Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
NILIOA MWANAMKE KUMBE JINI - 2
Mikasa ya kusisimus
Kuanzia muda huo, tulianza kuongea mambo mengi, kwanza nilimfahamisha Sakina maisha yangu kuwa sijawahi kuoa na nimekuwa nikitafuta mwanamke wa maisha yangu kwa muda mrefu sasa, nilipomuona nilihisi angeweza kufungua milango ya ndoa na kuweza kumuingiza katika himaya ya penzi la kweli.
Azizi, kusema kweli kuzunguzia habari za kuoa au kuolewa...sitaki!
Kwanini?
Wanaume wamenitenda, napenda nibaki peke yangu...najua hata nikikubali leo unioe kesho na kesho-kutwa utaniacha...wanaume ndiyo zenu, Sakina alitokwa na maneno hayo alipogundua nimezama katika penzi zito nikiwa tayari kumuoa.
Sakina, wanaume wanatofautiana, niamini naweza kuwa mume bora...
Mmh! Minina wivu sana...halafu napenda mwanaume mwenye mapenzi ya kweli...
Hicho ndicho nitakachokupa, Sakina...
Hutaweza, hajanizoea...hujui naishi vipi, napenda kula chakula gani, napenda kunywa kinywaji gani na hata starehe yangu kubwa!
Vyote hivyo nitavifanya, nitakachokiona kibaya nitakuambia hakifai, lazima tueleweshane...
Nilishawahi kuolewa na mwarabu ndoa ikavunjika siku saba, naamini wanaume wakorofi bora nibaki peke yangu, baada ya kusema hayo, Sakina alinisogelea akaniegemea kifuani machozi yakimtoka! Hakika alilia kwa uchungu akiniomba nisimuoe maana nisingeweza kutii masharti yake.
Masharti gani?
Kuombea kaburi la mama yangu...lipo Lamu...
Unaliombea kwa njia gani?
Kwa kulipigia magoti nikiwa na sarafu za kuziweka juu ya kaburi lake...tena nyakati za usiku, lazima niamke na kwenda makaburini, maneno hayo kidogo yalianza kunitisha, sikutegemea msichana mdogo na mzuri kama huyo anaweza kuwa na roho ngumu ya kwenda makaburini usiku akatupa sarafu za pesa juu ya kaburi la mama yake na kumuomba.
Mbona leo upo huku, unaendaje kumuombea wakati umedai kila siku lazima uende makaburini?
Nikisafiri, huwa namuomba ruhusa...mizimu yake inaridhika... na safari yangu inakuwa salama, alisema akiendelea kulia, hakika nilichukua muda mrefu kumliwaza na kumuambia habari njema kuwa nimeteuliwa na Mungu kumtuliza moyo wake na kumfanya awe miongoni mwa wanawake bora duniani watakaoiona pepo ya Mungu, licha ya kumfariji nilishindwa kudhibiti hisia zangu juu yake na nilimpenda kuliko kawaida.
Sharti lingine mpenzi, kwa mara ya kwanza nikamuita Sakina mpenzi alipotulia kulia.
Kuoga baharini, napenda sana..., alisema akiniangalia kwa ukaribu, kuna wakati macho yake yalibadilika akatoa miwani na kuvaa sikuweza kujua alificha nini.
Mbona una vaa miwani?
Macho yanauma, alinitazama na macho yake makubwa yakulegea, akatembea huku nyuma anikiacha hoi! Nilisisimka mwili kutokana na makalio makubwa ya Sakina ambayo licha ya kuvaa jumba bado yalionekana ya yalizunguka taratibu kulingana na anavyotembea. Hatua tatu alisimama akanigeukia, alipovua miwani macho yake yalikuwa mazuri yakuvutia. Hapo nikazidi kumpenda na kumuona mwanamke wa maisha yangu, nilikuwa tayari kufanya jambo lolote mradi nifunge ndoa na Sakina.
Sakina nakupenda!
Ahsante, nakupenda pia...
Tuliongea mambo mengi, katika mazungumzo Sakina alidai kuna michezo mingi anayoipenda huenda nisingevutiwa nayo, nilimwambia nipo tayari kuridhia michezo yote aipendayo.
Napenda sana kuogelea baharini, hiyo ndiyo hobi yangu.
Usijali, kumbe kuoga maji ya baharini...usijali...ukiridhia kuolewa na mimi, nitakupa uhuru huo, nilimwambia.
Tuliongea mambo mengi, baadaye nikalipia chumba, nikamuomba akafahamu chumba changu, mwanzoni alisuasua akidai anaogopa kubakwa, nilipomhakikishia nisingeweza kumuingilia bila ridhaa yake aliridhia ndipo tukaingia chumbani.
Mwili mzima ulianza kutetemeka, vinyweleo navyo vilizidi kunisimama juu ya ngozi. Sikujali sana nilihisi huenda woga wangu wa kukutana na mwanamke mrembo wa maisha yangu.
Ajabu na nilivyotegemea, muda mfupi tulipoingia chumbani, Sakina alianza kulaumu anahisi joto kali hivyo akaomba apunguze nguo za juu, kauli hiyo kwangu iliangukia katika mapenzi. Nilipatwa na hisia huenda anataka kunizawadia chenye thamani kwa kila kiumbe anayehema.
Taratibu akavua nguo ya juu na kuitundika kwenye msumari wa kuwekea nguo mlangoni, kuona hatua hiyo nilifarijika moyoni nikitamani kuona akiendelea kuvua zote. Niliridhia kwa shangwe zote, mapigo ya moyo yakiongeza mwendo, kuona msichana huyu kwangu ilikuwa ushindi mtupu.
Miguu yake mweupe yenye umbo lenye kuvutia wanaume wengi ilizidi kunifanya nijione kiumbe mwenye bahati, pua yake yenye asili ya msomali hakika usingeweza kuamini kama mrembo huyo ni mchaga wa Machame kama alivyosema. Alikuwa mrefu wa futi sita, ngozi yake ilitawaliwa na manyoya mengi mpaka mashavuni. Nilitamani kumkumbatia nikaogopa kumuudhi, alionekana mpole mwenye kupenda kubembelezwa.
Sakina, nakupenda sana...
Najua, unanipenda kwa vile hujanijua...ukinijua utaniacha...
Kukujua kivipi? Nilihisi anazungumzia kumjua kimwili kisha kula kona.
Kunijua kiundani, nyie wanaume si mnapenda sana kudanganya wanawake kila siku...hivi mfano nikakupa mwili wangu leo, si utasema mimalaya na mpango wa kunioa ukaishia hapa hotelini?
Siko hivyo, Sakina...najua mwanamke thamani yako na fahamu sheria za mapenzi ya kweli kuwa haziangalii wapi mmekutana, saa ngapi, mavazi gani, dini, raia na rangi. Wapenzi wanapopenda hawataki kuangalia muda wa kukutana kwao, hivyo basi naomba ukinizawadia penzi lako leo siwezi kukuacha...
Akah! Nakupenda, kukupa leo hapana..., aliniambia, akanisogelea na kuketi jirani yangu, nilikuwa napata tabu ya ajabu, kila mara mapigo ya moyo yaliongeza kasi isiyo kawaida na kusisimka mwili mzima.
Nilitamani kumbaka nikahofia kuharibu mpango mzima.
Zaidi, Sakina wangu hakuwa mwanamke wa kubakwa alitakiwa kubembelezwa na kuridhia mwenyewe, hilo ndilo penzi bora na si kukwazana.
Jambo la msingi kichwani mwangu lilinijia, nilifungua kiyoyozi hali ya chumba ikawa baridi kali, Sakina akazidi kuhisi baridi na kuniambia nizime kiyoyozi, nilimjibu napenda kumpa joto langu la mwili hadi asuuzike na kufarijika. Kabla ya kujibu sweetie wangu huyo alicheka sana na kuniambia namlaghai kimapenzi.
Kweli, nipo tayari kukuoa...
Unaongea mdomoni!
No, kitokacho mdomoni kipo moyoni, niliongea nikimwangalia kwa mapenzi mazito.
Kama ndivyo, vua nguo zako zote tulale watupu bila kugusana hadi asubuhi, nitajua wewe mvumilivu..., aliniambia, kwangu ulikuwa mtihani mkubwa sana maana nilijujia nisingeweza kupatwa na usingizi kila nitakapouona mwili mlaini wenye kuvutia.
Kama mchezo wa kuigiza, niliridhia akaenda chumbani kwake ambapo alichukua begi akarejea akiwa amejipulizia manukato makali yaliyonifanya nipate tabu kuhema lakini kwasababu nilishazama kwenye penzi nilitulia bila kuonyesha kukerwa na harufu hiyo.
Tukaagiza chakula na kula pamoja. Sakina alibarikiwa kipaji cha kuongea na stori zake zilikuwa za starehe hasa kwenda fukwe za bahari ya Hindi ambapo ndipo anapopenda kufurahia maisha.
Je, Azizi ataweza kuvumilia? Usikose wiki ijayo.Kitabu changu cha Kiss, Hug & Love chenye Love Message nzuri na makala za mahaba na Kitchen Party Kipo mtaani nchi nzima kwa Tsh. 2500/=
Mikasa ya kusisimus
Kuanzia muda huo, tulianza kuongea mambo mengi, kwanza nilimfahamisha Sakina maisha yangu kuwa sijawahi kuoa na nimekuwa nikitafuta mwanamke wa maisha yangu kwa muda mrefu sasa, nilipomuona nilihisi angeweza kufungua milango ya ndoa na kuweza kumuingiza katika himaya ya penzi la kweli.
Azizi, kusema kweli kuzunguzia habari za kuoa au kuolewa...sitaki!
Kwanini?
Wanaume wamenitenda, napenda nibaki peke yangu...najua hata nikikubali leo unioe kesho na kesho-kutwa utaniacha...wanaume ndiyo zenu, Sakina alitokwa na maneno hayo alipogundua nimezama katika penzi zito nikiwa tayari kumuoa.
Sakina, wanaume wanatofautiana, niamini naweza kuwa mume bora...
Mmh! Minina wivu sana...halafu napenda mwanaume mwenye mapenzi ya kweli...
Hicho ndicho nitakachokupa, Sakina...
Hutaweza, hajanizoea...hujui naishi vipi, napenda kula chakula gani, napenda kunywa kinywaji gani na hata starehe yangu kubwa!
Vyote hivyo nitavifanya, nitakachokiona kibaya nitakuambia hakifai, lazima tueleweshane...
Nilishawahi kuolewa na mwarabu ndoa ikavunjika siku saba, naamini wanaume wakorofi bora nibaki peke yangu, baada ya kusema hayo, Sakina alinisogelea akaniegemea kifuani machozi yakimtoka! Hakika alilia kwa uchungu akiniomba nisimuoe maana nisingeweza kutii masharti yake.
Masharti gani?
Kuombea kaburi la mama yangu...lipo Lamu...
Unaliombea kwa njia gani?
Kwa kulipigia magoti nikiwa na sarafu za kuziweka juu ya kaburi lake...tena nyakati za usiku, lazima niamke na kwenda makaburini, maneno hayo kidogo yalianza kunitisha, sikutegemea msichana mdogo na mzuri kama huyo anaweza kuwa na roho ngumu ya kwenda makaburini usiku akatupa sarafu za pesa juu ya kaburi la mama yake na kumuomba.
Mbona leo upo huku, unaendaje kumuombea wakati umedai kila siku lazima uende makaburini?
Nikisafiri, huwa namuomba ruhusa...mizimu yake inaridhika... na safari yangu inakuwa salama, alisema akiendelea kulia, hakika nilichukua muda mrefu kumliwaza na kumuambia habari njema kuwa nimeteuliwa na Mungu kumtuliza moyo wake na kumfanya awe miongoni mwa wanawake bora duniani watakaoiona pepo ya Mungu, licha ya kumfariji nilishindwa kudhibiti hisia zangu juu yake na nilimpenda kuliko kawaida.
Sharti lingine mpenzi, kwa mara ya kwanza nikamuita Sakina mpenzi alipotulia kulia.
Kuoga baharini, napenda sana..., alisema akiniangalia kwa ukaribu, kuna wakati macho yake yalibadilika akatoa miwani na kuvaa sikuweza kujua alificha nini.
Mbona una vaa miwani?
Macho yanauma, alinitazama na macho yake makubwa yakulegea, akatembea huku nyuma anikiacha hoi! Nilisisimka mwili kutokana na makalio makubwa ya Sakina ambayo licha ya kuvaa jumba bado yalionekana ya yalizunguka taratibu kulingana na anavyotembea. Hatua tatu alisimama akanigeukia, alipovua miwani macho yake yalikuwa mazuri yakuvutia. Hapo nikazidi kumpenda na kumuona mwanamke wa maisha yangu, nilikuwa tayari kufanya jambo lolote mradi nifunge ndoa na Sakina.
Sakina nakupenda!
Ahsante, nakupenda pia...
Tuliongea mambo mengi, katika mazungumzo Sakina alidai kuna michezo mingi anayoipenda huenda nisingevutiwa nayo, nilimwambia nipo tayari kuridhia michezo yote aipendayo.
Napenda sana kuogelea baharini, hiyo ndiyo hobi yangu.
Usijali, kumbe kuoga maji ya baharini...usijali...ukiridhia kuolewa na mimi, nitakupa uhuru huo, nilimwambia.
Tuliongea mambo mengi, baadaye nikalipia chumba, nikamuomba akafahamu chumba changu, mwanzoni alisuasua akidai anaogopa kubakwa, nilipomhakikishia nisingeweza kumuingilia bila ridhaa yake aliridhia ndipo tukaingia chumbani.
Mwili mzima ulianza kutetemeka, vinyweleo navyo vilizidi kunisimama juu ya ngozi. Sikujali sana nilihisi huenda woga wangu wa kukutana na mwanamke mrembo wa maisha yangu.
Ajabu na nilivyotegemea, muda mfupi tulipoingia chumbani, Sakina alianza kulaumu anahisi joto kali hivyo akaomba apunguze nguo za juu, kauli hiyo kwangu iliangukia katika mapenzi. Nilipatwa na hisia huenda anataka kunizawadia chenye thamani kwa kila kiumbe anayehema.
Taratibu akavua nguo ya juu na kuitundika kwenye msumari wa kuwekea nguo mlangoni, kuona hatua hiyo nilifarijika moyoni nikitamani kuona akiendelea kuvua zote. Niliridhia kwa shangwe zote, mapigo ya moyo yakiongeza mwendo, kuona msichana huyu kwangu ilikuwa ushindi mtupu.
Miguu yake mweupe yenye umbo lenye kuvutia wanaume wengi ilizidi kunifanya nijione kiumbe mwenye bahati, pua yake yenye asili ya msomali hakika usingeweza kuamini kama mrembo huyo ni mchaga wa Machame kama alivyosema. Alikuwa mrefu wa futi sita, ngozi yake ilitawaliwa na manyoya mengi mpaka mashavuni. Nilitamani kumkumbatia nikaogopa kumuudhi, alionekana mpole mwenye kupenda kubembelezwa.
Sakina, nakupenda sana...
Najua, unanipenda kwa vile hujanijua...ukinijua utaniacha...
Kukujua kivipi? Nilihisi anazungumzia kumjua kimwili kisha kula kona.
Kunijua kiundani, nyie wanaume si mnapenda sana kudanganya wanawake kila siku...hivi mfano nikakupa mwili wangu leo, si utasema mimalaya na mpango wa kunioa ukaishia hapa hotelini?
Siko hivyo, Sakina...najua mwanamke thamani yako na fahamu sheria za mapenzi ya kweli kuwa haziangalii wapi mmekutana, saa ngapi, mavazi gani, dini, raia na rangi. Wapenzi wanapopenda hawataki kuangalia muda wa kukutana kwao, hivyo basi naomba ukinizawadia penzi lako leo siwezi kukuacha...
Akah! Nakupenda, kukupa leo hapana..., aliniambia, akanisogelea na kuketi jirani yangu, nilikuwa napata tabu ya ajabu, kila mara mapigo ya moyo yaliongeza kasi isiyo kawaida na kusisimka mwili mzima.
Nilitamani kumbaka nikahofia kuharibu mpango mzima.
Zaidi, Sakina wangu hakuwa mwanamke wa kubakwa alitakiwa kubembelezwa na kuridhia mwenyewe, hilo ndilo penzi bora na si kukwazana.
Jambo la msingi kichwani mwangu lilinijia, nilifungua kiyoyozi hali ya chumba ikawa baridi kali, Sakina akazidi kuhisi baridi na kuniambia nizime kiyoyozi, nilimjibu napenda kumpa joto langu la mwili hadi asuuzike na kufarijika. Kabla ya kujibu sweetie wangu huyo alicheka sana na kuniambia namlaghai kimapenzi.
Kweli, nipo tayari kukuoa...
Unaongea mdomoni!
No, kitokacho mdomoni kipo moyoni, niliongea nikimwangalia kwa mapenzi mazito.
Kama ndivyo, vua nguo zako zote tulale watupu bila kugusana hadi asubuhi, nitajua wewe mvumilivu..., aliniambia, kwangu ulikuwa mtihani mkubwa sana maana nilijujia nisingeweza kupatwa na usingizi kila nitakapouona mwili mlaini wenye kuvutia.
Kama mchezo wa kuigiza, niliridhia akaenda chumbani kwake ambapo alichukua begi akarejea akiwa amejipulizia manukato makali yaliyonifanya nipate tabu kuhema lakini kwasababu nilishazama kwenye penzi nilitulia bila kuonyesha kukerwa na harufu hiyo.
Tukaagiza chakula na kula pamoja. Sakina alibarikiwa kipaji cha kuongea na stori zake zilikuwa za starehe hasa kwenda fukwe za bahari ya Hindi ambapo ndipo anapopenda kufurahia maisha.
Je, Azizi ataweza kuvumilia? Usikose wiki ijayo.Kitabu changu cha Kiss, Hug & Love chenye Love Message nzuri na makala za mahaba na Kitchen Party Kipo mtaani nchi nzima kwa Tsh. 2500/=