambavyo alikuwa kabadilika. Alikuwa kanawiri sana, kawa na hali ya utu uzima zaidi na pia alionekana ni kijana ambaye alikuwa na pesa.
Tulikutana na kukaa mahali kwa ajili ya kuzungumza.
Kitu cha kwanza aliniuliza …
Charlote,,, je una rafiki ama mpenzi?