Nilitegemea aseme medical attendant asifanye kazi ya Nurse na si kumzuia Nurse kuuza dawa

Mechanist

JF-Expert Member
Jan 31, 2015
724
491
Hii nchi ya ajabu sana, eti unazuia nurse asiuze dawa meanwhile unaruhusu medical attendant aendelee kufanya kazi za nurse wakati hajasoma nursing! Halafu kuna watu wanakurupuka na kusifu ati hiyo ni kazi ya mfamasia! Hamjui madaktari, manesi na wafamasia wote husoma clinical pharmacology? Hamjui kuwa Nurse ana exposure na cases nyingi na hivyo anaweza uza dawa bila kuathiri afya za watumiaji? Kwa leo yangu ni hayo tu, kila siku mimi naona maajabu nji hii.
 
Vitu vingine ni vya kuwazika tu. Maduka ya vijijini huko huyo mfamasia utampata wapi?
Halafu unakuta medical attendant anafanya kazi ya Nurse! Hilo hawataki kulisema coz wananchi wengi hawana elimu na hawajui kuwa wale si nurses coz wengi wao wanatumia uzoefu na wanafanya vizuri but they are not licensed to act as nurses
 
Wewe sijui umefikaje chuo!! Pharmacology yenu mnayo soma semester tatu ni ya kwenu pamoja na hayo tukija kwenye clinical pharmacology hata na ninyi mnaoma semester moja kama sisi
Nashindwa nikuambieje, ila nakuhurumia sana.

Kusoma kwako Clinical pharmacology kwa semister moja haina tofauti na kusoma anatomy semister moja ambayo MD nayo wanaisoma.

Kwa mantiki hiyo huwezi kufanana na hicho unachokilalamikia.
 
Nashindwa nikuambieje, ila nakuhurumia sana.

Kusoma kwako Clinical pharmacology kwa semister moja haina tofauti na kusoma anatomy semister moja ambayo MD nayo wanaisoma.

Kwa mantiki hiyo huwezi kufanana na hicho unachokilalamikia.
Kwa hiyo unaungana na wenye mawazo madogo kuwa kuuza dawa ni Kazi ya mfamasia? Hivi ukiwa mfamasia unakuwa muuza dawa? Kama wewe ni mfamasia basi unawaaibisha wafamasia
 
Hii nchi ya ajabu sana, eti unazuia nurse asiuze dawa meanwhile unaruhusu medical attendant aendelee kufanya kazi za nurse wakati hajasoma nursing! Halafu kuna watu wanakurupuka na kusifu ati hiyo ni kazi ya mfamasia! Hamjui madaktari, manesi na wafamasia wote husoma clinical pharmacology? Hamjui kuwa Nurse ana exposure na cases nyingi na hivyo anaweza uza dawa bila kuathiri afya za watumiaji? Kwa leo yangu ni hayo tu, kila siku mimi naona maajabu nji hii.
Cjawah kusoma ufamasia, unesi, wala udaktari, (nachojua ni biology na chemistry) lkn nimeuza duka la dawa muhimu kwa muda mrefu kiasi cha kuitwa Dokta kwa ufanisi wa kazi niliyokuwa nafanya. Nazijua dawa , najua kusoma doctors' prescription na kutoa dozi kwa usahihi na ushauri kwa mgonjwa. Haya matamko nayo!
 
Watanzania tumezoea kupindisha pindisha.Kama pharm assistants wapo wengi tu kwanini hao attendants wauze dawa hapo?

Kila siku tunalia na irrational use of medicine na kuongezeka kwa usugu wa dawa ila waziri kaona kazi ifanywe na waliosomea bado tunalalamika

Kusoma kwangu Procurement and Supplies hakunifanyi niwe Afisa Ugavi maana wapo waliosoma miaka yao yote kwenye ugavi

Tuheshimu mgawanyo wa kazi
 
Unaposema wafamasia in layman language means all pharmaceutical carde. Labda waziri kajiandaa kuajiri hawa watu in huge amount. Hoping for the best
Kila mtu afanye alichosomea huu mtindo wa manesi na madaktari kupenda sana kazi ya kutunza dawa na kuwapatia wagonjwa unakwenda kukoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kama nurse au doctor wamesoma clinical pharmacology na wanauwezo wa kutoa dawa
je hii taaluma ya pharmacy iliwekwa kwa lengo gani? au niseme mpharmasia ana role gani kwenye kitengo chake?
ni makosa makubwa tu kwa nurse kujikita kutoa dawa kwa kigezo cha uzoefu wa kazi, pharmacology anayoisoma nurse darasa ni ya kiwango kidogo sana cha kuzielewa dawa tu lakini sio kazi yake ku prescribe au kutoa kwa mgonjwa
nina ndugu yangu mmoja yeye ni doctor MD alitaka kufungua pharmacy yake kwa kigezo cha udokta wake bila kuweka tafuta mpharmasia, mission yake ilifeli kwa kubanwa na sheria za pharmacy
hiyo story ya doctor hapo inaonesha umuhimu wa mpharmasia, inshort tueshimu vitengo vya kila kazi sio kuvamia majukumu yasiyo kuhusu kisa unauzoefu na kazi

NB; dawa sio pipi zile useme unatoa tu kama mangi anavyo toa bazoka dukani
 
Clinical pharmacology ya semister moja utalinganisha vipi na mfamasia aliyesoma pharmacology kwa semister tatu?
Wewe utakuwa na diploma ya pharmacy, nenda kauze dawa. Kama utakuwa na degree ya pharmacy basi kafanye kazi ya maana. Bahati nzuri mimi sijawahi kusoma diploma
 
Ni maajabu makubwa kumzuia nurse asi dispense madawa kwenye maduka ya madawa wakati mahospitalini manesi ndio huwagawia wagonjwa wote dawa kama jinsi zilivyoandikwa na clinician.

Basi ni hivi kama manesi hawahusiki na madawa basi hao mapharmasia wawe mawodini wanawapa wagonjwa dawa alafu kazi ya nurse iwe kukaa tu kustarehe mahodini maana kama ni maswala ya usafi wapo ma medical attendant hivyo kumbe nurse kwa TZ hana kazi ya kufanya.

Kweli hii nchi haiishi vituko. Eti nurse na waganga hawana ruhusa ya kumpa mtu dawa kwenye maduka lakini mtu aliyetokea mtaani akaenda fundishwa na mapharmasia kwa muda wa mwezi mmoja eti anamamlaka ya kutoa dawa, anapewa cheti na na koti la TFDA hiki ni kituko.

Alafu nyinyi mapharmasia msijifanye wajuaji sana hata nyinyi hamna mamlaka ya kuwaandikia wagonjwa dawa, mwenye mamlaka hayo ni mganga wala nyinyi hamna jeuri ya kumpangia mganga aandike dawa ipi na dozi gani kwa mgonjwa lakini kwenye maduka yenu mnamazoea ya kuwapa wagonjwa madawa pila kuwa na prescription ya kutoka kwa mganga hilo ni kosa la jinai.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa mm sioni tatizo. Waziri alichokisema nakiunga mkono asilimia mia. Kwanza wanawatesa sana nurses kwa kuwatumia kwenye maduka ya dawa ya hospital wakati wodi za wazazi hazina manurse wakutokosha. Hii iwe ni sawa kwa isivyowezekana nurse kukaa kwenye chumba cha daktari na kumsikiliza mgonjwa. Nurse afanye kazi za unurse na pharmasia afanye kazi yake.
 
Nurses wanasoma drug administration, kama wamewazuia basi wafute na topic ya drug administration ili mafamasia wawe wanagawa dawa mawodini na dirishani, nurse abaki na majukumu mengine

_ where ever you are remember me_
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom