Elections 2010 Nilitamani kupiga Kura leo, lakini...

Mundu

JF-Expert Member
Sep 26, 2008
2,707
638
Ninasikitika kwa kutokuweza kutumia haki yangu ya kuchagua viongozi wangu leo. Nilijiandikisha kupiga kura, nilihakiki jina langu kwenye tovuti ya NEC, bahati mbaya nimepata safari ya ghafla ya kikazi. Nipo nje ya nchi. Najua kuna watanzania wengi leo ambao hawataweza kupiga kura kwa sababu mbali mbali. Sote, nami kwa niaba yao, nawatakia uchaguzi mwema.
 
Ninasikitika kwa kutokuweza kutumia haki yangu ya kuchagua viongozi wangu leo. Nilijiandikisha kupiga kura, nilihakiki jina langu kwenye tovuti ya NEC, bahati mbaya nimepata safari ya ghafla ya kikazi. Nipo nje ya nchi. Najua kuna watanzania wengi leo ambao hawataweza kupiga kura kwa sababu mbali mbali. Sote, nami kwa niaba yao, nawatakia uchaguzi mwema.

tupo pamoja mkuu...lakini najua watanzania hawatafanya kosa.....mimi familia yangu yote imeniwakilisha.......:peace:
 
tupo pamoja mkuu...lakini najua watanzania hawatafanya kosa.....mimi familia yangu yote imeniwakilisha.......:peace:
Nashukuru kwa hilo Preta, nami nimeshaamsha familia yangu, ndio wako kituoni saa hii.
 
kuna haja ya kuwa na kipindi cha early voting kama inavyofanywa nchi nyengine...............though nikifikiria kwa undani naona hapo ndo watakapopata chance ya kuchakachua
 
Nikisoma thread yako naelewa kuwa wewe tayari umeshabadilika kimawazo na kukombolewa, hilo tu linanipa faraja, hata kama haupo nyumbani!...

Cha msingi ni mbegu ya fikra mpa inayoendelea kukua katika ubongo wako, hiyo ndiyo mtaji wa maendeleo kwa nchi...

Kama umekosa sasa hivi, naamini 2015 utakuwepo, na tutakuhitaji zaidi muda huo.
Safari njema, tunachoomba ni sala zako!
 
kuna haja ya kuwa na kipindi cha early voting kama inavyofanywa nchi nyengine...............though nikifikiria kwa undani naona hapo ndo watakapopata chance ya kuchakachua

advance voting ni nzuri sana ila sisi hatuna miundombinu ya kuhakikisha utakatifu wa kura hizo unalindwa kwa uaminifu ulionyooka. Ila sitashangaa wazo hilo likipata upinzani na kudaiwa kuwa unaletwa umarekani
 
kuna haja ya kuwa na kipindi cha early voting kama inavyofanywa nchi nyengine...............though nikifikiria kwa undani naona hapo ndo watakapopata chance ya kuchakachua

Ni kweli nchi zilizoendelea kama Austria, Germany, New Zealand, Canada na US, wana utaratibu huu wa "early voting" kwa watu ambao hawatakuwepo katika nchi yao, au kwa namna moja au nyingine wapo nchini lakini kwa sababu mbalimbali kama ugonjwa nk, hawatafanikiwa kufika vituoni.
Kwa muelekeo wa uchaguzi wa mwaka huu, kama tungetumia system hii; nahisi jamaa wangechakachua ile mbaya. Hali ni tata mno kwao.
 
Nikisoma thread yako naelewa kuwa wewe tayari umeshabadilika kimawazo na kukombolewa, hilo tu linanipa faraja, hata kama haupo nyumbani!...

Cha msingi ni mbegu ya fikra mpa inayoendelea kukua katika ubongo wako, hiyo ndiyo mtaji wa maendeleo kwa nchi...

Kama umekosa sasa hivi, naamini 2015 utakuwepo, na tutakuhitaji zaidi muda huo.
Safari njema, tunachoomba ni sala zako!

Hata wewe nahisi una fikra na mtazamo wa ukombozi. Sala zangu ni kwa nchi yangu leo. Tusisahau kuwaombea Twiga Stars pia leo. Wana kipute na Banyanya Banyana kule Bondeni.
Wao pia nina uhakika waliitamani siku hii ya leo, wawepo nyumbani ili kufanya mabadiliko.
Mungu Ibariki Tanzania.
 
Mbatia mgombea ubunge jimbo la kawe hajapiga kura source ITV sasa hivi alikuwa anahojiwa,pia ameonyesha kadi moja feki ambayo haina picha.
 
Ninasikitika kwa kutokuweza kutumia haki yangu ya kuchagua viongozi wangu leo. Nilijiandikisha kupiga kura, nilihakiki jina langu kwenye tovuti ya NEC, bahati mbaya nimepata safari ya ghafla ya kikazi. Nipo nje ya nchi. Najua kuna watanzania wengi leo ambao hawataweza kupiga kura kwa sababu mbali mbali. Sote, nami kwa niaba yao, nawatakia uchaguzi mwema.

Pole sana, kama unamchagua Dr Slaa, nakushauri washawishi watu wasiopungua 10 kumpigia Dr Slaa na CHADEMA. hivyo utakuwa umeshiriki nasi vizuri.
 
Back
Top Bottom