Nimekuwa nifuatilia hoja mbalimbal kuhusu ombwe la uongozi lililo ndani ya CCM niakaamini kuwa hoja zilizokuwa zinatolewa zinamantiki kutokana na kauli za viongozi wengi wa CCM na maamuzi yao yanavyokinzana wao kwa wao hata na sheria za nchi. Mifano mizuri ni pale waziri mmoja anasema Dowans walipwe haraka, mwingine isilipwe hiyo ni mijizi, mwingine katiba iliyopo haina matatizo anaibuka mwingine ifanyiwe marekebisho.
Mwingine madiwani wa Arusha wamefukuzwa na chama chao anasema waendelee kulipwa posho na kuhudhuria mikutano. hayo ndio baadhi e hoja zilizoniaminisha kuwa CCM sasa hamnazo. Lakini wiki hii nzima hasa baada ya kuanza kampeni za Igunga nimeendelea kugundua na kuamini zaidi kuwa CCM kwa upande wa think tank KWISHENI kwa sababu zifutazo:
Mwingine madiwani wa Arusha wamefukuzwa na chama chao anasema waendelee kulipwa posho na kuhudhuria mikutano. hayo ndio baadhi e hoja zilizoniaminisha kuwa CCM sasa hamnazo. Lakini wiki hii nzima hasa baada ya kuanza kampeni za Igunga nimeendelea kugundua na kuamini zaidi kuwa CCM kwa upande wa think tank KWISHENI kwa sababu zifutazo:
- CCM Hawana tena ubunifu wamebakia kuwaiga CHADEMA- Chadema wamebuni kutumia helkopta katika kampeni CCM na CUF mwanzoni wakaponda walipoona maji ya shingo wakaingia wate kutumia helkopta, CCM kwisheni ubunifu.
- Wanaeneza maneno kwa wananchi kuwa CHADEMA wameleta magaidi kutoka Libya , Pakistani na kwingineko bila kufikiri kuwa kwa mtu mwenye akili za kawaida atajua kuwa huo ni uongo kwa kuwa wao ndio wenye serikali na jeshi lipo chini yao ingekuwa hivyo tayari baadhi ya watu wangekuwa wamekamatwa lakini kwa kutotambua kuwa Watanzania kwa sasa kuna wasomi wengi wameendela kutumia mtaji wa ujinga wa Watanzania.Kali zaidi ili pale leo hii waliposema CHADEMA wamepanga kujipaka rangi nyekundu ili kuwatisha akina mama, hizi ndizo mbinu gani jamani hata mtoto wa darasa la kwanza anajua huu ni uongo.