Nilikosea kuolewa na huyu, nimekutana na perfect choice kazini

Sexless

JF-Expert Member
Mar 11, 2017
21,543
50,320
Nimeolewa na mwanaume mwenye sifa zote ambazo kila mwanamke angependa kuwa naye maishani. Tumebahatika kupata mtoto mmoja ndani ya ndoa yetu yenye umri wa miaka 5. Na kwa muda wote huo tumeishi kwa kuheshimiana na kupendana vilivyo.

Mimi na mume wangu sote ni wafanyakazi lakini katika sekta tofauti. Sasa basi, mwaka jana kuna kaka mmoja alihamishiwa kuja kwenye kitengo na kituo ninachofanyia kazi mimi.

Nilipomuona kwa mara ya kwanza tu (first impression ama first glance) moyo wangu ulinienda mbio. Nikajikaza kike na kujitahidi kumpotezea. Kadri siku zilivyoenda na mazoea yalivyoongezeka nikajikuta nafall in love automatically. Sijui kama jamaa aligundua ama la. Lakini alipoonyesha nia sikuwa na namna ya kukataa.

Mapenzi yakaanza mwanzoni mwa mwaka huu, huku nikichukua tahadhari kubwa mume wangu asinikamate. Tulikubaliana kuwasiliana mwisho ni saa 11 jioni na iwe siku za kazi tu ili kujilinda na kukamatwa.

Siku akitaka kuliamsha dude na mimi huwa natoka asubuhi kwangu kama kawaida kama vile naenda kazini kumbe naenda getoni kwa jamaa. Huku kila mtu akiwa ametoa udhuru wake binafai kwa bosi ya kutoenda kazini. Jamaa ameoa lakini kaiacha familia yake alikokuwa mwanzo.

Lakini hivi sasa uzalendo unanishinda, nashindwa kukaa bila kuwasiliana na huyu kaka kutwa nzima hasa weekend. Hivyo huwa natafuta mbinu hata ya kwenda kwenye maduka jirani ama kujifungia chumbani ama kujificha jikoni ama chooni ili tu niongee na huyu kaka.

Kwa hakika najuta kwanini sikukutana na huyu kaka mapema. Ningeolewa naye hata kwa ndoa ya mkeka. Maana sasa mume wangu hata hamu ya kumpa penzi sina. Kama nikimpa basi navuta taswira ya yule kaka wa kazini.

Jamani nifanye nini mimi? Mume wa ndoto yangu bila shaka ni huyu kaka.
 
Kesho nenda kanisani pata muda na Mungu wako...muulize kwanini wewe hapo umemsaliti mumeo ? Na niliapa mbele yako Mungu kwamba nitakua naye huyu na sitashuhulika na wengine na ulichounganisha wewe binadamu mwingine asitenganishe..imekuwaje mimi nimeenda na kimyume na kila kiapo nlichoapa kwako??
Halafu sikiliza majibu
 
Ndiyo mkuu.
Basi jua hata ungepata nafasi ya kuolewa na huyu wa sasa ingefika hatua ungemchoka...kupata mume wa ndoa ni zawadi kutoka kwa Mungu usiichezee kirahisi rahisi hivyo,ukija kufumaniwa na kuachwa ndo utajua thamani ya mume wako maana nakuhakikishia huyo kaka hayupo tayari kuacha familia yake(wanaume hawapendi kirahisi hivyo) hapo kapata pakusuuzia rungu lake maana mke wake yupo mbali,utakapofumaniwa na yeye atakukataa,nani abebe mzigo??? Hapo huna gharama yoyote,uko kwa mume wako



Alafu hivi ingekuwa mumeo ndo anakufanyia hivyo ingekuaje?
Ishinde tamaa ya uzinzi itagharimu maisha yako yote na ya mwanao
 
Nimeolewa na mwanaume mwenye sifa zote ambazo kila mwanamke angependa kuwa naye maishani. Tumebahatika kupata mtoto mmoja ndani ya ndoa yetu yenye umri wa miaka 5. Na kwa muda wote huo tumeishi kwa kuheshimiana na kupendana vilivyo.

Mm na mume wangu sote ni wafanyakazi lkn ktk sekta tofauti. Sasa basi, mwaka jana kuna kaka mmoja alihamishiwa kuja kwenye kitengo na kituo ninachofanyia kazi mm. .

Nilipomuona kwa mara ya kwanza tu ( first impression ama first glance) moyo wangu ulinienda mbio. Nikajikaza kike na kujitahidi kumpotezea. Kadri siku zilivyoenda na mazoea yalivyoongezeka nikajikuta nafall in love automatically. Sijui kama jamaa aligundua ama la. Lakini alipoonyesha nia sikuwa na namna ya kukataa.

Mapenzi yakaanza mwanzoni mwa mwaka huu, huku nikichukua tahadhari kubwa mume wangu asinikamate. Tulikubaliana kuwasiliana mwisho ni saa 11 jioni na iwe siku za kazi tu ili kujilinda na kukamatwa.

Siku akitaka kuliamsha dude na mm huwa natoka asubuhi kwangu kama kawaida kama vile naenda kazini kumbe naenda getoni kwa jamaa. Huku kila mtu akiwa ametoa uzuru wake binafai kwa bosi ya kutoenda kazini. Jamaa ameoa lkn kaiacha familia yake alikokuwa mwanzo.

Lkn hivi sasa uzalendo unanishinda, nashindwa kukaa bila kuwasiliana na huyu kaka kutwa nzima hasa wikendi. Hivyo huwa natafuta mbinu hata ya kwenda kwenye maduka jirani ama kujifungia chumbani ama kujificha jikoni ama chooni ili tu niongee na huyu kaka.

Kwa hakika najuta kwann sikukutana na huyu kaka mapema. Ningeolewa naye hata kwa ndoa ya mkeka. Maana sasa mume wangu hata hamu ya kumpa penzi sina. Kama nikimpa basi navuta taswira ya yule kaka wa kazini.

Jamani nifanye nn mm? Mume wa ndoto yangu bila shaka ni huyu kaka.
Kokote ilipo papachi ilaaniwe kabisaaa!! Wanawake kama wewe ndio mnaotufanya tuchelewe kuoa.
Papuchi na ilaaniwe popote ilipo ilaaniwe kabisaaaa
 
Hapa ndo mnapotukatisha tamaa kuingia kwenye hizo ndoa...hivyo viapo hua mnaweka vya nini sasa ...ni kama kumdhihaki Mungu...binafsi sijapenda unachofanya ila huenda kuna tusichokifahamu zaidi....beyond observation there is reality...
 
MTU anatangaza umalaya mubashara! ka! Huyo mume ana bahati mbaya sana! Hakuna kitu kama mume au mke perfect lakini kuna pair perfect inayoundwa na wanandoa wasio perfect! Hapo kusameheana, kuchukuliana na kuvumiliana ni lazima! Ukishaoa/olewa unaamua kufumba macho usitazame wengine! Shida una macho ya uzinzi! Samahani lakini huo ndio ukweli!
 
MTU anatangaza umalaya mubashara! ka! Huyo mume ana bahati mbaya sana! Hakuna kitu kama mume au mke perfect lakini kuna pair perfect inayoundwa na wanandoa wasio perfect! Hapo kusameheana, kuchukuliana na kuvumiliana ni lazima! Ukishaoa/olewa unaamua kufumba macho usitazame wengine! Shida una macho ya uzinzi! Samahani lakini huo ndio ukweli!
Nimevumilia sana lkn kwa kweli mwenzenu nimezidiwa na hisia za kimapenzi juu ya huyu kaka
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom