Nilistuka kumuona nyoka yuko ndani kwangu, pembeni ya mlango wa kutokea nje!

Naona kama unataka kuingiza imani zetu kwny hili...kama nje kuna unyevu basi nyoka lazima atafute sehem yenye joto


Muhimu ni kuondoa vichaka nje ya nyumba yako
Ahsante kwa ushauri, ila hakuna vichaka but kuna maua mengi yawezekana ikawa ni sababu. Ahsante nitazingatia ushauri wako
 
Heri ya mwezi mpya wa Novemba, 2017 wanajf.

Jana muda wa saa mbili usiku nilistuka kumuona nyoka yuko ndani kwangu, pembeni ya mlango wa kutokea nje!

Nyoka wa kimo cha kati, mweusi.

Nimeshangaa amepitia wapi na hali milango imefungwa, amewezaje kupita kwenye vigae na hali vigae vinateleza.

Niliogopa na hata kuchanganyikiwa!

Mungu mkubwa, ninaishi vizuri na majirani zangu waliweza kunisaidia kumuua!!!
Nimelala nastuka nastuka namuona kama vile ananipandia kitandani.

Naomba mnisaidie ushauri na kinga ya kuzuia huyo "ndudu" asiingie tena ndani na hali sioni sehemu ya kumuwezesha kupenya hadi ndani.
Daaah
 
aggyjay chini hakuna upenyo! ila mie kwa imani yangu ya kanisa katoliki nilichofanya nilinyunyizia maji ya Baraka nyumba nzima
basi kama hivyo.umefanya vema kumwaga maji ya baraka.

kikwetukwetu ukiona nyoka mweusi ujue ni ishara ya msiba au balaa .
ila usiyaamin na hayatakutokea.
 
Back
Top Bottom