Nilipanga kusave laki 2, hatimaye nimesave laki 4 kwa mwezi. Nimefanikiwa kutumia Tsh 374,200/= kwa siku 28, ninaishi Geto.

Dx and Rx

JF-Expert Member
Jul 16, 2017
1,303
3,085
Mwezi uliopita nilisoma uzi humu ukielezea njia mbali mbali za kujiwekea akiba katika kipato anachopata mtu kwa kazi husika hasa kwa mwezi kama ilivyozoeleka kwa watu walioajiriwa.

Watu walifunguka kwa njia mbalimbali jinsi wanavyosave pesa zao za ujira baada ya mwezi, wengine wakasema wanatumia njia ya vibubu kusave na zinginezo.

Nilihamasika sana nikafikiria sana, kwa nini na mimi nisifanye hivyo...nikaangalia kipato changu ninachopata kwa kibarua changu, nikagundua ninaweza kusave laki 2 kwa mwezi(kwa makadirio ya chini).

Katika kufanikisha hilo nikaanza kucontrol kiasi cha matumizi kila siku, nikaanza kuandika kiasi cha hela kwa kila kitu ninachotumia, kila jioni nakokotoa jumla ya hela niliyoitumia kwa siku nzima na kuiandika kwenye doxc. Hapa kwenye doxc nimeamua kutumia soft copy, nimedownload App ya Microsoft Word ambayo naweza kuandika taarifa zote za matumizi(hii ndio njia bora zaidi kuliko diary/note book). Popote nikiwa kwenye mizunguko nikitumia hata Sh 100/= naingia kwenye file langu kwenye simu naiandika na kuisave.

Tangu nianze kutunza hizi kumbukumbu tarehe 22/3/2019, leo ni siku ya 28 na nimefanya mahesabu ya jumla nikakuta nimetumia jumla ya Tsh 374,200/= huku nikibakiwa na laki 4 kwenye account ambayo tayari imekutwa na kiasi kingine cha ujira.

Sasa najiwekea lengo la kusave laki 3 ili jumla iwe laki 7 baada ya mwezi kuisha(yaani kwa miezi 2 iwe jumla laki 7 niliyoisave), hapa malengo yangu ni kusave kwa muda wa miezi 10, endapo nikifanikiwa nitakuwa na jumla ya 3,000,000/=(kwa makadirio ya chini nikizingatia na Emmergency ambazo zinaweza kutokea), kwa kiasi hicho nitaweza kufungua kijiwe cha biashara yoyote nitakayoona inafaa.

Haya hapa chini ndio matumizi yangu ya muhimu na mara kwa mara:
1. Nauli(kwenda na kurudi kibaruani)
2. Nauli ya dogo(kwenda na kurudi shule), naishi na mdogo wangu namsomesha QT
3. Chakula cha mchana nikiwa kibaruani
4. Mahitaji madogo madogo kwa ajili ya chakula cha jioni
5. Vocha(2000/= kwa wiki)
6. Bili ya maji
7. Gesi(natumia mtungi mdogo, zaidi ya miezi 2)
8. Umeme(Luku)
9. Mengineyo kulingana jinsi yatakavyojitokeza kwa siku husika.

Nimeleta uzi huu kwa lengo la kupeana hamasa katika suala zima la kumanage hela.

NB: Mali bila daftari hupotea bila habari.


UPDATES 1.
Mungu ni mwema!

Kwa mara nyingine tena nimefanikiwa kusave laki 4, nimetumia TSh 591,300/= kwa siku 28.

UPDATES 2.
Mungu ni mwema!

Safari inaendelea, kwa mara nyingine tena nimefanikiwa kusave laki 4.

Kipindi hiki kilikuwa kigumu kidogo, nimetumia zaidi ya Laki 5 kwa matumizi mbalimbali.

Endapo nisingejikaza nisingeweza kusave kiasi nilichotaka maana ilihitaji kuwa na roho ya korosho sometimes..

UPDATES 3.

Ule msemo wa tumia pesa ikuzoee naona umepisha hodi hapa.

Kipindi hiki mambo yalikuwa mengi, nimejitahidi kusave Laki 1, chini ya lengo nililojiwekea lakusave angalau Laki 3.

Hakika hii safari ya saving inahitaji ujasiri mkubwa sana. Uvumilivu na kuweka tamaa pembeni ndio msingi wake

UPDATES 4.
Daaaahhh, pesa imekuwa tamu sana aisee kiasi kwamba hadi navunja kanuni niliyojiwekea.

Kipindi hiki nimefanikiwa kusave laki 1 na nusu, chini ya lengo la kusave angalau laki 3.

Nimegundua nikiendekeza ujinga siwezi kusogea hatua yoyote.

Kwa sasa nimepanga kusave laki 5 ili niweze kufidia magap ya nyuma. Endapo nikifuata mchanganuo huu lazima niweze kusave laki 5.

Mchanganuo:
Kwa siku natumia wastani wa Tsh 7,500/=

Kwa mwezi itakuwa 7,500 X 30 = 225,000/=.

Hii 7,500/= kwa siku afe kipa, afe beki tatu lazima niimaintain isizidi. Nimejaribu kuset nimeona kwa siku inakuwa chini ya 7,500/=, Hiyo inayobaki inakuwa akiba ya dharura ambapo naweza kutumia zaidi ya 7,500/=.

Kwa mwezi natenga 175,000/= kwa matumizi mengine kama vocha( 8,000/= kwa mwezi), Gesi, Unga wa kula na chochote kitakachotokea nje ya bajeti ya siku ambayo ni 7,500/=

UPDATES 5.
Nimesave laki 5 kutokana na kutekeleza mchanganuo niliouweka kwenye updates namba 4

NB: Msimamo, maamuzi sahihi, utekelezaji ndio mpango mzima.
 
Matumizi mengine hamishia huku.Maisha yenyewe mafupi ubahiri tu mwishowe upate ulcers bure sababu ya kushinda njaa


Mada maalumu ya walevi na wanywa pombe..
 
Hongera sana mkuu

You have done wonders

Familia zetu nyingi za kibongo hatukuzoeshwa utamaduni wa kujiwekea akiba pindi tunapoanza kupata vipato vyetu kwa ajili ya dharura na mambo mengine

Labda jambo moja ningekushauri, hiyo akiba uifungulie akaunti yake ya kujitegemea, usichanganye na hela ya matumizi ya kawaida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Matumizi mengine hamishia huku.Maisha yenyewe mafupi ubahiri tu mwishowe upate ulcers bure sababu ya kushinda njaa


Mada maalumu ya walevi na wanywa pombe..
aiseeee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maisha yako magumu Sana asee. Yaani huongi, huli bata, hununui pamba za gharama, hurembeshi geto, unaushije. Achana na kusevu tumia vikuzoee. Ujue duniani km mbinguni shauri yako
Mkuu sina haraka japo naona kama nimechelewa, pamba ninazo na nanunua zinazonipendeza, nakuwa nadhifu muda wote nikiwa kwenye mizunguko na kibaruani kama kawaida.

Kula bata sio lazima utume kiasi kikubwa cha fedha, unaweza ukala bata na ukaridhika kwa kiasi kidogo kikubwa tu upate unacbokipenda.

Geto naliremba mdogo mdogo japo sio priority sana, kwa sasa vitu vyenye thamani getoni ni PC, Kitanda, godoro, mtungi wa gesi, viti 3 vya kawaida na vyombo vya kawaida.

Huu msemo wa kusema tumia pesa ikuzoee hauko applicable kwa kila mtu, pesa inakuzoea kwa kadri unavyoitafuta nakuitumia kwa nidhamu
 
Mwezi uliopita nilisoma uzi humu ukielezea njia mbali mbali za kujiwekea akiba katika kipato anachopata mtu kwa kazi husika hasa kwa mwezi kama ilivyozoeleka kwa watu walioajiriwa.

Watu walifunguka kwa njia mbalimbali jinsi wanavyosave pesa zao za ujira baada ya mwezi, wengine wakasema wanatumia njia ya vibubu kusave na zinginezo.

Nilihamasika sana nikafikiria sana, kwa nini na mimi nisifanye hivyo...nikaangalia kipato changu ninachopata kwa kibarua changu, nikagundua ninaweza kusave laki 2 kwa mwezi(kwa makadirio ya chini).

Katika kufanikisha hilo nikaanza kucontrol kiasi cha matumizi kila siku, nikaanza kuandika kiasi cha hela kwa kila kitu ninachotumia, kila jioni nakokotoa jumla ya hela niliyoitumia kwa siku nzima na kuiandika kwenye doxc. Hapa kwenye doxc nimeamua kutumia soft copy, nimedownload App ya Microsoft Word ambayo naweza kuandika taarifa zote za matumizi(hii ndio njia bora zaidi kuliko diary/note book). Popote nikiwa kwenye mizunguko nikitumia hata Sh 100/= naingia kwenye file langu kwenye simu naiandika na kuisave.

Tangu nianze kutunza hizi kumbukumbu tarehe 22/3/2019, leo ni siku ya 28 na nimefanya mahesabu ya jumla nikakuta nimetumia jumla ya Tsh 374,200/= huku nikibakiwa na laki 4 kwenye account ambayo tayari imekutwa na kiasi kingine cha ujira.

Sasa najiwekea lengo la kusave laki 3 ili jumla iwe laki 7 baada ya mwezi kuisha(yaani kwa miezi 2 iwe jumla laki 7 niliyoisave), hapa malengo yangu ni kusave kwa muda wa miezi 10, endapo nikifanikiwa nitakuwa na jumla ya 3,000,000/=(kwa makadirio ya chini nikizingatia na Emmergency ambazo zinaweza kutokea), kwa kiasi hicho nitaweza kufungua kijiwe cha biashara yoyote nitakayoona inafaa.

Haya hapa chini ndio matumizi yangu ya muhimu na mara kwa mara:
1. Nauli(kwenda na kurudi kibaruani)
2. Nauli ya dogo(kwenda na kurudi shule), naishi na mdogo wangu namsomesha QT
3. Chakula cha mchana nikiwa kibaruani
4. Mahitaji madogo madogo kwa ajili ya chakula cha jioni
5. Vocha(2000/= kwa wiki)
6. Bili ya maji
7. Gesi(natumia mtungi mdogo, zaidi ya miezi 2)
8. Umeme(Luku)
9. Mengineyo kulingana jinsi yatakavyojitokeza kwa siku husika.

Nimeleta uzi huu kwa lengo la kupeana hamasa katika sula zima la kumanage hela.

NB: Mali bila daftari hupotea bila habari.
Pls naomba uweke hapa huo uzi na mimi nijifunze

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Matumizi mengine hamishia huku.Maisha yenyewe mafupi ubahiri tu mwishowe upate ulcers bure sababu ya kushinda njaa


Mada maalumu ya walevi na wanywa pombe..
Katika maisha yangu naomba isije ikatokee hata siku moja nikajiingiza kunywa pombe au kutumia aina yoyote ya kilevi. Ninyi endeleeni kulipa kodi kwa mtindo huo na mimi nitalipa kwa mtindo mwingine
 
Endelea kukomaa... baada ya hiyo miezi 10 usitumie zaidi ya nusu kuanzisha biashara, isimamie kwa ukaribu mpaka ikue, trust me later utakula bata zisizo na mawazo hata kidogo
Sawa mkuu, nikifanikiwa nitachukua kiasi kidogo cha kukiingiza kwenye mzunguko hata kama nikija kukwama nisije kuumia sana.

Kujaribu si kushindwa
 
Me nilisha shindwa ..maana jinsi navyopata zaidi ,ndio jinsi navyozidi kutumia

Nikiwa na laki mbili mfukoni ntatumia sana ,tofauti na nikiwa na 30,000 ila nayo ntaitumia.

Ushauri: tumia uwezavyo ukifa ya duniani huwezi yafahamu ,marehemu utazikwa ata na manispaa
 
Hongera sana mkuu


Labda jambo moja ningekushauri, hiyo akiba uifungulie akaunti yake ya kujitegemea, usichanganye na hela ya matumizi ya kawaida

Ahsante sana.

Hilo ndio nalifikiria nitafanya mchakato muda si mrefu ili niwe na hiyo account ya akiba
 
Back
Top Bottom