Nilishangaa Waziri Mbarawa kutumia muda mwingi kuelezea mradi ambao watanzania hawautaki

saigilomagema

JF-Expert Member
Jun 5, 2015
4,131
6,130
Jana wakati waziri wa ujenzi na uchukuzi anahitimisha hoja zake kimsing iangetueleza mpango wa kujenga barabara kuunganisha wilaya zetu na mikoa kuliko kuelezea mradi wa SGR. Huu mradi ni wazi watanzania wengi hawajaufurahia kwani hauwagusi watanzania wengi unapitia sehemu chache sana kulinganisha na ukubwa nchi yetu. Ushahidi ni kuwa ni km hakuna wabunge walioujadili, asilimia 96 walijadili barabara zilizo katika maeneo yao. Rais aliyejua mahitaji ya watanzania ni Jakaya Mrisho Kikwete. Mwaka 2010 alikuja na ajenda ya kuunganisha mikoa kupitia makao makuu ya mikoa. Vilevile aliunganisha nchi yetu na nchi za jirani kupitia mipaka yetu.

Kiukweli kwa mtazamo wangu matrilioni yaliyopelekwa kujenda SGR yangetumika kuunganisha wilaya zetu na kumalizia kuunganisha mikoa iliyobaki. Kwa mfano kwa mkoa wa Morogoro ijengwe barabara ya Ifakara-Kilombero-Mahenge-Malinyi-Mwaya na kuunganisha Morogoro - Songea na Njombe. Ijengwe Barabara ya Handeni-Kiteto-Kondoa. Same-Simanjiro-Arusha. Barabara ya Karatu-Mbulu-Haydom-Nduguti-Gumanga-Ibaga-Sibiti-Meatu-Lalago-Kolandoto na Lalago-Maswa. Barabara nyingine muhimu kama ya Karatu-Matala-Meatu. Barabara ya nafikiri Kilindi-Turiani-Dumila-Kilosa

Hii ni mifano michahe ninayoweza kuitoa. Hizi barabara zingegusa maisha ya watanzania moja kwa moja Tanzania yetu ingependeza sana. Matrilioni yanayotumika kujenga SGR yangeelekezwa ktk hizi na zingine zinazofanana na hizi.
 
Umetumwa na wamiliki wa Malori weye hivi mfano mizigo makontena 100 yavutwe na kichwa 1 Cha treni kutoka Dar Hadi labda Itigi Kisha Malori yapeleke huko wilayani huoni gharama kubwa inakuwa imeokolewa au Makonte yaende Hadi Mwanza hata mafuta yakisafurishwa Kwa Reli bei inapungua kuliko Kwa Njia ya barabara, duniani kote usafiri wa Reli ni WA nafuu zaidi
 
Umetumwa na wamiliki wa Malori weye hivi mfano mizigo makontena 100 yavutwe na kichwa 1 Cha treni kutoka Dar Hadi labda Itigi Kisha Malori yapeleke huko wilayani huoni gharama kubwa inakuwa imeokolewa au Makonte yaende Hadi Mwanza hata mafuta yakisafurishwa Kwa Reli bei inapungua kuliko Kwa Njia ya barabara, duniani kote usafiri wa Reli ni WA nafuu zaidi

Mkuu, ukijadiliana na watu wanaotumia emotions utachoshwa! Kama mradi huu unakosa pesa zote ningepeleka SGR hadi Manyoni (kuondoa congestion Dodoma) na kisha nikatoa SGR Dodoma mpaka Tunduma. Kosa ninaloliona kwa SGR ni kuipeleka Mwanza badala ya kusini ambako kuna Malawi, Zambia na super-rich DRC. Otherwise SGR si upotevu wa pesa kama mradi unakamilika on time and budget!
 
Mkuu, ukijadiliana na watu wanaotumia emotions utachoshwa! Kama mradi huu unakosa pesa zote ningepeleka SGR hadi Manyoni (kuondoa congestion Dodoma) na kisha nikatoa SGR Dodoma mpaka Tunduma. Kosa ninaloliona kwa SGR ni kuipeleka Mwanza badala ya kusini ambako kuna Malawi, Zambia na super-rich DRC. Otherwise SGR si upotevu wa pesa kama mradi unakamilika on time and budget!
Kule tuna Reli ya Tazara ambayo haitumiwi vema na nchi zetu za Zambia na Tanzania, huwa nasikitika kuona kijana hajui faida ya Reli
 
Kiukweli kwa mtazamo wangu matrilioni yaliyopelekwa kujenda SGR yangetumika kuunganisha wilaya zetu na kumalizia kuunganisha mikoa iliyobaki.
Umeshafanya hesabu za ulinganifu katika suala zima la kiuchumi ukaona faida ya kuunganisha barabara za wilaya kwa lami na SGR kuwa ni ipi inamzidi mwenzake ikiwa vitakamilika. Pia kipi kikianza kinaweza kusaidia kuleta kingine kwa urahisi. Halafu uje kwenye gharama za uendeshaji.

Kwa mfano kwa mkoa wa Morogoro ijengwe barabara ya Ifakara-Kilombero-Mahenge-Malinyi-Mwaya na kuunganisha Morogoro - Songea na Njombe.
Kwa huo mfano wako hii inaweza kuwa na tija gani kubwa ukilinganisha na SGR kwa ukamilifu wake.
 
Umetumwa na wamiliki wa Malori weye hivi mfano mizigo makontena 100 yavutwe na kichwa 1 Cha treni kutoka Dar Hadi labda Itigi Kisha Malori yapeleke huko wilayani huoni gharama kubwa inakuwa imeokolewa au Makonte yaende Hadi Mwanza hata mafuta yakisafurishwa Kwa Reli bei inapungua kuliko Kwa Njia ya barabara, duniani kote usafiri wa Reli ni WA nafuu zaidi
Huyu jamaa mleta hoja anasukumwa na mihemko ya kisiasa kuliko uhalisia wa mambo ulivyo.

Wala hajui faida za usafiri wa reli unavyoweza kudhibiti mfumko wa bei kutokana na urahisi wake.

Pia hajui kwamba SGR ni kitegauchumi kwa bandari yetu ta Dar es salaam kwenda nchi za maziwa makuu.

Yeye anamuwaza Riziwani na wabia wake wa Malori.
 
Jana wakati waziri wa ujenzi na uchukuzi anahitimisha hoja zake kimsing iangetueleza mpango wa kujenga barabara kuunganisha wilaya zetu na mikoa kuliko kuelezea mradi wa SGR. Huu mradi ni wazi watanzania wengi hawajaufurahia kwani hauwagusi watanzania wengi unapitia sehemu chache sana kulinganisha na ukubwa nchi yetu. Ushahidi ni kuwa ni km hakuna wabunge walioujadili, asilimia 96 walijadili barabara zilizo katika maeneo yao. Rais aliyejua mahitaji ya watanzania ni Jakaya Mrisho Kikwete. Mwaka 2010 alikuja na ajenda ya kuunganisha mikoa kupitia makao makuu ya mikoa. Vilevile aliunganisha nchi yetu na nchi za jirani kupitia mipaka yetu.

Kiukweli kwa mtazamo wangu matrilioni yaliyopelekwa kujenda SGR yangetumika kuunganisha wilaya zetu na kumalizia kuunganisha mikoa iliyobaki. Kwa mfano kwa mkoa wa Morogoro ijengwe barabara ya Ifakara-Kilombero-Mahenge-Malinyi-Mwaya na kuunganisha Morogoro - Songea na Njombe. Ijengwe Barabara ya Handeni-Kiteto-Kondoa. Same-Simanjiro-Arusha. Barabara ya Karatu-Mbulu-Haydom-Nduguti-Gumanga-Ibaga-Sibiti-Meatu-Lalago-Kolandoto na Lalago-Maswa. Barabara nyingine muhimu kama ya Karatu-Matala-Meatu. Barabara ya nafikiri Kilindi-Turiani-Dumila-Kilosa

Hii ni mifano michahe ninayoweza kuitoa. Hizi barabara zingegusa maisha ya watanzania moja kwa moja Tanzania yetu ingependeza sana. Matrilioni yanayotumika kujenga SGR yangeelekezwa ktk hizi na zingine zinazofanana na hizi.
Akili kubwa ni kuiharakisha hiyo reli ya SGR. Hii itasaidia hizo barabara kupata umuhimu na kurefusha uhai wake.
Rudi usome upya umuhimu wa reli kwenye uchumi wa nchi kama yetu! Wala huhitaji degree kuelewa!
Tanzania si kisiwa. Lazima iunganisbwe na mtandao wa biashara duniani.
Think Big!
 
SGR inapita katika mikoa 10. Kwa nini unaona haiwagusi watanzania wengi...!?
Imepitia Morogoro kwa mfano, kwani Ifakara, Kilombero, Mahenge, Malinyi, Turiani, Dumila na Kilosa Haviko Morogoro? Imepitia Singida je Nduguti, Itigi, Ibaga na Sibiti Haviko Singida? Itapitia Shinyanga na je Mhunze(Kishapu), Lalago, Sangamwalogesha haviko Shinyanga? Elewa Nachozungumzia ukiwa umetulia.
 
Imepitia Morogoro kwa mfano, kwani Ifakara, Kilombero, Mahenge, Malinyi, Turiani, Dumila na Kilosa Haviko Morogoro? Imepitia Singida je Nduguti, Itigi, Ibaga na Sibiti Haviko Singida? Itapitia Shinyanga na je Mhunze(Kishapu), Lalago, Sangamwalogesha haviko Shinyanga? Elewa Nachozungumzia ukiwa umetulia.
Ni ajabu kuwa wakoloni waliona mbali sana kuliko wewe.
Malori ya makontena na mizigo mizito inatakiwa kupita kwenye reli ikitoka au kwenda bandari. Fikra zako zijikite locally lakini uwaze kuunganisha hivyo vijiji na biashara ifanyikayo duniani kupitia bandari n.k
 
Kama wewe huitaki elezea nafsi yako SGR ili uilewe lazima uwe na upeo kuhusu uchumi na msitakabali wa nchi. Ila ukiwa mweupe huwezi kuielewa.
 
SGR inapita katika mikoa 10. Kwa nini unaona haiwagusi watanzania wengi...!?
SGR itachukua miaka 30 kukamilika na itatuacha na deni la trilioni 200,

Kama hicho kipande cha Dar hadi Moro hakijakamilika na ni mwaka wa 5 sasa, na deni la tifa ni trilioni 80 tayari, fikiria hadi mwanza itachukua muda gani na gharama kiasi gani

Ni mradi wa kipuuzi sana... afadhali hata tungejenga TAZARA tukarahisisha safari za Congo na Zambia
 
Umetumwa na wamiliki wa Malori weye hivi mfano mizigo makontena 100 yavutwe na kichwa 1 Cha treni kutoka Dar Hadi labda Itigi Kisha Malori yapeleke huko wilayani huoni gharama kubwa inakuwa imeokolewa au Makonte yaende Hadi Mwanza hata mafuta yakisafurishwa Kwa Reli bei inapungua kuliko Kwa Njia ya barabara, duniani kote usafiri wa Reli ni WA nafuu zaidi
Nakubaliana na wewe kwamba treni husaidia kusafirisha mizigo mikubwa.
Hata hivyo, kuna kitu ambacho hakipo sawa. Kwa nini hii reli ya meter gauge haifanyi hiyo kazi kwa sasa? Au hayo makonteina yatakuja ghafla baada ya SGR kukamilika?
Kama kutumia reli iliyokuwepo effectively and efficiently, kwa nini SGR isiwe hivyo hivyo?
 
Jana wakati waziri wa ujenzi na uchukuzi anahitimisha hoja zake kimsing iangetueleza mpango wa kujenga barabara kuunganisha wilaya zetu na mikoa kuliko kuelezea mradi wa SGR. Huu mradi ni wazi watanzania wengi hawajaufurahia kwani hauwagusi watanzania wengi unapitia sehemu chache sana kulinganisha na ukubwa nchi yetu. Ushahidi ni kuwa ni km hakuna wabunge walioujadili, asilimia 96 walijadili barabara zilizo katika maeneo yao. Rais aliyejua mahitaji ya watanzania ni Jakaya Mrisho Kikwete. Mwaka 2010 alikuja na ajenda ya kuunganisha mikoa kupitia makao makuu ya mikoa. Vilevile aliunganisha nchi yetu na nchi za jirani kupitia mipaka yetu.

Kiukweli kwa mtazamo wangu matrilioni yaliyopelekwa kujenda SGR yangetumika kuunganisha wilaya zetu na kumalizia kuunganisha mikoa iliyobaki. Kwa mfano kwa mkoa wa Morogoro ijengwe barabara ya Ifakara-Kilombero-Mahenge-Malinyi-Mwaya na kuunganisha Morogoro - Songea na Njombe. Ijengwe Barabara ya Handeni-Kiteto-Kondoa. Same-Simanjiro-Arusha. Barabara ya Karatu-Mbulu-Haydom-Nduguti-Gumanga-Ibaga-Sibiti-Meatu-Lalago-Kolandoto na Lalago-Maswa. Barabara nyingine muhimu kama ya Karatu-Matala-Meatu. Barabara ya nafikiri Kilindi-Turiani-Dumila-Kilosa

Hii ni mifano michahe ninayoweza kuitoa. Hizi barabara zingegusa maisha ya watanzania moja kwa moja Tanzania yetu ingependeza sana. Matrilioni yanayotumika kujenga SGR yangeelekezwa ktk hizi na zingine zinazofanana na hizi.


Yaani kama tukianza kujenga kwa kufurahisha watu tutaishia pabaya
 
Nakubaliana na wewe kwamba treni husaidia kusafirisha mizigo mikubwa.
Hata hivyo, kuna kitu ambacho hakipo sawa. Kwa nini hii reli ya meter gauge haifanyi hiyo kazi kwa sasa? Au hayo makonteina yatakuja ghafla baada ya SGR kukamilika?
Kama kutumia reli iliyokuwepo effectively and efficiently, kwa nini SGR isiwe hivyo hivyo?
Nakumbuka ilikuwa inafanya sana na hata Kuna kipindi walitangaza idadi ya metric tonne za mizigo walizosafirisha na ikionekana iliongezeka Kwa karibu 200%
 
Mleta mada nna uhakika umetumwa na wenzio,ila nna uhakika majibu ya hao watanzania waliowengi umeyaona yanataka nini kati ya bara bara na SGR kipi chenye kipaumbele?,Nadhani kama walikutuma uje kuandika hilo tangazo lako na hawajakupa Posho kwanza ukimaliza ndo waje wakulipe jioni ,chief hawatakulipa trust me mana umefail vibaya sana!!!!!
 
Back
Top Bottom