mtoto mdogo sana
JF-Expert Member
- Apr 16, 2020
- 460
- 1,337
Nimepanga kwenda beach yoyote siku ya tarehe 11 Desemba 2020, kwa ajili ya kwenda kutumia nusu siku kule nikilia machozi. Siku hiyo itakuwa siku moja baada ya sherehe za kutunukiwa degree pale mlimani City.
Maisha yangu Tangu nikiwa n miaka 9 hayajawahi kuwa ya kawaida. Sehemu kubwa ya Simulizi ya maisha yangu nimeshawahi kuisimulia humu kwenye nyuzi mbali mbali, kwa hiyo nimeona sio vyema kurudia tena. Ila sasa nasimulia maisha yangu baada ya kuzamia Mwanza nikiwa mtoto.
Sikuwa na baba wala mama, tangu nikiwa na miaka hiyo 9. Hivyo, kuna mengi yalitokea baada ya mama yangu kufariki ila kwa mbinde nilimaliza elimu ya msingi mwaka 2008 huko mkoa wa kaskazini magharibi mwa Tanzania.
Nilipata ufaulu mzuri sana wa alama zaidi ya 200 kati ya 250, ila sikuwa na mzazi wala ndugu yeyote. Hivyo sikupata bahati ya kusoma shule ya sekondari. Niliishi kichokoraa pale kijijini, msosi shida, sina hata nguo, halafu kuna dhana iliyojengeka kuwa mimi nilikuwa na mkosi. Kitendo cha kumpoteza mama yangu na kutokuwa na mtu wa ukoo wangu ilikuwa ni kiashiria cha mkosi. Kwamba kila nitakayekuwa karibu nae anaweza pia kufariki au kupata matatizo. Niliishi mpaka nilipopata wazo la kuzamia katika jiji la Mwanza nikatafute maisha.
Baada ya kupata nauli nilipanda gari kuelekea Mwanza. Tatizo likaja kuwa aliyenikatia tiketi alinipandisha gari lisiloenda Mwanza, ila akampa maelekezo kondakta kuwa aniache Runzewe kwa maagent wanifaulishe. Mimi sikuwa najua iwapo ni sahihi au sio. Nikivofika Runzewe nikapandishwa kwenye hiace inayofika geita na nikarudishiwa chenchi. Nilipewa elfu 7. Geita nilifika jioni sana. Sikuwa na pesa hivyo nikatafuta magari ya kwenda Mwanza jioni hiyo hiyo. Nikaambiwa hayapo muda huo. Ila kama nahitaji.. nichukue hiace/mchomoko niende mpaka Sengerema. Kwamba pale itakuwa rahisi kupata gari la kwenda kamanga kabla ya saa tano usiku ambapo ni mwisho wa kivuko.
Mimi sikuwa najua chochote. Nikafuata ushauri. Nikaenda mpaka Sengerema. Nilifika usiku sana.. takriban saa tano na nusu. Gari lilisimamishwa na trafiki muda mrefu njiani.. ndio sababu. Mpaka abiria wakaingilia kati ndio likaachiwa. Kwa watu wenyeji wa barabara hiyo nadhani wanaelewa upkiaji wa abiria kwny ile michomoko, hali ilikuwa tete. Sengerema nilifika nikawa sina ramani. Nilikuwa sipajui, pia gari halikutushushia stendi kwa kuwa ilikuwa usiku. Nikapata wazo.. nitafute sehemu nikae mpaka asubuhi ndio niingie Mwanza. Wakati huo nilikuwa hata sijui ni kitu gani naenda kukifanya Mwanza. Ila niliamini naenda kufanikiwa.
Nilikuwa mdogo sana ila shida nilizopitia tangu utotoni kushinda porini nikichunga mbuzi, kushinda njaa, kulala chini ardhini, kunyoshewa vidole yalikuwa yamesha nikomaza. Na sikuwa nikiogopa chochote. Usiku ule nililala chini ya kalvati fulani pale. Maji hayakuwa mengi. Hivyo nikaegemea ukuta nikalala. Kulikuwa na harufu za mikojo sana pale. Ila sikujali.
Asubuhi hii hapa. Nikakurupuka baada ya magari mengi kuyasikia yakipita darajani. Sikuqa na mzigo wowote. Nilikuwa kama nilivyo yani. Mfukoni jumla nilikuwa na elfu 9 au 11 hivi. Nikaulizia stendi ya magari ya Mwanza nikaelekezwa. Nilipofika nikaambiwa ni mapema sana.. labda niende kutafuta hiace za kwenda Kamanga nikavuke niingie Mwanza. Nikasema poa.
Nikapanda hiace mpaka Kamanga. Nikalipia 800 nikavuka, nikafika Mwanza... Kamanga upande wa Mwanza. sasa hapa akili ndio ikafunguka. Yaani shamra shamra nilizokuta pale ukishuka tu kuna watu wanakuonesha pikipiki.. mm kwa kuwa nilikuwa mdogo na mchafchaf sikupata usumbufu. Wale jamaa.. daah.
Hii ni siku ya kwanza jijini Mwanza. Nikafuata njia ambayo niliona wengi wanapitia. Pia wengi nilisikia wakitaja kwa wale bodaboda kuwa wanaenda stendi ya Kisesa pale mjini.
Niliendelea kufuata lami mpaka nikatokea kwenye ile round about yenye samaki anatema maji upande mwingine naona bank ya DTB upande mwngine PPF Plaza, nilikaa pale muda mrefu nikijiuliza nishike njia ipi ukizingatia bado asubuhi nilikuqa na njaa kinoma. Tangu jana nilivoanza safari, nilikula muhogo nilionunua Nyakanazi na maji niliyopewa na abiria mwenzangu.
Pamoja na kuwa na pesa kidogo ya kula sikujua nikanunue wapi msosi.. basi nikashika njia mkono wangu wa kulia baada ya kuona magari mengi yanaelekea huko. Ninachokumbuka niliifuata hiyo barabara mapaka nilipoikuta njia panda nyingine.. kulikuwa na kama bustani watu wengi wamekaa chini. Kuna wengine wanakunywa chai pale.. kuna vijana wanauza maandazi na chai walikuw wanawapimia watu pale. Nikajiunga.. nikanywa chai na maandazi matatu. Nikamuomba huyo jamaa wa chai maji. Akasema hatembei na maji. Nisubiri muuza maji apite ninunue. Nikishangaa bado.. jamaa wa chai akamuita mwingine amebeba ndoo kichwani ya maji yale ya viroba huku Dar wanayaita kandoro.
>>Muedelezo bonyeza kiungo hapo chini
Sehemu ya pili
Sehemu ya tatu
Sehemu ya nne
Sehemu ya tano
Sehemu ya sita
Sehemu ya saba
Sehemu ya nane
Hitimisho
=======================
UPDATE
=======================
Habarini za wakati huu ndugu zangu.
Naanza kutoashukrani zangu za dhati kwa kila mmoja aliyeguswa na mkasa wangu. Kila aliyenipa ole, aliyeshiriki kunipa msaada wa kiutu, kimawazo, na kunitia moyo.
Shukrani zaidi ziende kwa Mubby777 kwa kukubali kunichukua niishi nae. Imani hii na upendo huu, niliamini dunia ya larne hii hawezi kupatikana tena mtu wa aina hii.
Upendo na msaada wa kila mmoja umenifanya nijione mtu mwenye thamani tena baada ya kuishi maisha yangu yote bil kuwaza kesho zaidi ya kutapia ntakula nini nisife.
Aidha, nia yangu kurudi hapa ni kuwakaribisha wooote watakaowiwa na watakaokuwa na nafasi ya kuhudhuria kwenye sherehe ya Mahafali nitakapokuwa natunukiwa shahada ya kwanza ya Sanaa na Elimu (Bachelor of Arts with Education) Katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City, na kisha baadae baada ya taratibu za mahafali tutaelekea GSM MSASANI MALL juu kabisa (floor ya mwisho) kuna mgahawa unaitwa TERRACE ambapo tutakaa hapo tukipata chakula (kila atakayekuja atajilipia sina hela) Tutapata nafasi ya kupiga stori mbili tatu na kufahamiana zaidi kwa wale watakaojisikia.
Nawakaribisheni sana mnipe kampani ndugu zangu. Natanguliza Shukrani zangu za dhati lwa kila mmoja atakayewiwa kuungana na mimi.
Maisha yangu Tangu nikiwa n miaka 9 hayajawahi kuwa ya kawaida. Sehemu kubwa ya Simulizi ya maisha yangu nimeshawahi kuisimulia humu kwenye nyuzi mbali mbali, kwa hiyo nimeona sio vyema kurudia tena. Ila sasa nasimulia maisha yangu baada ya kuzamia Mwanza nikiwa mtoto.
Sikuwa na baba wala mama, tangu nikiwa na miaka hiyo 9. Hivyo, kuna mengi yalitokea baada ya mama yangu kufariki ila kwa mbinde nilimaliza elimu ya msingi mwaka 2008 huko mkoa wa kaskazini magharibi mwa Tanzania.
Nilipata ufaulu mzuri sana wa alama zaidi ya 200 kati ya 250, ila sikuwa na mzazi wala ndugu yeyote. Hivyo sikupata bahati ya kusoma shule ya sekondari. Niliishi kichokoraa pale kijijini, msosi shida, sina hata nguo, halafu kuna dhana iliyojengeka kuwa mimi nilikuwa na mkosi. Kitendo cha kumpoteza mama yangu na kutokuwa na mtu wa ukoo wangu ilikuwa ni kiashiria cha mkosi. Kwamba kila nitakayekuwa karibu nae anaweza pia kufariki au kupata matatizo. Niliishi mpaka nilipopata wazo la kuzamia katika jiji la Mwanza nikatafute maisha.
Baada ya kupata nauli nilipanda gari kuelekea Mwanza. Tatizo likaja kuwa aliyenikatia tiketi alinipandisha gari lisiloenda Mwanza, ila akampa maelekezo kondakta kuwa aniache Runzewe kwa maagent wanifaulishe. Mimi sikuwa najua iwapo ni sahihi au sio. Nikivofika Runzewe nikapandishwa kwenye hiace inayofika geita na nikarudishiwa chenchi. Nilipewa elfu 7. Geita nilifika jioni sana. Sikuwa na pesa hivyo nikatafuta magari ya kwenda Mwanza jioni hiyo hiyo. Nikaambiwa hayapo muda huo. Ila kama nahitaji.. nichukue hiace/mchomoko niende mpaka Sengerema. Kwamba pale itakuwa rahisi kupata gari la kwenda kamanga kabla ya saa tano usiku ambapo ni mwisho wa kivuko.
Mimi sikuwa najua chochote. Nikafuata ushauri. Nikaenda mpaka Sengerema. Nilifika usiku sana.. takriban saa tano na nusu. Gari lilisimamishwa na trafiki muda mrefu njiani.. ndio sababu. Mpaka abiria wakaingilia kati ndio likaachiwa. Kwa watu wenyeji wa barabara hiyo nadhani wanaelewa upkiaji wa abiria kwny ile michomoko, hali ilikuwa tete. Sengerema nilifika nikawa sina ramani. Nilikuwa sipajui, pia gari halikutushushia stendi kwa kuwa ilikuwa usiku. Nikapata wazo.. nitafute sehemu nikae mpaka asubuhi ndio niingie Mwanza. Wakati huo nilikuwa hata sijui ni kitu gani naenda kukifanya Mwanza. Ila niliamini naenda kufanikiwa.
Nilikuwa mdogo sana ila shida nilizopitia tangu utotoni kushinda porini nikichunga mbuzi, kushinda njaa, kulala chini ardhini, kunyoshewa vidole yalikuwa yamesha nikomaza. Na sikuwa nikiogopa chochote. Usiku ule nililala chini ya kalvati fulani pale. Maji hayakuwa mengi. Hivyo nikaegemea ukuta nikalala. Kulikuwa na harufu za mikojo sana pale. Ila sikujali.
Asubuhi hii hapa. Nikakurupuka baada ya magari mengi kuyasikia yakipita darajani. Sikuqa na mzigo wowote. Nilikuwa kama nilivyo yani. Mfukoni jumla nilikuwa na elfu 9 au 11 hivi. Nikaulizia stendi ya magari ya Mwanza nikaelekezwa. Nilipofika nikaambiwa ni mapema sana.. labda niende kutafuta hiace za kwenda Kamanga nikavuke niingie Mwanza. Nikasema poa.
Nikapanda hiace mpaka Kamanga. Nikalipia 800 nikavuka, nikafika Mwanza... Kamanga upande wa Mwanza. sasa hapa akili ndio ikafunguka. Yaani shamra shamra nilizokuta pale ukishuka tu kuna watu wanakuonesha pikipiki.. mm kwa kuwa nilikuwa mdogo na mchafchaf sikupata usumbufu. Wale jamaa.. daah.
Hii ni siku ya kwanza jijini Mwanza. Nikafuata njia ambayo niliona wengi wanapitia. Pia wengi nilisikia wakitaja kwa wale bodaboda kuwa wanaenda stendi ya Kisesa pale mjini.
Niliendelea kufuata lami mpaka nikatokea kwenye ile round about yenye samaki anatema maji upande mwingine naona bank ya DTB upande mwngine PPF Plaza, nilikaa pale muda mrefu nikijiuliza nishike njia ipi ukizingatia bado asubuhi nilikuqa na njaa kinoma. Tangu jana nilivoanza safari, nilikula muhogo nilionunua Nyakanazi na maji niliyopewa na abiria mwenzangu.
Pamoja na kuwa na pesa kidogo ya kula sikujua nikanunue wapi msosi.. basi nikashika njia mkono wangu wa kulia baada ya kuona magari mengi yanaelekea huko. Ninachokumbuka niliifuata hiyo barabara mapaka nilipoikuta njia panda nyingine.. kulikuwa na kama bustani watu wengi wamekaa chini. Kuna wengine wanakunywa chai pale.. kuna vijana wanauza maandazi na chai walikuw wanawapimia watu pale. Nikajiunga.. nikanywa chai na maandazi matatu. Nikamuomba huyo jamaa wa chai maji. Akasema hatembei na maji. Nisubiri muuza maji apite ninunue. Nikishangaa bado.. jamaa wa chai akamuita mwingine amebeba ndoo kichwani ya maji yale ya viroba huku Dar wanayaita kandoro.
>>Muedelezo bonyeza kiungo hapo chini
Sehemu ya pili
Sehemu ya tatu
Sehemu ya nne
Sehemu ya tano
Sehemu ya sita
Sehemu ya saba
Sehemu ya nane
Hitimisho
>>>Pia waweza soma simulizi nyingine ya mtoa mada inayohusu maisha yake ya utototni zaidi: Njooni tukumbuke nyakati ngumu tulizowahi pitia
=======================
UPDATE
=======================
Habarini za wakati huu ndugu zangu.
Naanza kutoashukrani zangu za dhati kwa kila mmoja aliyeguswa na mkasa wangu. Kila aliyenipa ole, aliyeshiriki kunipa msaada wa kiutu, kimawazo, na kunitia moyo.
Shukrani zaidi ziende kwa Mubby777 kwa kukubali kunichukua niishi nae. Imani hii na upendo huu, niliamini dunia ya larne hii hawezi kupatikana tena mtu wa aina hii.
Upendo na msaada wa kila mmoja umenifanya nijione mtu mwenye thamani tena baada ya kuishi maisha yangu yote bil kuwaza kesho zaidi ya kutapia ntakula nini nisife.
Aidha, nia yangu kurudi hapa ni kuwakaribisha wooote watakaowiwa na watakaokuwa na nafasi ya kuhudhuria kwenye sherehe ya Mahafali nitakapokuwa natunukiwa shahada ya kwanza ya Sanaa na Elimu (Bachelor of Arts with Education) Katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City, na kisha baadae baada ya taratibu za mahafali tutaelekea GSM MSASANI MALL juu kabisa (floor ya mwisho) kuna mgahawa unaitwa TERRACE ambapo tutakaa hapo tukipata chakula (kila atakayekuja atajilipia sina hela) Tutapata nafasi ya kupiga stori mbili tatu na kufahamiana zaidi kwa wale watakaojisikia.
Nawakaribisheni sana mnipe kampani ndugu zangu. Natanguliza Shukrani zangu za dhati lwa kila mmoja atakayewiwa kuungana na mimi.